Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Sina mamlaka ya kumhukumu mtu na wala sitahukumu, lakini jamii inajiuliza, iweje hawa wawe huru wakati miongoni mwa washtakiwa mahakama ilikiri kuwa walikuwepo waliokuwa eneo la mauaji msitu wa Pande, Mbezi Luis, jiji Dar es salaam siku ya mauaji hayo January 14, 2006.
Wananchi wanajiuliza, imethibitika bila kuacha shaka yoyote kuwa waliouawa hawakuwa majambazi. Imethibitika bila kuacha shaka yoyote kuwa waliouawa walikamatwa wakiwa hai mbele za watu, walifungwa pingu. Imethibitika bila kuacha shaka yoyote kuwa wakiwa hai waliwapeleka msituni Pande, imethibitika bila kuacha shaka yoyote kuwa walirudishwa kutoka msitu wa pande wakiwa maiti.
Katika hukumu yake, Jaji Massati alisema mahakama imeridhika kuwa wafanyabiashara watatu na dereva taksi mmoja waliuawa kwa kupigwa risasi kikatili kwenye msitu wa pande. Hakuishia hapo, alisema kuwa Zombe alikuwa na jukumu la kujua wahalifu walikohifadhiwa baada ya kukamatwa badala yake alifuata fedha. Jaji akanukuliwa akisema, Hapa ni wazi kuwa ni kweli Zombe alijua kilichokuwa kinaendelea! Akawaachia huru.
__________________________
Kunahitajika maoni bila ya jazba kuhusiana na kesi hii ambayo haina shaka yeyote ile kuwa wahusika au washitakiwa wamo ambao wamekiri mauaji haya na hata hivyo wameachiwa huru ,kuna imani kwamba ukinunua kitu cha wizi na wewe utakuwa mwizi namna ya wahusika walivyohusishwa katika kesi hii moja kwa moja na wao watakuwemo katika mkumbo wa mauaji.Kama kuna mtu anaweza kuwaweka sawa watu hawa na kutuonyesha kuwa hawastahili adhabu yeyote ile itakuwa vizuri atuwekee hapa na atufafanulie ili kueneza mwanga kwa WaTanzania walioachwa midomo wazi wakiishangaa Serikali na mahakama zake. Au ni sabotaji ya kuikwamisha serikali ya CCM na kuipa wakati mgumu.
Wananchi wanajiuliza, imethibitika bila kuacha shaka yoyote kuwa waliouawa hawakuwa majambazi. Imethibitika bila kuacha shaka yoyote kuwa waliouawa walikamatwa wakiwa hai mbele za watu, walifungwa pingu. Imethibitika bila kuacha shaka yoyote kuwa wakiwa hai waliwapeleka msituni Pande, imethibitika bila kuacha shaka yoyote kuwa walirudishwa kutoka msitu wa pande wakiwa maiti.
Katika hukumu yake, Jaji Massati alisema mahakama imeridhika kuwa wafanyabiashara watatu na dereva taksi mmoja waliuawa kwa kupigwa risasi kikatili kwenye msitu wa pande. Hakuishia hapo, alisema kuwa Zombe alikuwa na jukumu la kujua wahalifu walikohifadhiwa baada ya kukamatwa badala yake alifuata fedha. Jaji akanukuliwa akisema, Hapa ni wazi kuwa ni kweli Zombe alijua kilichokuwa kinaendelea! Akawaachia huru.
__________________________
Kunahitajika maoni bila ya jazba kuhusiana na kesi hii ambayo haina shaka yeyote ile kuwa wahusika au washitakiwa wamo ambao wamekiri mauaji haya na hata hivyo wameachiwa huru ,kuna imani kwamba ukinunua kitu cha wizi na wewe utakuwa mwizi namna ya wahusika walivyohusishwa katika kesi hii moja kwa moja na wao watakuwemo katika mkumbo wa mauaji.Kama kuna mtu anaweza kuwaweka sawa watu hawa na kutuonyesha kuwa hawastahili adhabu yeyote ile itakuwa vizuri atuwekee hapa na atufafanulie ili kueneza mwanga kwa WaTanzania walioachwa midomo wazi wakiishangaa Serikali na mahakama zake. Au ni sabotaji ya kuikwamisha serikali ya CCM na kuipa wakati mgumu.