Jaguar
JF-Expert Member
- Mar 6, 2011
- 3,440
- 1,029
Siku moja Karim,John na James waliweka kambi jangwani.kila mmoja alikuwa na hifadhi yake ya chakula na maji.Karim alikuwa na chuki ya kisirisiri dhidi ya John,wakiwa wamelala usiku Karim alitia sumu ndani ya chupa ya maji ya John.James naye alikuwa na chuki na john,kabla John hajanywa maji yake,James alitoboa tobo kwenye kitako cha chupa ya maji ya John,maji yote yakavuja.John alipoamka kutaka kunywa maji aliyakosa na hatimaye alikufa kwa kiu.Nani aliyemuua John?James au Karim?