Kesi namba 458 (Jamhuri v JamiiForums) yaahirishwa tena kwa kukosekana Shahidi. Mara ya mwisho kuwa na Shahidi ni Novemba 12, 2018

Kesi namba 458 (Jamhuri v JamiiForums) yaahirishwa tena kwa kukosekana Shahidi. Mara ya mwisho kuwa na Shahidi ni Novemba 12, 2018

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
4,783
Reaction score
14,975
Kesi namba 458 ya mwaka 2016 (Jamhuri dhidi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Jamii Media, Maxence Melo na mwenzake Mike William) imeendelea leo tarehe 23 Machi 2020 mbele ya Hakimu Huruma Shaidi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Katika shtaka la pili kwenye Kesi hiyo, Watuhumiwa wanashtakiwa kwa kuzuia upelelezi wa Polisi kwa kutokutoa taarifa za Mteja aliyeandika taarifa kuhusu Benki ya CRDB ikihusishwa na makato katika miamala zaidi ya inavyotakiwa

Kwa siku ya leo, upande wa Jamhuri umewakilishwa na Wakili Janeth Magoho huku upande wa utetezi ukiwakilishwa na Mawakili Hekima Mwasipu, Benedict Ishabakaki na Hassan Kiangio.

Wakili wa Jamhuri amesema bado hawajapata shahidi wa kuendelea naye katika shauri hili.

Kwa mara ya Mwisho kesi hii kuwa na shahidi Mahakamani ilikuwa mwaka 2018. Na kesi imekuwa ikiahirishwa kwa sababu mbalimbali. Tarehe ya mwisho shahidi kusikilizwa ilikuwa ni Novemba 12, 2018 ambapo Mpelelezi Kitengo cha Upelelezi wa Makosa ya Mtandaoni kutoka Makao Makuu ya Polisi (HQ), Inspekta Beatrice Majule ndiye alikuwa shahidi.

Hakimu Shaidi ameonyesha kutofurahishwa na maahirisho ya shauri hili kwa zaidi ya mwaka na kuutaka upande wa mashtaka kuja na msimamo unaoeleweka kwani anatambua akiifuta washtakiwa watakamatwa na kesi kuanza upya.

Leo kesi imeahirishwa hadi tarehe 23 Aprili 2020.
***

Shauri jingine namba 456 lililo chini ya Hakimu Thomas Simba dhidi yao linatarajiwa kutolewa hukumu mnamo Aprili 02, 2020


Kujua kilichojiri awali kwenye shairi hili na mengine ya JamiiForums, tembelea Muendelezo wa Kinachojiri Kisutu: Kesi za Jamhuri dhidi ya JamiiForums - JamiiForums
 
Mhh hakimu Thomas simba!
JamiiForum jiandaeni tu kulipa faini ya mamilioni kadhaa
 
Serikali hii inavyopenda kesi mpaka inawalazimisha mapolisi wake kuwa mashahidi
Kama police wamekwama, pesa ya kununua wapinzani iliyopo kwa nini wasinipe mimi kidogo tu nikawa shahidi wa upande wa mashitska? Nitachangia kiasi kuwalipia faini washitakiwa kutunisha mfuko wa maendeleo ya wananchi kutekeleza ilani ya chama.
 
Kwa nini haifutwi ikiwa hakuna mashahidi zaidi ya mwaka mzima?
 
Serikali hii inavyopenda kesi mpaka inawalazimisha mapolisi wake kuwa mashahidi
Police ni moja ya law enforcement agencies kusaidia kupeleleza na kutoa ushaidi ni kazi yao,japokuwa baadhi yao wasio na maadili wamenifanya niwachukie wote.
 
Back
Top Bottom