Kesho nchi itasimama, CC ya CHADEMA itakutana!

Kesho nchi itasimama, CC ya CHADEMA itakutana!

Tarajia kishindo kikuu kesho, mwelekeo mpya wa siasa za Tanzania utajipembua.

Kesho Kamati Kuu ya Chama Kikuu cha Upinzani Nchini Tanzania inakaa kitako kujadili mambo kadhaaa ya kisiasa na mwenendo mzima wa nchi,

Chama cha siasa kinachojiandaa kushika dola silaha kubwa ni vikao. Kikao hiki kitaongozwa na Mwenyekiti nguli wa chama hiki Mh Freeman Mbowe.

Na Yericko NyerereView attachment 1057350
Acha mzaha yericko nchi isimame kwa chadema
 
Huku Isunga hakuna mpya,mwenye updates sehemu ambayo nchi imedinda/simama au CC haijakutana?
 
Mkuu Yericko, japo jua limeisha ama, bado tunasubiria, hata kama nchi haijasimama mchana, tutaendelea kusubiria hata usiku, ila kishindo kikuu cha mchana ni tofauti na kishindo kikuu usiku.

Tupe basi update ya CC ya Chadema kusimamisha nchi kwa kishindo kikuu leo, hakuna kulala.
P
Na yeye atakuwa kasimama akikaa ataleta updates

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Yericko, japo jua limeisha zama, bado tunasubiria, hata kama nchi haijasimama mchana, tutaendelea kusubiria hata usiku, ila kishindo kikuu cha mchana ni tofauti na kishindo kikuu usiku.

Tupe basi update ya CC ya Chadema kusimamisha nchi kwa kishindo kikuu leo, hakuna kulala.
P

Haaaahaaaaa.....kazi kweli kweli
 
Mkuu Yeriko, kwanza asante kwa taarifa hii, hivyo na sisi kesho tukae mkao wa kula kusubiria nchi kusimama kwa kishindo kikuu, pili hakuna ubaya wowote kwa mtu yoyote kuwa na too great expectations, kuwa kesho nchi itasimama kwa kishindo kikuu, ila swali la kujiuliza ni kwa Chadema ipi hiyo ya kusimamisha nchi kwa kishindo kikuu ?, kama ndio kwa Chadema hii hii ninayoifahamu mimi, then take it from me, there will be nothing new cha kusimamisha nchi kwa kishindo kikuu kwa sababu kwa sasa karibu top brass yote ya uongozi wa juu wa Chadema, imeshehenezwa na a saturated solution, it can take no more than what it can, hivyo haina watu wenye that capacity ya kuisimamisha nchi kwa kishindo kikuu.

Kama ni kusimamisha nchi kwa kishindo kikuu, ilikuwa ni ile, 2015. Sasa kama mlishindwa pale, kwa sasa there is nothing big you can do cha kusimamisha nchi kwa kishindo kikuu now simply because kumetokea a beast ambae ni game changer, amechange all the political game of this country, and there is nobody and nothing anyone or anybody can do now kwa sababu Chadema toka zamani tuliwaambia humu

https://www.jamiiforums.com/threads...angi-na-hamtajipanga-2015-ni-ccm-tena.624364/

Japo mimi sina chama kabisa lakini kuna vitu huwa nawaambia watu humu na siku nikikutana nao huwa nawaambia face to face mfano

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/87532-ccm-imechokwa;-chadema-haijajipanga.html

https://www.jamiiforums.com/threads...i-zisikilizwe-zizingatiwe-zisipuuzwe.1352784/

https://www.jamiiforums.com/threads...us-credible-mature-enough-opposition.1249668/

Hivyo there will be nothing cha kusimamisha nchi kwa kishindo kikuu zaidi, the only thing kwa Chadema sasa and all serious opposition in Tanzania ni ku open up kwa ushirikiano wa vyama kuungana na kujenga umoja wenye nguvu ili kutengeneza a winning coalition against the giant beast, to start with kutangaziwa Chadema kujitoa iliyokuwa UKAWA na kuanzisha ushirikiano mpya wa Chadema na ACT, na kukaribisha vyama vingine serious opposition na sio vikaragosi.

P
Mwambie huyo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tutaendelea tu kuwashauri hata kama hamtaki. Iwapo mwaka huu mtafanya uchaguzi wa ndani wa chama chenu, mumshauri kamanda Mbowe asigombee kwa mhula wa nne mfululizo hata kama ana nguvu na uwezo kiasi gani ili kuwanyamazisha lumumba na pia kujenga msingi imara wa kuachiana madaraka na kuondoa ile dhana ya kwamba chadema ni ya watu wa kaskazini.

Mpeni John Heche uenyekiti maana alishawahi kuwa mwenyekiti wa bavicha Taifa na alifanya kazi nzuri. Katibu pia abadilishwe na kupewa yeyote yule mwenye haiba kwa wanachama. Pia muanze mkakati wa kujenga ofisi za chama kuanzia makao makuu mpaka vijijini. Mlisha anza kuaminiwa na watanzania wapenda mabadiliko (ushahidi ni uchaguzi wa 2015) na hivyo si vizuri kuwakatisha tamaa kwa kufanya siasa nyepesi nyepesi zinazoenda sambamba na matukio.
Ushauri makini sana.... wakifanya hayo ntachukua kadi ya chadema haraka sana
 
Tarajia kishindo kikuu kesho, mwelekeo mpya wa siasa za Tanzania utajipembua.

Kesho Kamati Kuu ya Chama Kikuu cha Upinzani Nchini Tanzania inakaa kitako kujadili mambo kadhaaa ya kisiasa na mwenendo mzima wa nchi,

Chama cha siasa kinachojiandaa kushika dola silaha kubwa ni vikao. Kikao hiki kitaongozwa na Mwenyekiti nguli wa chama hiki Mh Freeman Mbowe.

Na Yericko NyerereView attachment 1057350
"Chama cha siasa kinachojiandaa kushika dola..."

Hahaha, haya bana.
 
Amini nakuambia wafuasi wa CUF Maalim hawawezi kwenda CHADEMA hata wakihisi ACT imeasisiwa na CCM.

Mizengwe wanyopigwa ACT wasifanye mitihani ya kugawa ni kujaribu kuonesha hakuna upendeleo. Kuonesha no partiality, no double standard kwa vyama vyote hakuna mikutano.

Lakini kiuhalisia CCM wanafanya mikutano bila vikwazo hivyo hii ni partiality, na double standard.

CHADEMA kwa sasa baada ya Maalimy kupeleka wafuasi ACT inapunguza nguvu kubwa ya CHADEMA. Maalim Seif ana wafuasi wengi sana sio Zanzibar tu bali kote hadi huku Tanganyika. Kuna wafuasi wa chadema wa siku nyingi tumeshawaona sasa wanashabikia ACT hii ni sababu ya imani yao kwa Zitto na Maalim Seif.
Mbona akina cuf wafuasi wake wa bara hawakuzidi wa chadema
 
Mbona akina cuf wafuasi wake wa bara hawakuzidi wa chadema
Miaka 12 iliyopita CHADEMA ilikuwa taasisi imara kwa kiasi kikubwa.

Sasa imerudi nyuma hatua kadhaa. Kumbuka kabla ya hiyo miaka CUF ilikuwa juu sana ikashuka.

Sasa wale CUF walioona CHADEMA ndio mbadala wa CUF huku bara na wale CHADEMA asili ambao wanaomuelewa Zitto na wali huzunishwa na kufukuzwa kwake CHADEMA wote wataungana ACT.

Ili dudu la kugawanya kura za upinzani limeundwa makusudi halijatokea kwa bahati mbaya.

Amini nakuambia huu ndio muendelezo wa mwanzo wa mwisho wa CHADEMA ulionzishwa 2015 na ile gia angani ya kumpokea Lowassa na kuwa mwakilishi wa CHADEMA.

Sio kwamba CHADEMA itafutika kabisa ktk uso wa siasa za Tanzania bali itakuwepo kama vile ilivyo NCCR au CUF kwa sasa.

Pattern ni ile ile inayopitia CUF sasa migogoro ndani ya chama utaona pia kifo cha NCCR kilikuja na kuleta migogoro ndani ya chama. NCCR ikabaki kipande na kipande kingine kikaenda kuipa nguvu TLP.

Ndio haya haya ya CUF imegawanyika na kubaki kipande cha Lipumba na kingine kimeenda kuipa nguvu ACT.

CHADEMA hadi sasa inafuata njia hizo hizo. Kuondoka kwa Slaa, kudorora kwa Mashinji, kufukuzwa kwa Zitto na wenzie akina Prof.Kitila, baadae vurugu za Kubenea na Komu ni kama ya CUF yalianza na akina Ahmad Rashid ndio imefikia hapa sasa kwa Maalim Seif.

Kumbuka kufukuzwa kwa mzee alie ibua hoja ya Escrow bungeni toka NCCR Mageuzi ni muendelezo wa yale yale ya mwanzo wa migogoro toka enzi za Mrema na akina Lamwai na Marando.

Hadi Mh.magufili anaondoka CHADEMA itakuwa hoi sio ile tena ya 2008 - 2015.
 
Tarajia kishindo kikuu kesho, mwelekeo mpya wa siasa za Tanzania utajipembua.

Kesho Kamati Kuu ya Chama Kikuu cha Upinzani Nchini Tanzania inakaa kitako kujadili mambo kadhaaa ya kisiasa na mwenendo mzima wa nchi,

Chama cha siasa kinachojiandaa kushika dola silaha kubwa ni vikao. Kikao hiki kitaongozwa na Mwenyekiti nguli wa chama hiki Mh Freeman Mbowe.

Na Yericko NyerereView attachment 1057350
Ndugu yangu Yeriko Nyerere tupe basi mrejesho wa chama nguli na kikao chao cha Jana ambacho kweli nchi ilisimama Kwa kikao chao cha jana
Cc Pascal Mayalla kama ndugu yangu nawe una mrejesho unaweza kumsaidia Ndugu yangu Yeriko
 
Mkuu Yeriko, kwanza asante kwa taarifa hii, hivyo na sisi kesho tukae mkao wa kula kusubiria nchi kusimama kwa kishindo kikuu, pili hakuna ubaya wowote kwa mtu yoyote kuwa na too great expectations, kuwa kesho nchi itasimama kwa kishindo kikuu, ila swali la kujiuliza ni kwa Chadema ipi hiyo ya kusimamisha nchi kwa kishindo kikuu ?, kama ndio kwa Chadema hii hii ninayoifahamu mimi, then take it from me, there will be nothing new cha kusimamisha nchi kwa kishindo kikuu kwa sababu kwa sasa karibu top brass yote ya uongozi wa juu wa Chadema, imeshehenezwa na a saturated solution, it can take no more than what it can, hivyo haina watu wenye that capacity ya kuisimamisha nchi kwa kishindo kikuu.

Kama ni kusimamisha nchi kwa kishindo kikuu, ilikuwa ni ile, 2015. Sasa kama mlishindwa pale, kwa sasa there is nothing big you can do cha kusimamisha nchi kwa kishindo kikuu now simply because kumetokea a beast ambae ni game changer, amechange all the political game of this country, and there is nobody and nothing anyone or anybody can do now kwa sababu Chadema toka zamani tuliwaambia humu

https://www.jamiiforums.com/threads...angi-na-hamtajipanga-2015-ni-ccm-tena.624364/

Japo mimi sina chama kabisa lakini kuna vitu huwa nawaambia watu humu na siku nikikutana nao huwa nawaambia face to face mfano

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/87532-ccm-imechokwa;-chadema-haijajipanga.html

https://www.jamiiforums.com/threads...i-zisikilizwe-zizingatiwe-zisipuuzwe.1352784/

https://www.jamiiforums.com/threads...us-credible-mature-enough-opposition.1249668/

Hivyo there will be nothing cha kusimamisha nchi kwa kishindo kikuu zaidi, the only thing kwa Chadema sasa and all serious opposition in Tanzania ni ku open up kwa ushirikiano wa vyama kuungana na kujenga umoja wenye nguvu ili kutengeneza a winning coalition against the giant beast, to start with kutangaziwa Chadema kujitoa iliyokuwa UKAWA na kuanzisha ushirikiano mpya wa Chadema na ACT, na kukaribisha vyama vingine serious opposition na sio vikaragosi.

P
Post yangu hii bado iko valid
P
 
Post yangu hii bado iko valid
P
Inawezekana mambo sio shwari. Hadi muda huu tupo tunasubiri Press Release ya hicho kikao. Taarifa zisizo rasmi na tetesi zinajitokeza kutoka kwenye vyanzo visivyo aminika, nyoyo zinadunda na wanademokrasia tunaendelea kuvuta uradi. Tunaomba wahusika waondoe hili ombwe na kuondoa mahasidi wasiendelee kutafuta wanayoyataka kutokea.
 
Back
Top Bottom