Kero za vodacom?? Tcra

May 24, 2012
79
54
Nimekuwa nikitumia line ya voda kwa muda wa zaidi ya miaka 12. Nimepoteza hiyo line nikaamua kwenda kurenew pale Vodashop Ubungo Plaza. Ajabu nikaambiwa niorodhesha namba tano (5) nilizopiga mara ya mwisho. Ile line nilikuwa natumia kwenye modem ya voda. Sijaitumia kwa calls kama miezi mitano hivi. Katika namba tano, moja tu ndo imeonekana. Nikaambiwa siwezi kuhuisha line hiyo hadi namba tano zitimie.

Mimi nimeona huu ni ''ujima'' wa hali yajuu sana maana ile line nilishaisajili na kitambulisho nilichotumia kusajili ndio nilikuwa nacho. Si ingetosha kucheki taarifa zangu za usajili na kulinganisha na kitambulisho? Hivi haya mambo ya simu tano yanasaidia vipi,watu tuna mambo mengi sana isitoshe tunapiga simu bila hata kukumbuka umempigia nani maana mtu unakuwa na laini zaidi ya moja.

Hii pia ni kero kubwa jamani....
 
Namba tano inasaidia kujua kama wewe kweli ni mtumiaji wa namba hiyo, unajua mtu anaweza iba kitambulisho chako akaenda renew lain yako akaitumia isivyo.
Anyway ilipaswa waangalie vigezo vingine zaidi ya namba tano incase mtu alikuwa anaitumia kwenye modem tu, wakuulize bundlE gani 3 uliweka mara ya mwisho n.k

hiYo ndio kibongo bongo, mfano crdb benki ukipoteza kadi ya benki unaambiwa upeleke picha, wakati picha yako tayari wanayo!
 
Back
Top Bottom