Kero ya Vodacom na SMS za kamata mpunga

Kero ya Vodacom na SMS za kamata mpunga

harakat

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2011
Posts
2,887
Reaction score
1,359
UJUMBE MUHIMU KWA NAMBA 767xxxxxxxx: Tuma neno GO kwenda 15544 SASA na ushiriki kwenye droo ya TZS 100,000,000 LEO! Vodacom KAMATA MPUNGA!


Hiyo kitu inakera mno kila baada ya muda naona SMS imeingia unakuta ndio hiyo ya kamata mpunga hawa wabadilishe utaratibu wao hii ni kerooooo au tuhamie mitandao mingine
 
Haha wanaboa sana mie kila siku natumiwa kila kukicha.

Internet tununue
Maongezi tununue

Hawatosheki wanatulazimisha tuwape pesa zingine za bure
 
Wananikera sana ata mimi hawa jamaa yani kila ikifika saa tano naona sms yao wananiboa sana.
 
Ni Kero kweli hiyo SMS. mi kwa siku natumiwa Mara mbili na nikiiona tu nafutilia mbali
 
UJUMBE MUHIMU KWA NAMBA 767xxxxxxxx: Tuma neno GO kwenda 15544 SASA na ushiriki kwenye droo ya TZS 100,000,000 LEO! Vodacom KAMATA MPUNGA!


Hiyo kitu inakera mno kila baada ya muda naona SMS imeingia unakuta ndio hiyo ya kamata mpunga hawa wabadilishe utaratibu wao hii ni kerooooo au tuhamie mitandao mingine
Ingefaa kukawa na option ya ku block matangazo usiyoyapenda. Kila sekunde wakinitumia hako katangazo ninakazi ya ku delete na kuguna kimoyomoyo sijui athari zake kiafya zikoje!
 
Wanaboa sana........wataalamu wa masoko husema mpatie mteja kile kitu anachotaka ndipo biashara itakuwa na maana.......sasa wao hizi takataka wanazokazana nazo kututumia katika ujumbe mfupi pumbavu zao nani kawaambia yupo interested na kamali........kama ningekuwa napenda kamali si ningekuwa nafanya betting kila siku maana ndio kamali yenye fursa at least.......sio hizi kamali za kitapeli unatuma meseji halafu unaasikilizia kuitwa kwenye fainal draw ambayo wao wameshampigia simu mshindi wanayemtaka wao ili aje kuigiza kwenye t.v kuwa ameshinda na amefurahi sana.
 
Vodacom noma sana na matangazo yao yanakera mbaya. Siku moja nilikuwa nipo office flan na mmama wa heshima tu....ikaingia number ya vodacom ya yule dada anayesema "hi mimi ni msichana mrembo"......hahahaa yule mama akapokea asijue nani amepiga akasikia hi mimi ni msichana mrembo......teh mama akastuka akamuuliza "who is this please" hakuna jibu manzi anaendelea kubwabwaja.....kuona vivyo mother akajua hawa ni washenzi tu akamtolea bonge la tusi akakata simu....duh nilicheka sana. But all in all Vodacom watoe option kama kublock number zao za matangazo especially adverts zinazoingia daily zinakera aiseee.
 
Mimi juzi niliwapigia Huduma kwa wateja na kuwauliza kulikoni kutuma tuma sms zao zisizo na maana? Wakadai,wazo langu wanalifanyia kazi. Kuanzia siku hiyo sijazipata tena. Nilimkoromea jamaa mpaka mwenyewe akaona sitanii na sitaki ujinga.
Kama mtu hataki ni hataki tu.
Wanaudhi sana hawa majamaa
 
Ingefaa kukawa na option ya ku block matangazo usiyoyapenda. Kila sekunde wakinitumia hako katangazo ninakazi ya ku delete na kuguna kimoyomoyo sijui athari zake kiafya zikoje!
Ipo bhana
 
Nshashinda million mwaka jana so naonaga poa sana tu binafsi na ndo ilikiwa. Mara ya kwanza
 
mimi nimejitia kimbelembele cha kujibu hizo mesej za voda daaaah najuuta
 
Mi kwa kweli line nimeiweka kwenye katecno kadogo kwa silent na hata hicho kicm Sinai nacho muda mwingi kwa kukimbia kero hii Halotel kachukua nafasi kwa line mhm yaani wana upuuzi usiovumilika hata kidogo.
 
TCRA hawamlindi mteja dhidi ya hii kero
 
Huwaga naishiwa pozi nikikutana na sms za voda badala ya sms za madili
 
Mi kwa kweli line nimeiweka kwenye katecno kadogo kwa silent na hata hicho kicm Sinai nacho muda mwingi kwa kukimbia kero hii Halotel kachukua nafasi kwa line mhm yaani wana upuuzi usiovumilika hata kidogo.
Washatuma ujinga huu
375aa84a011a8edd36ae71c73d4a3804.jpg

9b880ef637793a2d8b4cf3b8a2ec97ca.jpg
 
Mi nilidhani peke yangu kumbe tuko wengi tunaokereheka na hiyo mitangazo yao ovyo ovyo
 
Back
Top Bottom