Kenyan crisis: what is next?

Kitila Mkumbo

JF-Expert Member
Feb 25, 2006
3,354
1,943
Kwa mara ya kwanza katika uchaguzi wa kiafrika kila mshikadau sasa amekubali na kukiri kuwa uchaguzi umeibwa. Yaani hata international community ambao hupenda kumumunya maneno kwa kuweka diplomasia sasa wametoka open na kusema Kibaki kaiba. Kimsingi uchaguzi huu umeturudisha nyuma Afrika. Tulikuwa na nafasi nzuri sana ya kuithibitishia dunia kwamba hata sisi waafrika tunaweza kuwa wastaraabu na tukaheshimu maamuzi ya watu. Lakini sasa inawezekana hii tukawa tumeipoteza. Hata hivyo nahisi bado tuna nafasi ya kuonyesha kwamba tunaweza kutatua matatizo yetu kistaraabu bila kupoteza maisha ya watu au angalau kuepusha upotevu wa maisha zaidi. Ni katika hili nawaalika tutoe mawazo yetu juu ya namna ya kuikoa Kenya na umwagaji wa damu na wakati huohuo kupata suluhisho la maana la matatizo ya kisiasa yanayowakabili.

Inawezekana mawazo yetu yasiwe na impact sana kwa yale yanayotokea na yatakayotokea Kenya, lakini najisikia kwamba tunawajibika kuwasaidia wenzetu japo kimawazo juu ya namna ya kutatua hili gogoro ambalo Kibaki ameamua kulitengeneza. Kama ni swala la amani na utulivu nafikiri sisi tuna nafasi nzuri sana ya kusaidia hapa. Je, mnafikiri kwamba tunaweza kuwashawishi hawa ndugu zetu wakakubaliana na ile falsafa yetu watanzania kwamba kama imefikia hatua ya watu kuuawa basi bwana tunakubali yaishe?
Ni wazi kuwa huyu bwana baada ya kuapishwa harakaharaka ndiye sasa ni Rais wa Kenya (ukweli unaouma) na hakuna shortcut ya kumtoa pale.Kuna options mbili kubwa ambazo zipo open kwa wana Kenya na hasa ODM supporters:

i) mtindo wa Ulaya Mashariki: maandamano hadi kieleweke; hii ni nzuri sana, lakini naogopa kwamba kwa sisi waafrika na jinsi majeshi yetu ya polisi yasivyo na utu itakuwa ni ghalika ya damu, watu wengi watauwa, na hapa ndipo nasema hii njia naona kwamba haina tija kwa wakenya wala kwa ODM

ii) Hii ndio naona mimi ni njia sawa. Madamu ODM wana wabunge wa kutosha, watumie nguvu ya bunge. Waende bungeni wabadilishe sheria kandamiza ikiwemo kumnyang'anya Rais madaraka ya kuteua tume ya uchaguzi na kuiacha mikononi mwa Bunge au chombo kingine. Kisha wabadilishe sheria ya vote of no confidence kutoka 2/3 iwe nusu; within few months wa-table kura ya kutokuwa na imani na Rais kwa madai hayohayo ya kwamba aliingia madarakani kinyemela kwa kuiba kura. Nafikiri kwamba hii ni njia nzuri zaidi. Japokuwa inaweza kuchukua muda kidogo lakini itaepusha ile nchi kuingia katika machafuko. Na mara zote ODM wasisitize kwamba haya mapambano sio kati ya Kikuyu na makabila mengine bali kati ya Demokrasia na udikteta. Hii itawavuta wengi zaidi kujiunga nao wakiwemo wakikuyu wanaokerwa na ubakaji wa sanduku la kura.

Inawezekana hii lecture yangu ikawa too late kwa jinsi mambo yanavyotokea Kenya au ikawa useless kabisa na hata mimi kuonekana mwoga kutokana na hasira zilizopo lakini nafikiri kwamba maisha ya watu wa Kenya na nchi yao ni wa maana zaidi na kama kuna njia ya kuepusha vifo basi itumike.
 
Kitila
Hapa inaonekana kuwa it is not only about kuiba kura. It is more than this, kuna mstari wa ukabila unaimzuia Odinga kuingia Ikulu hilo ndio tatizo. Unajua hapa wakiendelea kulealea hii inaweza kuleta precedence mbaya, in my opinion juhudi zote zinatakiwa kufanywa ili ODM wapate haki yao waliyopewa na wananchi wa kenya.
Kama Round table itafanya hivyo well and good, kama violence itafikisha huko well and good. Lakini wakijindanganya kufanya kama Zanzibar watakuwa wanadangayana, unaona jinsi CUF wanavyoibiwa wanadanganywa na muafaka, na muafaka huu utaendelea mpaka 2010, CUF watapigwa mikwaju tena na kuleta muafaka mwingine matokeo yatakuwa yaleyale danganya toto.
Sasa hivi ODM wana kila ground ya kufanya lolote wanalotaka, kwenye international community imewapa greenlight ya kureclaim walichopewa na wananchi. Inaonekana kama PNU wamejifunza ya Tanzania so ni better watumie njia nyingie ya kujipatia haki na sio kama ya CUF!
 
Bongolander: Mawazo mazuri sana. Naelewa wasiwasi wako kuhusu njia hizo ambazo nimependekeza. Lakini nafikiri kuna katofauti kidogo kati ya ushindi wa CUF na ODM. Kumbuka CCM Zanzibar waliiba pia kwenye ubunge kwa hivyo hata huko bungeni (barazani) CUF hawakuwa na majority. Vilevile angalau wizi wa CCM ulikuwa debatable, na kuna watu hadi leo hawataki kukubali kwamba CUF waliibiwa. Lakini hii ya ODM ni tofauti sana (i) wizi umefanyika kweupe na mashuhuda wakaeleza jinsi ulivyofanyika akiwepo mzungu (hii mzee haijawahi kutokea) (ii) ODM wana wabunge wengi kuliko wa Kibaki kwa hiyo maanake wakiamua na kushikamana wanaweza kumfanyia sarakasi ya ajabu sana huyu Kibaki na urais wake ukaonekana ni maigizo ya ukiranja mkuu wa primary school na bado maisha ya watu yakawepo na kenya ikasonga mbele.
 
Kwa mara ya kwanza katika uchaguzi wa kiafrika kila mshikadau sasa amekubali na kukiri kuwa uchaguzi umeibwa. Yaani hata international community ambao hupenda kumumunya maneno kwa kuweka diplomasia sasa wametoka open na kusema Kibaki kaiba. Kimsingi uchaguzi huu umeturudisha nyuma Afrika. Tulikuwa na nafasi nzuri sana ya kuithibitishia dunia kwamba hata sisi waafrika tunaweza kuwa wastaraabu na tukaheshimu maamuzi ya watu. Lakini sasa inawezekana hii tukawa tumeipoteza. Hata hivyo nahisi bado tuna nafasi ya kuonyesha kwamba tunaweza kutatua matatizo yetu kistaraabu bila kupoteza maisha ya watu au angalau kuepusha upotevu wa maisha zaidi. Ni katika hili nawaalika tutoe mawazo yetu juu ya namna ya kuikoa Kenya na umwagaji wa damu na wakati huohuo kupata suluhisho la maana la matatizo ya kisiasa yanayowakabili.

Inawezekana mawazo yetu yasiwe na impact sana kwa yale yanayotokea na yatakayotokea Kenya, lakini najisikia kwamba tunawajibika kuwasaidia wenzetu japo kimawazo juu ya namna ya kutatua hili gogoro ambalo Kibaki ameamua kulitengeneza. Kama ni swala la amani na utulivu nafikiri sisi tuna nafasi nzuri sana ya kusaidia hapa. Je, mnafikiri kwamba tunaweza kuwashawishi hawa ndugu zetu wakakubaliana na ile falsafa yetu watanzania kwamba kama imefikia hatua ya watu kuuawa basi bwana tunakubali yaishe?
Ni wazi kuwa huyu bwana baada ya kuapishwa harakaharaka ndiye sasa ni Rais wa Kenya (ukweli unaouma) na hakuna shortcut ya kumtoa pale.Kuna options mbili kubwa ambazo zipo open kwa wana Kenya na hasa ODM supporters:

i) mtindo wa Ulaya Mashariki: maandamano hadi kieleweke; hii ni nzuri sana, lakini naogopa kwamba kwa sisi waafrika na jinsi majeshi yetu ya polisi yasivyo na utu itakuwa ni ghalika ya damu, watu wengi watauwa, na hapa ndipo nasema hii njia naona kwamba haina tija kwa wakenya wala kwa ODM

ii) Hii ndio naona mimi ni njia sawa. Madamu ODM wana wabunge wa kutosha, watumie nguvu ya bunge. Waende bungeni wabadilishe sheria kandamiza ikiwemo kumnyang'anya Rais madaraka ya kuteua tume ya uchaguzi na kuiacha mikononi mwa Bunge au chombo kingine. Kisha wabadilishe sheria ya vote of no confidence kutoka 2/3 iwe nusu; within few months wa-table kura ya kutokuwa na imani na Rais kwa madai hayohayo ya kwamba aliingia madarakani kinyemela kwa kuiba kura. Nafikiri kwamba hii ni njia nzuri zaidi. Japokuwa inaweza kuchukua muda kidogo lakini itaepusha ile nchi kuingia katika machafuko. Na mara zote ODM wasisitize kwamba haya mapambano sio kati ya Kikuyu na makabila mengine bali kati ya Demokrasia na udikteta. Hii itawavuta wengi zaidi kujiunga nao wakiwemo wakikuyu wanaokerwa na ubakaji wa sanduku la kura.

Inawezekana hii lecture yangu ikawa too late kwa jinsi mambo yanavyotokea Kenya au ikawa useless kabisa na hata mimi kuonekana mwoga kutokana na hasira zilizopo lakini nafikiri kwamba maisha ya watu wa Kenya na nchi yao ni wa maana zaidi na kama kuna njia ya kuepusha vifo basi itumike.

Kitila,

Asante sana kwa hii thread.

Mimi mwenyewe nimekuwa na very antagonizing night kuhusu hili swala. Kwa bahati nzuri au mbaya ninaifahamu jiografia ya kenya kwa kiwango fulani kutokana na sababu nyingi.

Mauaji yanayoendelea sasa hivi kenya sio dhidi ya wakikuyu kama watu wanavyodhani. Ukisoma miji ambayo mauaji yanatokea ni kule ambako kama kuna wakikuyu walishaondoka zamani sana.

Mji wa Kisumu ni centre ya wajaluo. Once ulikuwa one of the best around lake nyanza. Hizi picha za mioto na figure za bbc kuwa zaidi ya watu 50 wamekufa nyanza ni habari mbaya kwa ODM. Mji wa mombasa sina cha kueleza zaidi kwani nadhani wengi mushafika huko. Hizi picha zo mioto na namba ya watu zaidi ya 50 wa kutoka mombasa wamekufa zinatisha.

Kibera ile na Mathare ni mixed lakini wakikuyu walishakimbia saa nyingi sana. Eldoret ni mixed city ya wakikuyu na kalenjin lakini sidhani kama kikuyu bado wako huko. Kwa sasa imebaki ni vita dhidi ya ODM na polisi. Polisi wanapiga risasi za moto for whatever reasons wanajua wao. Wanaokufa sasa hivi ni wana ODM na kama ulisikia BBC ya jana, watu wa nyeri (kikuyu) na meru (wameru) na baadhi ya towns za wakamba wao wanasherehekea ushindi na kunywa na kulewa.

Nakubaliana nawe kuwa for the sake of our people and the future of Mombasa, Kisumu, Eldoret, Nakuru nk watu wa kenya wachoose your second option. Waafrika tuliungana tukawatoa makaburu huko Afrika kusini. Tunaweza tena kuungana na kuwatoa hawa makaburu weusi tukishajipanga vizuri kwa kuanza na kibaki na mugabe and the rest of them.

Inauma lakini maisha ya wana ODM wanaokufa sasa hivi yawe ni muhimu sana kuliko long term strategy. Haya ni maoni yangu tu.
 
Katika kipindi cha miaka mitano ya kibaki tutegemee mauaji ya kutisha nchini Kenya,kuna taarifa zisizokuwa rasmi kwamba jeshi limeshasema lina muunga mkono Raila Odinga na kwamba mzee Kibaki amejibanza Mombasa huku Moi akiwa Afrika ya Kusini.Hayo yakiendelea watu sitini wameuawawa soma hapa nchini

www.bbc.co.uk/swahili/news/story/2007/12/071227_kenya_elex2.shtml
JESHI HALIJASEMA LITAMUUNGA MKONO RAILA.bigman acha kutupotosha.Mareakani wamempongeza Odinga kwa kuwa RAis wa Kenya,Na Pongeza zinazidi kumiminika ikiwamo ya Mugabe,
 
NAIROBI, Kenya (CNN) -- At least 124 people have reportedly been killed in violence sparked by allegations of vote-rigging in Kenya's disputed presidential elections.


A looter carries clothes he stole past a burning shack in the Kibera slum of Nairobi.

1 of 4 more photos » Kenya's national broadcaster KTN reported the death toll on Monday following two days of violence across the African nation, from Nairobi's shantytowns to the tourist-friendly coast.

Earlier, media reports said 46 bodies were taken overnight to a morgue in the western Kenyan city of Kisumu -- its third largest city and a bastion of defeated opposition challenger Raila Odinga.

Police fired warning shots and tear gas at opposition protesters in Nairobi on Monday, a day after President Mwai Kibaki was controversially returned to power.

Several officers, who spoke to The Associated Press on condition of anonymity for fear of reprisals, said they were ordered to shoot to kill to halt the violence.

However, a government spokesman insisted that no such order was given, AP reported.

The streets of the Kenyan capital were almost deserted Monday as the government deployed riot police to quell opposition supporters, some of whom said they would risk death to protest what they called a stolen election.

"We have been rigged out, we are not going to accept defeat," 24-year-old James Onyango, who lives in Nairobi's Kibera slum, told AP. "We are ready to die and we're ready for serious killings."

Small bands of Odinga supporters were stopped from making their way to a rally in Uhuru Park -- a traditional site for political demonstrations in the center of the city. The rally was called by Odinga, who accused Kibaki of "doctoring" the vote after narrowly losing out to his rival.

Odinga told CNN on Monday that Kenyans were "in a state of mourning" following the result. "They are mourning the loss of democracy," he said.

Businesses in the city were shut down and a government ban on live television broadcasts imposed Sunday was still in place as Kibaki struggled to cope with the fallout from the vote.

A member of staff in the Imperial hotel in Kisumu told CNN by telephone that a curfew was in force on the streets.

The woman, who did not want to be named, said the city center was deserted except for armed police patrols. She said she and other hotel staff had been forced to sleep in the hotel overnight after police threatened to shoot on sight anyone who breached the curfew.

"I have not been home to my family. We do not know what is happening," she said.

A Kenyan woman interviewed by CNN on the streets of Nairobi said: "It's dictatorship. Can't you see that?"

Witnesses told CNN of widespread violence in the Nairobi slum of Kibera as angry Odinga supporters set fire to buildings and clashed with police.

Don't Miss
Kenya counts millions of ballots
Local media reported a number of deaths as a result of the rioting, as well as reports of police brutality.

The most closely fought election in Kenya's history threatened to unravel Sunday as opposition officials shouted down the electoral commission chairman as he tried to announce the result.

The official count put Kibaki narrowly ahead of Odinga of the opposition Orange Democratic Movement -- 4,584,721 votes to 4,352,993.

The result was immediately called into question, however, with election observers from the European Union saying they had doubts about the legitimacy of the count.

British Foreign Secretary David Miliband said in a statement Sunday that Britain had "real concerns at the irregularities reported by the EU observers and others."

One international observer, who did not wish to be identified, told CNN that the vote count was "clearly cooked."

Analysts said, however, that it was probable that both of the main parties had been involved in electoral fraud.

Thomas Cargill, a specialist on African politics at the British think tank Chatham House, said it was difficult to imagine Odinga giving up his claims for the presidency without a fight.

"It is very worrying," Cargill told CNN.

Kibaki was sworn in hurriedly Sunday in a ceremony at the presidential palace. His slim margin of victory is a marked difference from his win five years ago, in a landslide election. He had run on promises to fight corruption.

Since, he has seen his authority erode amid a number of high-profile corruption scandals in his government.

He faced a serious challenge from Odinga, a flamboyant politician who hails from the minority Luo tribe and has won support from the rural and urban after promising to share the wealth among all the people.

A peaceful election and a smooth transition of power were seen as crucial for Kenya, a stable country in an otherwise-volatile region
 
Hivi jumuia ya Afrika Mashariki haikuwa na observers huko? Hawa wangeprovide cover kwa Kibaki kama wanavyofanya wenzao wa SADC kwa Mugabe!
 
Hivi jumuia ya Afrika Mashariki haikuwa na observers huko? Hawa wangeprovide cover kwa Kibaki kama wanavyofanya wenzao wa SADC kwa Mugabe!

Fundi,
Kuna vinavyo wezekana kuwa covered vingine viko wazi mno! Vinginevyo ni kujitumbukiza katika aibu na migogoro isiyo kuhusu!

The best thing they can do is to stand for the obvious truth!
 
Fundi,
Kuna vinavyo wezekana kuwa covered vingine viko wazi mno! Vinginevyo ni kujitumbukiza katika aibu na migogoro isiyo kuhusu!

The best thing they can do is to stand for the obvious truth!

Wachunguzi wa Africa Mashariki wapo huko Kenya. Hawakutegemea waliyoyaona ni aibu maana taarifa walizokuwa wakitoa Raila alikuwa ameshinda na taarifa hizo zipo ikulu za Marais wetu Uganda na Tanzania. Kukaa kwao kimya bado ni ujinga unaolelewa hapa Africa na wala hamna maana ya kamati hizi maana zinafanya kazi kwa uwoga wa kidiplomasia badala ya kusimamia haki ya wanajumuia. Sasa kama wao wapo kwa ajili ya maslai ya serikali zao ni nini faidi ya wao kuwepo?

Kifo ni kitu kibaya, lakini kudai haki ni jambo la msingi. Kuna Waafrika wengi waliuwawa wakati wa kutafuta uhuru, je, tuwalaumu wale wote waliyoanzisha harakati hizo za uhuru? La hasha, waliyokufa kwetu ni mashujaa. Hivyo ndugu zangu damu ya wana ODM haipotei bure bali inajenga historia ya mapambano dhidi ya udharimu wa democrasia. Kibaki ni mkenya just like other Kenyan. Ni mtu mwenye kwao na ndugu zake na pale Ikulu ni mahali panapomilikiwa na Wakenya wote. Ni mahala patilivu, penye heshima, ulinzi, magari na uduma zote za msingi pengine kuliko mahala pengine Kenya hivyo kuweka utaratibu wa nani aishi hapo na wanakubaliana kuwa wakenya washiriki kumteuwa mtu huyo. Kibaki baada ya kuona wakenya wanamtoa Ikulu akaamua kuingia kwa njia zake Mwenyewe. Ni kwa nini wakenya wasipiganie heshima ya Ikulu maana kazi ya Kibaki ikulu imekataliwa na wakenya.
Pole Kibaki upo ikulu na DONDA KUBWA LISILOPONA. Miaka yote umekuwa ktk siasa tangu miaka ya 60 lakini hitaji lako la miaka mitano imefuta mengi mazuri yako ya miaka mingi ktk siasa za kenya. POOR PRESIDENT. Na sasa wakikuyu wanakupinga maana hawakutegemea ushinde kwa wizi wa wazi.
 
Back
Top Bottom