Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,172
Pamoja na Celina Kombani kuongopa ya kuwa nafasi ya raisi katika katiba mpya kutuchagulia waandishi wake na huku akijigamba na mifano ya Ghana na Kenya lakini ukweli unamuumbua kwa sababu kenya Raisi kazi yake ni kuthibitisha majina baada ya mfumo wazi wa kupata viongozi umefanyika.............................iwe ni Tume ya uchaguzi, iwe ni majaji, iwe ni nafasi yoyote ile ikiwemo ya kuandika katiba mpya...................nafasi hutangazwa magazetini na kutoa fursa sawa kwa raia wote kushiriki katika kuziomba nafasi hizo........................kwenye baadhi ya nafasi tume husika huchekecha majina na kuyapeleka bungeni kwa uthibitisho na baada ya bunge kuyathibitisha basi raisi hufanya uteuzi................hapa teuzi ni siri ya Raisi.............na hakuna demokrasia shirikishi.............mtanzania mwenye sifa lakini hajuani na Raisi au vikaragosi wake kamwe hatapewa nafasi sawa................................katika teuzi za Raisi........................matokeo yake ni bora viongozi badala ya kuwa uongozi bora...........Hongereni Kenya na Tanzania tupende tusipende.................the future lies in photocopying Kenyan constitutional example....................tusipofanya hivyo tununue vifaru vingi......................maji pilipili kibao...................mabomu ya machozi lukuki...........................ili kuzima azma halali ya watanzania kushirki katika kujiletea maendeleo yao wenyewe....................taasisi ya Uraisi imeshindwa kutuletea maendeleo yetu wenyewe katika miaka 50 iliyopita kwa nini tuendelee na uozo uleule?