Zero Hours
JF-Expert Member
- Apr 1, 2011
- 12,944
- 18,654
Kenya mjini kisumu, umeanzishwa msikiti mpya wenye jina la " The Mosque of Jesus Christ the son of Mary".
Hii imetoa gumzo kubwa hasa kwenye mitandao wa kijamii huku wengi wakihoji huu ni msikiti au kanisa.
Abdul Rashid ambaye ni Mwadhini wa msikiti huo, alihojowa na gazeti la The Standard la Kenya na kusema kuwa '' Tumekuwa na mvutano wa muda mrefu kuhusu ardhi na hii ni moja ya sababu zilizotufanya kuchagua jina hili. Sisi hatuna uadui na Wakristo,'' alisema.
Amesema kuwa Waislamu pia wanaamini Yesu na kuwa alikuwa sambamba na manabii wanne akiwemo Mtume Muhamad (S.A.W).
''Waislamu wanaamini katika Yesu Kristo . Uchaguzi wa jina pia ni shukrani ya Yesu Kristo ambaye tunaamini atarudi tena," Rashid aliliambia gazeti la The Standard.
Mipango ya kujenga msikiti wa kudumu inaendelaa ingawa Waislamu wanaoabudu kwenye eneo hilo wamejenga jengo la muda mfupi kwa ajili ya kuswali.
Baadhi ya waumini wa Kikristo wamepokea kwa mikono miwili hatua hii wakisema kuwa itajenga hali ya kuishi kwa amani.
Hili si tukio geni hata hivyo kwani jina la The Mosque of Jesus Christ" limepewa pia Msikiti ulio katika mji wa Madaba, Kusini mwa mji mkuu wa Amman huko Jordan, Msikiti huu ulianzishwa mwaka 2008 kwa ajili ya kutoa ujumbe wa umoja na kustahimiliana miongoni wa dini hizo mbili.
Source:BBC swahili.
Hii imetoa gumzo kubwa hasa kwenye mitandao wa kijamii huku wengi wakihoji huu ni msikiti au kanisa.
Abdul Rashid ambaye ni Mwadhini wa msikiti huo, alihojowa na gazeti la The Standard la Kenya na kusema kuwa '' Tumekuwa na mvutano wa muda mrefu kuhusu ardhi na hii ni moja ya sababu zilizotufanya kuchagua jina hili. Sisi hatuna uadui na Wakristo,'' alisema.
Amesema kuwa Waislamu pia wanaamini Yesu na kuwa alikuwa sambamba na manabii wanne akiwemo Mtume Muhamad (S.A.W).
''Waislamu wanaamini katika Yesu Kristo . Uchaguzi wa jina pia ni shukrani ya Yesu Kristo ambaye tunaamini atarudi tena," Rashid aliliambia gazeti la The Standard.
Mipango ya kujenga msikiti wa kudumu inaendelaa ingawa Waislamu wanaoabudu kwenye eneo hilo wamejenga jengo la muda mfupi kwa ajili ya kuswali.
Baadhi ya waumini wa Kikristo wamepokea kwa mikono miwili hatua hii wakisema kuwa itajenga hali ya kuishi kwa amani.
Hili si tukio geni hata hivyo kwani jina la The Mosque of Jesus Christ" limepewa pia Msikiti ulio katika mji wa Madaba, Kusini mwa mji mkuu wa Amman huko Jordan, Msikiti huu ulianzishwa mwaka 2008 kwa ajili ya kutoa ujumbe wa umoja na kustahimiliana miongoni wa dini hizo mbili.
Source:BBC swahili.
Kwanini 'Msikiti huu ukaitwa jina la Yesu Kristo? - BBC News Swahili
Ilianzia katika mvutano wa kisheria kati ya jumuia ya Kiislamu na Kanisa la Waadventista wa Sabato (SDA) kuhusu umiliki wa ardhi.
www.bbc.com