Kenya mshahara wa rais uko wazi

Kenya mshahara wa rais uko wazi

So what? Corruption is everywhere. Important is they are trying to be transparent about how public funds are spent. In Tanzania everything important for public knowledge is a big secret, and this makes me sick to the gut!!
Uko sahihi

Sent from my TECNO L8 Lite using JamiiForums mobile app
 
Pendekeza na huku maana huku ndio tuna rais mzalendo kuliko Kenya. Huku ndio hilo wazo litapita kirahisi maana hii ni serekali inayojali wanyonge. Huenda ww ukasikilizwa maana sasa hivi huwa unawatetea sana, sisi tunapinga kila kitu hatutasikikizwa.

Nimeanza kuhoji kuhusu mshahara wa rais zaidi ya miaka 10 iliyopita.
 
Jana tume ya mishahara [ya watumishi wa umma] ya Kenya imetangaza viwango vipya vya mishahara ya viongozi wa umma.

Viwango hivyo vipya ni vidogo kidogo kulinganisha na viwango vya sasa.

Kwa hiyo, rais mpya ajaye baada ya uchaguzi wao wa mwezi ujao ataanza kupokea huo mshahara mpya.

Na kama Uhuru Kenyata akishinda basi ina maana mshahara ataopokea kuanzia mwezi Septemba utakuwa ni pungufu kuliko apatao sasa.

Tofauti na huku kwetu ambapo kuna wapumbavu ukiulizia mshahara wa rais wanakwambia 'mshahara wa mtu ni siri'.



Kuna yule tuliambiwa akitoka Chato atatoa salary slip yake mhhhh mpaka leo imebaki historia, Afrika civilization ni msamiati mgumu sana!
 
Nyani, kumbuka kipindi kile yupo chato likizoni, alisema akija atataja mshahara wake, tulisha sikia tena? Na watu wanasema mshahara wa Rais Tz ni mkubwa sana. Nadhani kwa Afrika Tz ni ya tatu kwa mshahara mnono wa Marais. Ngoja tuendelee na uzalendo huu tuliouanzisha

Inapaswa kuwepo na sheria inayolazimisha uwazi wa malipo ya viongozi wote wa umma.

Sasa hivi sidhani kama ipo.

Kwa yeye kusema atautaja mshahara wake kwetu hiyo ni hisani tu.

Inapaswa iwe lazima kisheria.
 
Inapaswa kuwepo na sheria inayolazimisha uwazi wa malipo ya viongozi wote wa umma.

Sasa hivi sidhani kama ipo.

Kwa yeye kusema atautaja mshahara wake kwetu hiyo ni hisani tu.

Inapaswa iwe lazima kisheria.
Siyo viongozi tu hata watumishi wengine
 
Inapaswa kuwepo na sheria inayolazimisha uwazi wa malipo ya viongozi wote wa umma.

Sasa hivi sidhani kama ipo.

Kwa yeye kusema atautaja mshahara wake kwetu hiyo ni hisani tu.

Inapaswa iwe lazima kisheria
Na hapo karibia makatibu wakuu, manaibu katibu wakuu, mawaziri na manaibu ni PhD holders wrote!! Huwa najiuliza wanafanya kazi gani huko? Kusaini vocha na cheque na kupitisha madokezo!!? Maana kila juhudi anaanzisha Rais yenyewe yanafyata!
 
Pombe si alisema atatuonesha salary slip yake mbona jiiiiiiii hadi leo

From Magogoni
 
Tanzania hata wa diwan haujulikan

[Color= yellow]Triple A[/color]
 
Mshahara wa Raisi ni danganya toto tu kwasababu Raisi aishi kwa kutumia mshahara wake. Sisi watu weusi ni wepesi kudanganyika. Hata ukimpunguzia Raisi mshahara wake hauwezi kuboresha maisha ya watu wengine ambao wengi ni masikini. Hali kadhalika ata ukiwashusha mishahara watumishi wote kiasi kitakachopatikana hakitawasaidia wananchi wa kawaida. Kwasababu kwa kupitia mishahara ya hao ajira ndogo ndogo zinapatikana na kinyume chake ni majanga. Kimsingi, huwezi kuboresha maisha ya raia wako kwa kushusha vipato vya raia wengine ( pathetic). Tunataka tuwe na viongozi visionary, wanaoweza kuboresha maisha ya watu kwa kuwa wabunifu. Hizi drama za kushusha mishahara ni alama kwamba uwezo wetu wa kufikiri ni mdogo na umefikia mwisho.
 
Budget ijayo anapunguza mshahara wake (rais) pia kuna punguzo la mishahara ya wafanya kazi serikalini including you.. Upo tayari?
 
Back
Top Bottom