Usijali mkuu, ukiona uko sehemu hawaithamini value yako wala hata usiwasanue. We anza kutafuta chaka jingine kimyakimya.
Mimi iliwahi nitokea kipindi flani nikifanya kazi sehemu. Offcourse nilibargain mshahara kizembe na sababu kubwa ilikuwa ni njaa kali iliyokuwa ikinikabili kitaa. Baada ya miaka minne kazini ikatokea mdau mmoja karesign kwenye position ambayo ni ya juu kidogo. Nakumbuka kiongozi wangu aliulizwa na director whether wanipromote au waajiri mtu mwingine akasema waajiri mtu kwa sababu mimi bado sitoshi kwenye hiyo nafasi meanwhile mimi ndie niliyekuwa natekeleza majukumu yote yake na ya kumtumia report ambazo alikuwa anaenda kupatia ujiko kwenye management. Huyo mwamba alivyoresign ni mimi pia nilipewa majukumu yake na nilikuwa nafanya kazi kama punda vile.
Basi bwana ikafanyika interview jamaa akamkingia kifua nadhani manzi yake kipindi akiwa chuoni akapata hiyo nafasi. Kiroho safi kafika nkaambiwa nimfundishe kazi. Haloo manzi alikuwa mweupe kupita maelezo kiasi kwamba kiongozi wangu akawa ananipa majukumu yake. Yaani akawa kama bosheni tu ofisini.
Mungu sio Athumani nikapataga chaka moja nafasi kama ya kiongozi wangu tena kwa mshahara wa zaidi ya mara 3 ya mshahara wa kiongozi wangu. Nikaandika barua ya kuresign mwezi mmoja kabla. Saa ngapi nisiitwe na director ati kiongozi kamwambia aniite tuje tudiscuss kuboreshewa maslahi yangu ili nisiende kwenye ajira mpya. Asee niliwagomea katakata, yaani sikutaka kusikia la mtu.
Ni miaka mitatu imepita sasa, yule manzi alishatimuliwa kwa kuunderperform na kiongozi wangu kashaletewa bosi wake maana utendaji ulilegalega kwenye nafasi yake.
Kupitia kisa changu nakushauri usikate tamaa na ongeza juhudi kwenye kazi yako, ila usiache kutafuta chaka jipya. Na ukilipata usiende kinyonge kabisa kwenye kubargain maslahi. Mungu ni mwema utatoboa maana uwezo huwa hauongopi. Kila lakheri mkuu.
Angalizo:
Usijihusishe na kitendo chochote cha fitna kutokana na uchungu ulionao hivyo hufanya wivu usio na faida.