Haya matatizo yanaletwa na watu wanao husika na mshahara kutokuwa wa siri! Mshahara wa mtu ni siri ya mtu aya mambo ndo yataleta uchawi apo
Shida ni mwenzako kulipwa kukuzidi au Shida ni mshahara mdogo?
Anyway akimpunguzia mkaliwa sawa kwenye makaratasi utaridhika?
Mambo ya connection hayo,kama umeshindwa kuendana na hali tafuta kazi ingine otherwise kubali uhalisia
Sent from my HUAWEI MLA-AL10 using JamiiForums mobile app
Usijali,utaanza hata na biashara ya Vigogo utaviuza katika viwanda vya wachina,angalau uwe na M1 kwa kuanzia sio mbaya. Then utakuja huku katika mbao Mzee.mmh! Sio rahisi ivo ,una saw mill yako? Una nunua miti mwenyew?
Ukiacha roho mbaya mambo mazuri yatakuja tu upande wako. Kwa ufupi wewe umeshaonekana boya na ukiendelea na ujinga watakufukuza kazi.
Mshahara wa mtu mwingine haukuhusu, akili kama za Feitoto yani.
Alete kwanza CV yake na CV ya huyo anayemlalamikia.
Kuna wajinga bado hawajui mtu anaweza kukuzidi madaraka na wewe ukamzidi mshahara.
Mwalimu mkuu wa shule anaweza kuzidiwa mshahara na Mwalimu wa kuwaida ambaye hana Madaraka.
Hii imeendaaaaUtakua uko kwa wahindi na huyo staff mwingine ni muhindi mwenzao.
hili jibu zuri sanaNjoo Mufindi tuchane mbao Kaka,achana na masuala ya kuajiriwa ajiriwa.
Sent from my M2006C3MG using JamiiForums mobile app
Mshahara haujawahi kutosha hata siku moja,acha kuangalia au kufuatilia mishahara ya wenzako,Shida mshahara ni mdogo
Usipoacha hiyo tabia utafutwa kazi soon.analipwa salary kubwa kuliko mimi na ni gap kama la 950k hivi ila mara nyingi kazi mimi Ndio namwelekeza na mara nyingi pia huwa naulizwa. Mimi moyo yea kufanya kazi haupo kabisa naona kazi ngumu Halafu mwenzangu analipwa vizuri.
Fanya hivi ukiiva omba kuongezewa mshahara ukiona wanakuletea mapichapicha nenda katafute kwingineChapa kazi kama vile unafanya kazi bure ili upate experience usepe
Acha wivu wa kijinga nenda kasomeHabarini wanajamii,niende moja kwa moja kwenye changamoto yangu.Nimeajiriwa kwenye taasisi moja hapa jijini dar,sasa katika ajira yangu kitengo nilichopo tulikuwa wawili mimi na huyo niliyemkuta yeye mwenzangu alikuwa kanitangulia kama miaka miwili pale kazini japo tulikuwa level moja ila kiwango cha mshahara alikuwa ananizidi kwa gap kama 800k kabla ya makato.
Baada kama ya mwaka mmoja jamaa aliondoka baada ya kupata kazi nyingine so pale nikabaki mwenyewe na baada kama ya miezi miwili akaletwa mtumishi mwingine,changamoto inakuja yeye analipwa salary kubwa kuliko mimi na ni gap kama la 950k hivi ila mara nyingi kazi mimi Ndio namwelekeza na mara nyingi pia huwa naulizwa. Mimi moyo yea kufanya kazi haupo kabisa naona kazi ngumu Halafu mwenzangu analipwa vizuri.
Hebu wakuu mnisaidie katika hali hiyo nifanye nn?