Kazi za kuitwa kibarua kinapotokea zina maslahi mazuri? Hasa kwa mafundi

hilker mhema

Member
Mar 20, 2017
81
23
Wakuu habari za leo, naombe kuuliza.
Kuna kampuni ya ujenzi wa minara ya simu ilitoa nafasi ya kutrainee vijana waliosoma halafu itaanza kuwatumia kutokana na tenda zinavyokuja.
But wao kama wao wakasema hiyo kampuni haiajiri bali itamtumia huyo mtu kutokana na kazi zinazotokea kwenye kampuni.
Ikitokea kuna kupandisha antena site fulani basi watakuita then utaifanya hiyo kazi na ukimaliza basi subiri uitwe siku nyingine.

Wazoefu wa hizi sector/kama umewahi kutana na hii scenario je hizi kazi zinalipa? Au je kuna uhakika wa kupata permanent job hapo?
Na je ikitokea umepata nafasi ya kazi ya kuwa broadcast technician wa redio fulani kipi bora kubaki trainee au kwenda kwenye nafasi ya kazi yenye mkataba(broadcast technician)?

Natanguliza shukrani wakuu
 
Back
Top Bottom