Kaulimbiu ambazo kilimo chetu kimepitia

Kaulimbiu ambazo kilimo chetu kimepitia

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,650
Reaction score
21,011
Nimesikia kuwa PM Majaliwa amewaagiza mawaziri wa kilimo, biashara na mwingine gani sijui, wakae na kuja na mpango kwaajili ya kilimo. Nawaza sijui watakuja na kaulimbiu gani. Hii ni historia fupi ya kaulimbiu za kilimo.

1.Siasa ni kilimo, azimio la Iringa.
2. Kilimo cha kufa na kupona.
3. Chakula ni uhai.
4. Ukulima wa kisasa
5.Kilimo kwanza.

Kwa kweli hizo zote zimefeli. Kwa maoni yangu, ili kilimo kifanikiwe kifanywe huria. Tuvunje hivyo vyama vya ushirika, watu wakitaka ushirika waunde wenyewe kwa hiari zao. Mtu awe huru kuuza mazao yake atakako. Mnunuzi yeyote aruhusiwe kununua. Kodi na tozo kwenye mazao zipunguzwe, ziwe za chini kabisa. Wananchi wanajua jinsi ya kulima. Wakiwa na uhakika wa kurudisha mitaji yao na kupata faida, yatatokea mapinduzi makubwa kabisa ya kilimo katika nchi hii.
 
Huwezi ukaendelea kwa kukitupa mkono kilimo.
Wakoloni walianza na kuinua kilimo.
Soko la China ni kubwa sana hata kila Mtza akilima hatuwezi walishatosha wachina.Tiss wa wenzetu wapo bize kuiba mbinu za kuwini uchumi awapo bize kuiba kura au kudukua wapinzani.
Wapo bize na uchumi ndo KILA kitu.
 
Busara ingetumika bajeti kuhamia Dodoma, tungejenga miundombinu kuliko na umwagiliaji SGR ingepata 90% Toka sector hiyo na viwanda vidogo vilivyo ongezwa thamani.
 
Busara ingetumika bajeti kuhamia Dodoma, tungejenga miundombinu kuliko na umwagiliaji SGR ingepata 90% Toka sector hiyo na viwanda vidogo vilivyo ongezwa thamani.
Pesa kama hiyo tungetumia kujenga miundombinu ya umwagiliaji, tungeweza tengeneza hizo ajira 8m wanazozinadi.
 
Tanzania tumejaliwa na Mungu kuwa na ardhi nzuri tumezungukwa na mito, Bahari na Ziwa...kufeli kwa Kilimo ni kwa sababu Serikali hawajatilia Mkazo mikakati yao yote tokea enzi za kilimo cha Kufa na Kupona mpaka Kilimo kwanza....ni upigaji tu unaendelea hakuna mikakati....
 
.... Kilimo ni Uti wa Mgongo!
... kama kuna sekta imeundiwa taasisi nyingi basi ni sekta ya kilimo!
  1. Naliendele Research Institute
  2. Chuo Kikuu cha Kilimo SUA
  3. Chuo Kikuu cha Kilimo Mwl. Nyerere - Musoma
  4. Bodi ya Mazao Mchanganyiko
  5. Shirika la Usagishaji la Taifa - NMC
  6. Bodi ya Korosho
  7. Bodi ya Pamba
  8. Bodi ya Kahawa
  9. Chuo cha Utafiti Uyole
  10. Mradi wa Jeshi wa Power Tiler
  11. Mamlaka ya Hifadhi ya Chakula
  12. Mamlaka ya Ubora wa Mbolea
  13. Skimu ya Umwagiliaji Rufiji
  14. Skimu ya Umwagiliaji Mto Kilombero
  15. Rufiji Basin Water Board
  16. Lake Victoria Basin Water Board
  17. Kiwanda cha Kukoboa Kahawa Moshi
  18. Kiwanda cha Kukoboa Kahawa Mbinga
  19. Tanzania Farmers Association - TFA
  20. Mradi wa Kilimo cha Mawese Kigoma
  21. Kiwanda cha Mbolea Minjingu
  22. Mradi wa Taifa wa Kupambana na Nzige
  23. Mradi wa Taifa wa Kupambana na Nguruwe Pori
  24. Kamati ya Taifa ya Usuluhishi Wakulima na Wafugaji
  25. Hanang Wheat Plantations
  26. West Kilimanjaro Wheat Plantations
  27. Bodi ya Taifa ya Sukari
  28. National Milling Corporation
  29. Mradi wa Taifa wa Kupambana na Panya Buku
  30. Taasisi ya Taifa ya Kudhibniti Ubora wa Mbegu
  31. Jeshi la Kujenga Taifa JKT
  32. Vyama vya Ushirika - KNCU, MCU, NCU, etc.
  33. Tanzania Pesticide Research Institute - TPRI
  34. NAFCO
  35. ... etc.
  36. ... etc.
  37. ... etc.
Dah! The list is countless! Kote huko waliwekwa makada; output big ZERO!

Aione: Red Giant
 
Bashe nae tulizani anaweza kutusaidia kwenye hii secta kipindi kile kabla ya ya uteuzi wake
alikua mwenye ushawishi mkubwa na uwezo wa kujenga hoja ila nae naona amechemka tu.
 
Bashe nae tulizani anaweza kutusaidia kwenye hii secta kipindi kile kabla ya ya uteuzi wake
alikua mwenye ushawishi mkubwa na uwezo wa kujenga hoja ila nae naona amechemka tu.
Kachemka vibaya mno.
 
.... Kilimo ni Uti wa Mgongo!
... kama kuna sekta imeundiwa taasisi nyingi basi ni sekta ya kilimo!
  1. Naliendele Research Institute
  2. Chuo Kikuu cha Kilimo SUA
  3. Chuo Kikuu cha Kilimo Mwl. Nyerere - Musoma
  4. Bodi ya Mazao Mchanganyiko
  5. Shirika la Usagishaji la Taifa - NMC
  6. Bodi ya Korosho
  7. Bodi ya Pamba
  8. Bodi ya Kahawa
  9. Chuo cha Utafiti Uyole
  10. Mradi wa Jeshi wa Power Tiler
  11. Mamlaka ya Hifadhi ya Chakula
  12. Mamlaka ya Ubora wa Mbolea
  13. Skimu ya Umwagiliaji Rufiji
  14. Skimu ya Umwagiliaji Mto Kilombero
  15. Rufiji Basin Water Board
  16. Lake Victoria Basin Water Board
  17. Kiwanda cha Kukoboa Kahawa Moshi
  18. Kiwanda cha Kukoboa Kahawa Mbinga
  19. Tanzania Farmers Association - TFA
  20. Mradi wa Kilimo cha Mawese Kigoma
  21. Kiwanda cha Mbolea Minjingu
  22. Mradi wa Taifa wa Kupambana na Nzige
  23. Mradi wa Taifa wa Kupambana na Nguruwe Pori
  24. Kamati ya Taifa ya Usuluhishi Wakulima na Wafugaji
  25. Hanang Wheat Plantations
  26. West Kilimanjaro Wheat Plantations
  27. Bodi ya Taifa ya Sukari
  28. National Milling Corporation
  29. Mradi wa Taifa wa Kupambana na Panya Buku
  30. Taasisi ya Taifa ya Kudhibniti Ubora wa Mbegu
  31. Jeshi la Kujenga Taifa JKT
  32. Vyama vya Ushirika - KNCU, MCU, NCU, etc.
  33. Tanzania Pesticide Research Institute - TPRI
  34. NAFCO
  35. ... etc.
  36. ... etc.
  37. ... etc.
Dah! The list is countless! Kote huko waliwekwa makada; output big ZERO!

Aione: Red Giant
Hahaaa, hatari sana haya mambo. Kila kada anaueteuliwa huko anaangalia namna ya kutajirika. Na kwenye kilimo hawajafanya hata nusu ya mambo aliyofanya mkoloni. Tafiti nyingi za wapi kunafaa nini alianzisha mkoloni. Hadi leo tunalima kwa kufuata ramani ya mkoloni.

Na mbaya zaidi, badala ya kufuata mazuri ya mkoloni, wakafuata mambo ya hovyo. Mfano, bodi za mazao zilikuwa ni taasisi za mkoloni ili kupanga bei ya mazao na kupanga tozo ili kumnyonya muafrika. Tukapata uhuru wakaziendeleza, wakaziimarisha na kuanzisha nyingine. Sasa hivi utasikia kuna bodi ya parachichi. Lengo ni kupiga tozo onevu.
 
Back
Top Bottom