Clouds bwana ni kama maji si kwamba naitetea lakini inavyoonekana asilimia kubwa ya wanaoiponda ndo wasikilizaji wakubwa ndo mana wameisikia hata hyo jingle ya rais lakini wakija jf wanatoa mipovu kama wamebwia sabuni ya unga huyo founder wa jamiiforums anaielewa clouds ndo mana alikuwa mmoja wa watoa mada kwenye fursa itakuwa wewe kidampa mwenye fake id acheni kuhate huku mnakubali mioyoni
jana nilijitahidi kuwaza fursa zilizotolewa, tangu nimelisika lile tangazo mpaka nashuka kwenye ile daladala sikuweza kupata jibu, hivi mchomvu , dj fetty na mbwiga ndo walikua wanatoa semina za fursa kwa exposure ipi ya enterpreneur walionayo, kuuza t shirt??, me naona yawezekana ndo weenda kudistort fikra nzuri za vijana mikoani, walishindwa kufanya mashindano ya vikundi vya vijana na kuwapa mitaji katika project zao, walishindwa kutembea na young enterpreneur wa mikoa husika kuwapa mwanga vijana wenzao, sababu fursa inalingana na eneo husika, wao wamewaza kauli mbiu nzuri, then wamefanya kutengeneza max profit kwa kuajiri vijana wao wajivishe elimu wasionayo ya kibiashara, na uandishi juu yake, Tanzania tuna tatizo la waliofanikiwa kuendelea kudidimiza fikra na juhudi za maendeleo kwa wasionayo. Mimi na Tanzania yangu.
radio inayosikilizwa na watu wengi tz ni Radio Free Africa. Kama umezunguka hii Tanzania utakubaliana na mimi, hakuna kona ya hii nchi ambapo radio free haikamati
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.