Qur'an 33:56:
"Hakika Allah na Malaika wake wanamswalia (wanamtukuza, kumheshimu na kumrehemu) Mtume. Enyi mlioamini! Mswalieni naye na mumsalimu kwa salamu ya amani."
Tafsiri ya maelezo hayo:
Allah anapotajwa kuwa "anaswali" juu ya Mtume, haimaanishi kwamba anasali kama binadamu wanavyosali au kuabudu. Kwa Kiarabu, neno "ṣalāh" (صلاة) linapohusishwa na Allah linamaanisha kutoa baraka, heshima, na rehema. Si tendo la kuabudu au kuomba kwa hofu kama wanadamu.
Watafsiri wakubwa wa Kiislamu kama Ibn Kathir, Al-Tabari na hata wasomi wa Kikristo wanaojua Kiarabu wanaelewa kwamba
"Swala ya Allah" kwa Mtume ni heshima na baraka, si ibada au kujinyenyekeza kwa nguvu ya juu zaidi.
Katika Qur’an, Allah hajawahi kusujudu, kuinama au kumuomba mungu mwingine. Yeye ni wa pekee na hajahitaji kitu chochote.
Mjifunze Quran kwa kina acheni kukurupuka bila kua na elimu ya kitu.