Chakaza
Platinum Member
- Mar 10, 2007
- 41,011
- 74,658
(From Zitto FB wallpage.)
Leo nitawapa mfano wa wanasiasa wenzetu wa upinzani katika nchi ya Venezuela, ambapo Rais Mjamaa mwenzetu, ndugu Nico Maduro, kamaradi, amezuia vyama kushiriki uchaguzi. Wakati wa Rais Chavez vyama vya upinzani na wanasiasa wa upinzani walikuwa wanabanwa kweli na Serikali. Hii tunayofanyiwa na Magufuli ya watu kufungwa na kuachiwa, kupigwa, kuzuia mikutano, kukamata watu wanaomkosoa kwenye mitandao ni cha mtoto.
Mwandishi William Dobson aliandika kitabu mwaka 2012 kiitwacho 'Dictator’s Learning curve: Inside the global battle for democracy'. Katika kitabu hiki alimhoji Meya mmoja wa chama cha upinzani katika mji mmoja masikini kabisa kuhusu siasa tofauti. Meya Carlos Ocariz wa Mji wa Petare alimshinda mgombea aliyekuwa anaungwa mkono na Rais Chavez. Rais Chavez akaamua kukata fedha kwenda kwenye mji huo, akaondoa magari ya takataka na kukata maji.
Meya Ocariz anasema, "sikuanza kulalama na kupiga kelele. NIliamua kufanya tofauti na kutekeleza masuala ya maendeleo yaliyo ndani ya uwezo wangu kwenye mji wangu. Kuhakikisha watu wangu wanapata maji nilitumia magari ya Mji kusambaza maji kwenye nyumba za watu. Nilizuia matumizi makubwa ya ofisi na kupeleka fedha kuzoa taka na kuanza kuwalipa wazazi ili wapeleke watoto shuleni".
Meya Ocariz akaendelea; "Upinzani tunalalamika lalamika tangu mwaka 2000, tunapata nini? Badala yake tuwaonyeshe wananchi tofauti ya siasa zetu na za Kamaradi Chavez. Tutatue matatizo ya watu".
Kwa kimombo anasema; "we must offer true political alternatives to Chavez, solving problems and not just complaining about how we are treated in the system that almost everyone agrees is unfair".
Ndugu wajumbe, sisi tuna maeneo tunaongoza, ama Vijiji, Kata au Manispaa. Sisi pia tumekuwa tukisema kuwa tunataka kufanya siasa tofauti. Je inawezekana tumeshindwa kufanya hivi ndio maana baadhi ya wenzetu wanaondoka na kutuhama? Ninatoa rai kuwa tujitafakari kwa kina sababu za ndani za mawimbi haya ya kisiasa na tupate majawabu ya namna ya kusonga mbele.
My take:
Pamoja na ZZK kutoaminika sana katika siasa zake, lakini falsafa aliyoitamka hapo juu nadhani ndio njia sahihi ya kupambana na uongozi Wa kidikteta pale ambapo Halmashauri zetu zinazoongozwa na wapinzani zinapo nyanyaswa kiuchumi
Leo nitawapa mfano wa wanasiasa wenzetu wa upinzani katika nchi ya Venezuela, ambapo Rais Mjamaa mwenzetu, ndugu Nico Maduro, kamaradi, amezuia vyama kushiriki uchaguzi. Wakati wa Rais Chavez vyama vya upinzani na wanasiasa wa upinzani walikuwa wanabanwa kweli na Serikali. Hii tunayofanyiwa na Magufuli ya watu kufungwa na kuachiwa, kupigwa, kuzuia mikutano, kukamata watu wanaomkosoa kwenye mitandao ni cha mtoto.
Mwandishi William Dobson aliandika kitabu mwaka 2012 kiitwacho 'Dictator’s Learning curve: Inside the global battle for democracy'. Katika kitabu hiki alimhoji Meya mmoja wa chama cha upinzani katika mji mmoja masikini kabisa kuhusu siasa tofauti. Meya Carlos Ocariz wa Mji wa Petare alimshinda mgombea aliyekuwa anaungwa mkono na Rais Chavez. Rais Chavez akaamua kukata fedha kwenda kwenye mji huo, akaondoa magari ya takataka na kukata maji.
Meya Ocariz anasema, "sikuanza kulalama na kupiga kelele. NIliamua kufanya tofauti na kutekeleza masuala ya maendeleo yaliyo ndani ya uwezo wangu kwenye mji wangu. Kuhakikisha watu wangu wanapata maji nilitumia magari ya Mji kusambaza maji kwenye nyumba za watu. Nilizuia matumizi makubwa ya ofisi na kupeleka fedha kuzoa taka na kuanza kuwalipa wazazi ili wapeleke watoto shuleni".
Meya Ocariz akaendelea; "Upinzani tunalalamika lalamika tangu mwaka 2000, tunapata nini? Badala yake tuwaonyeshe wananchi tofauti ya siasa zetu na za Kamaradi Chavez. Tutatue matatizo ya watu".
Kwa kimombo anasema; "we must offer true political alternatives to Chavez, solving problems and not just complaining about how we are treated in the system that almost everyone agrees is unfair".
Ndugu wajumbe, sisi tuna maeneo tunaongoza, ama Vijiji, Kata au Manispaa. Sisi pia tumekuwa tukisema kuwa tunataka kufanya siasa tofauti. Je inawezekana tumeshindwa kufanya hivi ndio maana baadhi ya wenzetu wanaondoka na kutuhama? Ninatoa rai kuwa tujitafakari kwa kina sababu za ndani za mawimbi haya ya kisiasa na tupate majawabu ya namna ya kusonga mbele.
My take:
Pamoja na ZZK kutoaminika sana katika siasa zake, lakini falsafa aliyoitamka hapo juu nadhani ndio njia sahihi ya kupambana na uongozi Wa kidikteta pale ambapo Halmashauri zetu zinazoongozwa na wapinzani zinapo nyanyaswa kiuchumi