Kauli Cheshi za KAKOBE

Hivi alipata wapi hivi Vipimo? Hapa lazima tukubali kwamba kama kweli alidanganya na ikathibitika Mbele yake Mwenyewe basi Credibility yake itakuwa imeshuka sana sema tu Waumini hawawezi kumweleza
Kuna post nilianzisha kuhusu Kakobe na powers zake.
Nilisema mimi najua the man has powers na kinachofanyika ni kutaka kufanya powers manifestations kuongeza followers.

Nililaani sana kitendo cha kuwalaza waumini wake pale nje for 70 days huku wakipigwa jua, na kunyeeshewa mvua kwa kuwaaminisha kuwa ni sehemu ya kumtumikia Mungu.

Baada ya hilo zoezi kushindikana, baadhi ya waumini watafunguka macho, they'll come back to their senses na kugundua kumbe walikuwa wakimtumia binadamu!.

Ili asiwapoteze wote, amekuja na ahadi kuwa huo umeme hautawaka!. anataka kujifanya yeye ni kama Shadraki, Meshaki na Abednego kwenye kitabu cha Danieli.

Baada ya Kakobe kusalimu amri, japo nilithibitisha Kakobe anazo nguvu, sasa nathibitisha tena, alikuwa anazo nguvu lakini sasa hana tena hizo nguvu, labda kwa kukiuka masharti, ama mpaka aende tena Nigeria aka renew.

Umeme utawaka, and this is the begining of an end of Kakobeism.
 

hapo ndipo nami niliuliza mwanzoni kuwa ikiwa umeme unaopitishwa ni mkubwa kama ule wa grid (ie check maeneo ya mbezi na kimara) mbona hairuhusiwi kujenga chini au karibu yake, huu wa sam nujoma ni wa kiasi gani na je hauna madhara? wengine tunataka kuelimishwa na si kushutumu kakobe wala tanesco.
 

Mkuu Pasco nataka nisikubaliane nawe katika hili la umaarufu na nguvu za kakobe kuisha ama kupungua.
Wewe, na aidha na watu wengine mnamtazama Kakobe katika muktadha wa kisiasa ambapo kwa bahati yake mbaya amekuwa mtu wa kupoteza. Alipotoa utabiri wa mrema kushinda urais na utabiri wake kushindwa kutimia umaarufu wake haukupungua, tena alizidi kujizolea waumini kedekede.

Hebu muangalie sasa Kakobe kwa muktadha wa kiimani, mtazame kakobe na huduma ya uponyaji anayoitoa kwa watu, halafu ujiridhishe kwamba wale watu waliokuwa na matatizo mbalimbali katika maisha yao kwa miaka nenda rudi lakini wakapata uponyaji wao baada ya kuombewa na Kakobe, kama wanaweza kumsaliti Askofu wao kwa kuwa tu ameshindwa kusimamia uamuzi wa kuzuia nyaya za umeme.Imani ya dini ni tofauti na imani ya siasa ndugu yangu.

Vuta pumzi halafu baada ya miezi kadhaa uende pale kanisani kwake uone watu wanavyotiririka kuingia kanisani ndipo utajua kwamba kakobe amekwisha ama bado wamo.
 
[
“Huu ni uwongo! Wanafikiri hatuna uelewa wa masuala hayo ya umeme? Si kweli kuwa kunaweza kutokea madhara iwapo kutawekwa kona kama wangepitisha upande wa pili; mbona karibu na kaburi la Kiyeyeu kule Iringa nguzo zimevushwa upande wa pili?” alihoji Askofu Kakobe.
Juzi Waziri Ngeleja aliwaambia waandishi wa habari kuwa mgogoro uliodumu kwa siku 77 kati ya serikali na Askofu Kakobe umemaliza kwa askofu huyu kukubali umeme huo kupitishwa eneo la kanisa lake.



SORCE Tanzania Daima.[/QUOTE] kwa hiyo kakobe anataka atuambie kuwa yeye anamamlaka kiasi kwamba umeme kwa wengine upite ila kwake ukwepeshwe? kwa mkuu kiyeyeu umeme hawakukwepesha kwa sababu kama zake, kama na yeye anaweza afanye miujiza ya kiyeyeu
 
Jamaa aliitwa na kuelezwa mambo yake yote ambayo ameyafanya kinyume cha sheria (10) akabaki mdomo wazi. mojawqapo lilikuwa ni sehemu ya kanisa kuwa kwenye road reserve. alitahadharishwa kuwa endapo hengesaini hati ya kuacha madai yake serekali ingetekeleza mara moja hatua ya kubomoa sehemu ambayo ipo kwenye road reserve bila kuchelewa. Jingine ni yeye kuwa na mabilioni ya fedha katika account zake ambazo hazina maelezo. Serikali ilikuwa tayari kufreeze account zake kwani inahisi fedha hizo kawaibia waumini wake
 
Jihadharini na watu ambao wanawajia wakiwa wamevaa ngozi ya kondoo lakini kwa ndani ni mbwa mwitu wakali
 

Mkuu PJ, these are interesting revelations! Hebu tumwagie zaidi yaliyojiri huko.
 
we unamtisha nani?
Mungu wangu ni yule aliyemtaja Daniel, He doesnt take crap.
 
Huwezi kupitisha umeme mkubwa karibu na makazi ya watu kama haya maana ni hatari kwa vyovyote ile
 
Huwezi kupitisha umeme mkubwa karibu na makazi ya watu kama haya maana ni hatari kwa vyovyote ile

Itabidi sasa tuulize wakuu wa Tanesco nini maana ya Umeme MKUBWA maana naona watu wanazungumza habari ya Umeme mkubwa bila kueleza kiasi chake
 

Mkuu Kuhusiana na Post yako hapo juu hebu tembelea hii link

http://www.tanesco.com/Mradi wa Upi...meme- Athari ya Kimazingira na kwa Jamii.pdf
 
Mkuu Kuhusiana na Post yako hapo juu hebu tembelea hii link
Mkuu sasa mbona kumekuwa na migongano kama hii report inajieleza?
Kipengere chenyerangi nyekundu vipi?



Report TANESCO said:
Ili kufanikisha uchambuzi wa tathmini hii, njia mbalimbali zilifuatwa. Njia hizo zinajumuisha hizi
Report TANESCO said:
zifuatazo


Kama TANESCO wangefuata mapendekzo yao wenyewe kama yalivyo kwenye link hiyo basi kusingekuwa na matatizo haya na Askofu Kakobe. Lakini pia watanzania tusimbeze Kakobe, mimi namuheshimu kwani ametuonyesha njia sahihi kusimamia lile tunaloliamini. Kwa mfano kama watanzania tungefanya hivyo kuhakikisha Reli ya kati inapitika na ina huduma nzuri unadhani wasingetekeleza? Kama tungesimamia kuwa warudishe pesa tulizolipa kampuni hewa ya Richmond je zisingerudi? Kama Tungeungana pamoja kukataa ufisadi na udanganyifu wote uliotokea kwenye manunuzi ya vifaa vya jeshi kama Kokobe anavyofanya na waumini wake leo hii tuisngekuwa masikini. Tujifunze kwa Askofu Kakobe, There is alot to learn behind this man Bishop Kakobe and his followers





 


Ahsante sana mdau,.. good observation.

Nadhani kabla hatujamnyooshea vidole Kakobe na kumtuhumu sana hebu tujitahidi kuisoma hiyo ripotiya Tanesco, itatusaidia kuwa na hoja zenye mashiko sio tu kwa suala la kakobe lakini pia na miradi migine ambayo inafanyika tu kiholela pasipo kushirikisha wananchi wa eneo husika.​
 
Naona hoja zimejaa ushabiki, vijembe, kuna wanaotukana nadhani hapa haitatusaidia kwa lolote kwanza nijadili maada hii kama ninavyoona inafaa; at leats we can discuss issue in other directions, siyo swala la Volt, watt, ampere!!

This is the fact!

TANESCO

Tanesco hawataweza kutolaumiwa katika saga loote hili la huu mradi;

1. Tanesco walitakiwa wafanye EIA ambayo ina comprise technical and social risk, katika hiyo EIA walitakiwa wafanye na risk analysis ya mradi kuanzia kuanza mpaka kuisha.However risk assessment unaweza ukaifanya kama separate study

Ninaposema risk assessment inayo-comprise social interest ni kuwashirisha raia wa hayo maeneo kuhusiana na mradi huo, ninachoandika hapa ni standard, na Tanesco wanalijua hilo na ndicho kilichopelekea wawe wapole muda wote huu.

Kilichotakiwakufanyika ni simple wakubwa; iteni watu aelezeni kuna mradi kwa ajili ya manufaa yao na taifa na yao, ndio ulikuwa muda mzuri wa kujadili issue zote hizi zilizotokea sasa. mkikubaliana wawakilishi wanaandika majina yao na kupiga sign ku-endorse mradi.

Mimi kama project manager ninapokuwa ninapanga schedule yangu ya kazi, naangalia time, qality ya kazi na gharama. kwa sababu nimeshafanya risk assessment nina hakika project yangu itaisha kama nilivyopanga kwa bajeti niliyopanga. This is taught everywhere in project management!

Risk assessment inamwokoa professional kukutana na watu kama Kakobe ambaye yuko wrong, haelewi na njia pekee ni kukutana nao mapema. kuna mtu atasema mbona kuna miradi haikufanyika bila EIA, that was old time!

Inakuwa kichekesho kutetea ujinga huu wa Tanesco ambao umetugharimu sisi wooote shilingi millioni 25!!! still mtu anapiga kelele kumtukana Kakobe, where is our thinking, nimemwajiri mtu ameniletea hasara ya milioni 25 ambayo angeikwepa kama angefuata utaratibu unaotakiwa unamlaumu mtu wa mbali kabisa??

ushiriki wa raia

Ushiriki wa raia ni lazima kwa standard za sasa za WB, IMF na first world, imegundulika kuna miradi mingine haiisaidii jamii bali wahusika fulani, haya yametokea sana UK , kwenye nuclear waste, migodi, food waste, toxic waste n.k, Tanzania tuna mradi wa mabati ya asbestos ambao ulifungwa kwa sababu raia wa hayo maeneo walipata na wanaendelea kupata cancer hata leo hii. Project in now a days lazima ufanye risk analysis ' tuache fikra za kizamani za zidumu fikra sahihi za serikali'' wangefanya the same approach kwa Asbestos watu wasingepata makansa. Leo hii tuna minara ya simu imezagaa kila kona nani alifanya EIA? nchi za asia hivi sasa hawataki kuona mnara karibu na shule za watoto n.k . why??

Kauna ushahidi approach hii ya serikali/Tanesco kutoshirkisha raia ndio iliyofanya watu wafukiwe migodini na miradi ya migodi kuanzishwa pasipo ushiriki wa raia. Hii imetokea sehemu nyingi duniani

KAKOBE

Nilipopata taarifa kwa mara ya kwanza nilikusifia sana kwa sababu umeonyesha njia ya wataalamu, kufanya kazi zao kitaalamu kadiri procedures na standard zinavyosema. Nilifurahi sana siyo kukutetea wewe bali at least watendaji wa serikali watajua nini kinatakiwa kifanyikekwenye project zingine.

I think by your capacity and status serikali ilikaa chini na kukusikiliza, hilo pekee lina -i-credit serikali kuwa inasikiliza watu kama wewe. Serikali wakati inaongea na wewe ilijishusha na kukusikiliza, hata kupelekea kufanya vikao mpaka jumamosi.

Mkutano wako wa Jumamosi ulipokataa tena maoni ya wataalamu wa BICO, wakiongozwa na Kyaruzi professor wa umeme nilikushangaa sana. Nilidhani kwako wewe ungekuwa wakati mzuri wa kuandikishiana mkataba na Taneco kuwa if anything happen Tanesco watakuwa liable. Siyo kubisha tu kama mtu ambaye hana sense sawa sawa au hawezi kufikia kuelewana.

Hatua hii ya ubishi siyo tu kuwa ime-kudevalue lakini pia imenipa picha na kunikumbusha mengi sana kuhusu wewe na kanisa kwa ujumla. Ubishi, ujuaji, kutokuamini siyo tabia za upendo kama ambayo wakorintho wa 1 sura ya 13 inavyosema. It was good time and only chance to show and rise up again and show the public you did that for good reasons. However now it will be difficult to suggest that, askofu kama wewe aispofikia hatu ya kusema nimekubali, je waumini wako?/ wanaiga nini??

Ubishi wako kutokana na kutokujua haukuwa na matatizo kamwe, ila ubishi wako baada ya kujua ndiyo umeleta maswali mengi na jina la Yesu kuchafuliwa.
 
All in All, nimeipenda sana approach ya Serikali katika hili Jambo! Serikali imetumia Delay technique, Wametoa Muda wa kutosha ili kila Mtu a digest na Kupembua Pumba na Mchele, Nadhani baada ya muda kupita hata wale waliokuwa wanalinda walijiuliza maswali na wakapata majibu Sahihi, na watakuwa wanamshuru sana Ngeleja kwa kuwafanya Wachomoke katika ile Loop
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…