GreatConqueror
Member
- Mar 27, 2009
- 75
- 5
Jumatano iliyopita tarehe 3 June nilinunua kama kawaida yangu gazeti la Mwanahalisi nilichokutana nacho kwenye page ya Katuni sikuamini macho yangu manake nilihisi labda ze utamu wameanzisha gazeti na nimelinunua bila kujitambua. Kwa kweli katuni ile mimi binafsi sikuilewa mantiki ya kuwekwa kwenye gazeti linaloheshimika kama hilo.
Hivi mchora katuni huyu na mhariri wake hawakuwa na njia mbadala ya kuonyeshwa kukerwa na safari za nje za Rais zaidi ya kumdhalilisha kiasi hiki? Hebu fikiria unasoma gazeti then mtoto anakuuliza hii katuni ina maana gani na huyo aliyechorwa kabeba nini? (nguo za aibu kweli kweli!!).
Jumanne June 2 katika gazeti la Sauti Huru ilitoka makala yenye kichwa "TUMSILIKILIZE MWAKYEMBE KISHA TUMPUUZE". Ndani ya hiyo makala kulikuwa na paragraph inayodai
Hivi mchora katuni huyu na mhariri wake hawakuwa na njia mbadala ya kuonyeshwa kukerwa na safari za nje za Rais zaidi ya kumdhalilisha kiasi hiki? Hebu fikiria unasoma gazeti then mtoto anakuuliza hii katuni ina maana gani na huyo aliyechorwa kabeba nini? (nguo za aibu kweli kweli!!).
Jumanne June 2 katika gazeti la Sauti Huru ilitoka makala yenye kichwa "TUMSILIKILIZE MWAKYEMBE KISHA TUMPUUZE". Ndani ya hiyo makala kulikuwa na paragraph inayodai
"Kwa nini Mwakyembe anataka kutufanya watu wote WAPUMBAVU?
Yaani kulala Ifunda ndio iwe sababu ya kutokulala kwenye gari?
Hii ni aina fulani ya UTAAHIRA".
Yaani kulala Ifunda ndio iwe sababu ya kutokulala kwenye gari?
Hii ni aina fulani ya UTAAHIRA".
Huyu mwandishi naye na mhariri wake hawakuwa na njia mbadala ya kuonyesha "HASIRA" zao kwa tamko la Mwakyembe kuhusu ajali yake? Tunajua kuna baadhi ya magazeti yameanzishwa ili kupambana na watu fulani, lakini tunaomba ziwe zinatumika lugha za staha kwani magazeti husomwa na watu wa rika zote!
Wanahabari mnatupeleka wapi?
Naomba kutoa hoja
Wanahabari mnatupeleka wapi?
Naomba kutoa hoja