Katuni ya Mwanahalisi na Hatima ya Magazeti Yetu

Katuni ya Mwanahalisi na Hatima ya Magazeti Yetu

Joined
Mar 27, 2009
Posts
75
Reaction score
5
Jumatano iliyopita tarehe 3 June nilinunua kama kawaida yangu gazeti la Mwanahalisi nilichokutana nacho kwenye page ya Katuni sikuamini macho yangu manake nilihisi labda ze utamu wameanzisha gazeti na nimelinunua bila kujitambua. Kwa kweli katuni ile mimi binafsi sikuilewa mantiki ya kuwekwa kwenye gazeti linaloheshimika kama hilo.

Hivi mchora katuni huyu na mhariri wake hawakuwa na njia mbadala ya kuonyeshwa kukerwa na safari za nje za Rais zaidi ya kumdhalilisha kiasi hiki? Hebu fikiria unasoma gazeti then mtoto anakuuliza hii katuni ina maana gani na huyo aliyechorwa kabeba nini? (nguo za aibu kweli kweli!!).

Jumanne June 2 katika gazeti la Sauti Huru ilitoka makala yenye kichwa "TUMSILIKILIZE MWAKYEMBE KISHA TUMPUUZE". Ndani ya hiyo makala kulikuwa na paragraph inayodai

"Kwa nini Mwakyembe anataka kutufanya watu wote WAPUMBAVU?
Yaani kulala Ifunda ndio iwe sababu ya kutokulala kwenye gari?
Hii ni aina fulani ya UTAAHIRA".

Huyu mwandishi naye na mhariri wake hawakuwa na njia mbadala ya kuonyesha "HASIRA" zao kwa tamko la Mwakyembe kuhusu ajali yake? Tunajua kuna baadhi ya magazeti yameanzishwa ili kupambana na watu fulani, lakini tunaomba ziwe zinatumika lugha za staha kwani magazeti husomwa na watu wa rika zote!

Wanahabari mnatupeleka wapi?

Naomba kutoa hoja



moz-screenshot-12.jpg
moz-screenshot-13.jpg
 

Attachments

  • KATUNI.JPG
    KATUNI.JPG
    86 KB · Views: 124
Mkuu kuhusu hiyo katuni mimi sijaona ubaya wake... labda tufafanulie zaidi. Ni hizo nguo za ndania au??
 
kwa upande wangu naona jamaa alikuwa sawa kabisa,maana amefananisha safari ya vasco da ***** kuwa ni safari ambayo haina manufaa kwa taifa,duh! weli prezida wetu watu wamemchoka,kumbe alikwenda kumnunulia wife kufuli na S***a mweh!
mkuu asante sana kwa picha hii maana umenivunja mbavu.
 
Lazima tuelewe kuwa kadiri tunavyoendelea, na kukuza demokrasia, uhuru wa kujieleza nao pia unakua.Uhuru wa kujieleza unaendana na ustaarabu.Mwingine anaweza kufikiri ustaarabu ni kutomchora rais vibaya, kwa kuendeleza kile Jaji Warioba alichokiita "rais ni alama ya taifa".Lakini wengine tutapinga vikali na kusema watu wana uhuru wa kujieleza, ikiwa ni pamoja na kutoa maoni yaliyo tofauti na ya wengine -pamoja na kumkaragosi rais- ilimradi tu hawavunji sheria.

Rais ni mtu na anaishi katika jamii yetu, hivyo anaweza kukosea.Anapokosea, waandishi wa habari pamoja na wachora katuni wana wajibu wa kuifikishia jamii ujumbe kuhusu maoni yao.Kilichofanyika hapa ni kuwakilisha maoni ya baadhi ya watanzania kuhusu safari za Kikwete.Inawezekana maoni haya yako sawa au hayako sawa, haisumbui kama yako sawa au hayako sawa ilmuradi hayajavunja sheria, kinachosumbua ni kuona kuna watu hawataki maoni yaliyo tofauti na yao yachapishwe.

Kwangu mimi, ukiachilia mbali maudhui ya kikatuni -kwamba kiko sawa au si sawa- kikatuni hiki kamwe hakimvunjii heshima rais, bali kinamuongezea heshima na kumfanya aonekane bingwa wa demokrasia ambaye anaweza kufungia gazeti kwa sababu nyingi tu lakini hajachagua kufanya hivyo kwa kuelewa umuhimu wa demokrasia na uhuru wa kujieleza.
 
Jumatano iliyopita tarehe 3 June nilinunua kama kawaida yangu gazeti la Mwanahalisi nilichokutana nacho kwenye page ya Katuni sikuamini macho yangu manake nilihisi labda ze utamu wameanzisha gazeti na nimelinunua bila kujitambua. Kwa kweli katuni ile mimi binafsi sikuilewa mantiki ya kuwekwa kwenye gazeti linaloheshimika kama hilo.

Hivi mchora katuni huyu na mhariri wake hawakuwa na njia mbadala ya kuonyeshwa kukerwa na safari za nje za Rais zaidi ya kumdhalilisha kiasi hiki? Hebu fikiria unasoma gazeti then mtoto anakuuliza hii katuni ina maana gani na huyo aliyechorwa kabeba nini? (nguo za aibu kweli kweli!!).

Jumanne June 2 katika gazeti la Sauti Huru ilitoka makala yenye kichwa "TUMSILIKILIZE MWAKYEMBE KISHA TUMPUUZE". Ndani ya hiyo makala kulikuwa na paragraph inayodai

"Kwa nini Mwakyembe anataka kutufanya watu wote WAPUMBAVU?
Yaani kulala Ifunda ndio iwe sababu ya kutokulala kwenye gari?
Hii ni aina fulani ya UTAAHIRA".


Huyu mwandishi naye na mhariri wake hawakuwa na njia mbadala ya kuonyesha "HASIRA" zao kwa tamko la Mwakyembe kuhusu ajali yake? Tunajua kuna baadhi ya magazeti yameanzishwa ili kupambana na watu fulani, lakini tunaomba ziwe zinatumika lugha za staha kwani magazeti husomwa na watu wa rika zote!​



Wanahabari mnatupeleka wapi?​



Naomba kutoa hoja​






moz-screenshot-12.jpg
moz-screenshot-13.jpg

Mimi binafsi sikuona ubaya wowote kwenye ile cartoon ya Mwanahalisi; kwa uelewa wangu cartoon ile ilikuwa na ujumbe kuwa safari za muungwana hazina tija kwa wadanganyika ila pengine kwa familia yake!! Sikuona kitu chochote cha kulidhalisha gazeti la Mwanahalisi. Ulikuwa ujumbe sawia!
 
Back
Top Bottom