Katibu wa Nyerere atishwa

Katibu wa Nyerere atishwa

Ewe punguani pitia nyuzi wacha kiherehere, hilo swali nimeshalijibu.

Joan Wicken ndiye katibu wa Nyerere huyo mwingine mnaemoachika labda alikuwa ni tarishi tu wa Ikulu hakuna zaidi.

punguan wahed!!! don't discuss people instead of issues...turejee kwenye mada: je hayo aliyoyasema huyo katibu wa nyerere unayemkataa (kwa sababu za udini uliokujaa damuni) kasema ukweli au uongo? hiyo ndiyo hoja ya msingi ya kujadili hapa, sio blaablaa zako.

lowasa ni fisadi mkubwa, hafai kuwa kiongozi wa nchi hii...kama ameinajisi nchi akiwa nje ya ikulu, je akiingia magogoni itakuwaje? acha kushabikia ujinga wee ajuza!
 
punguan wahed!!! don't discuss people instead of issues...turejee kwenye mada: je hayo aliyoyasema huyo katibu wa nyerere unayemkataa (kwa sababu za udini uliokujaa damuni) kasema ukweli au uongo? hiyo ndiyo hoja ya msingi ya kujadili hapa, sio blaablaa zako.

lowasa ni fisadi mkubwa, hafai kuwa kiongozi wa nchi hii...kama ameinajisi nchi akiwa nje ya ikulu, je akiingia magogoni itakuwaje? acha kushabikia ujinga wee ajuza!

Huo udini sasa unauleta wewe. Joan Wicken dini gani? Nyerere dini gani? Huyo tarishi mnaempachika u katibu dini gani?

Think before you bark.

Punguani double wahed.
 
Sio kwamba hujui unachokisema ila unajitoa akili kwa sababu zako za UDINI uliokujaa hadi kwenye hilo juba lako...mdini mkubwa wewe! Unafahamu maana ya KATIBU MYEKA weye ajuza au unapendaga kujitoa akili bila sababu? Tofautisha kati ya PA na Katibu Myeka....na usitake kutubadilishia mada.

baada ya maCCM kuona mmebanwa kotekote, mmeanza kuwatisha watu na kuwateaua wakuu wa wilaya kwa ajili ya kupitisha katiba ya CCM na kuiba kura. hamuambulii kitu mwaka huu, wapuuzi wakubwa!

Kuna ukweli ndani ya hoja ya FF ingawa ni kweli mzee Kasori alikuwa mmoja wa wasaidizi wa Mwalimu Nyerere. Hata hivyo ninayo shaka kwamba aidha kwa kujua ama kutofahamu,amekuwa anatumiwa vibaya na kambi za uRais ndani ya CCM!

Imekuwa kawaida siku hizi huyu mzee kuitwa kuhutubia mikutano ya taasisi,mashirika ya umma na idara za serikali. Lakini wote tunavyo fahamu watawala wa sasa wanafanya mambo kinyume kabisa na Mwl. Nyerere! Sasa msaidizi wa mtu ambaye wahusika wametupa sera zake zote inakuwaje amegeuzwa lulu?!
 
Mimi siko kambi ya Lowasa wala ya mtu yeyote. Lakini napata wasiwasi na maelezo haya, maana mtu mwenyewe kakili kuwa ni mwongo kamwongopea Nyerere itakuwa sisi.
Nadhani uzi huu una propaganda fulani.

mkuu,kusema uongo ni dhambi ni ni mbaya,lakini zaidi ni kusema uongo ukiwa mtu mzima,na mbaya zaidi sana ni kuweza kusema uongo kwa Mzee Nyerere,mtu mwongo wa namna hiyo leo unaweza kumuamini kweli pasi shaka?
 
KATIBU Myeka mstaafu wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, Samuel Kasori, ameyakimbia makazi yake yaliyopo mjini Arusha na kwenda kujificha kusikojulikana kwa hofu ya kuuawa na wale anaowaita "magaidi wa kisiasa".

Kasori ndiye aliyekuwa Katibu Myeka wa mwisho wa Nyerere kabla hajafariki dunia Oktoba 14 mwaka 1999, amedai kwamba wanaomtishia maisha wanamwona yeye kama kikwazo kwa kundi katika mbio za kuwania Urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

Mstaafu huyo tayari ametoa taarifa katika ngazi za juu za nchi na katika vyombo vya dola na Raia Mwema linafahamu kwamba tayari Dola inafanyia kazi taarifa zake hizo.

Katika mojawapo ya ujumbe mfupi wa maneno kupitia simu ya mkononi (SMS), Kasori aliandika kwa mmoja wa viongozi wa juu wa serikali na vyombo vya dola maneno haya;

"Utakumbuka kwamba tarehe 12 Februari 2015, nilikutaarifu kuwa maisha yangu yanatishiwa na Mheshimiwa [amemtaja jina] kupitia kwa ADC [Aide de Camp – Mlinzi] wake [anamtaja jina] ambaye ni mtumishi wa Serikali [Usalama wa Taifa] niliyekuwa naye kwa hayati Mwalimu J. K. Nyerere…..";na akaendelea kuelezea kwa kina kile anachokiita "hali hatarishi" akisema:

"Tarehe 05/03/2015, siku ya Alhamisi, saa 11.00 jioni, wamekuja nyumbani kwangu, watu wawili wanaume, kijana na mzee wakiwa na usafiri wa Toyota, wakagonga geti langu wakitaka wafunguliwe; wakamuuliza mmoja wa wanafamilia yangu: "Mr. Kasori yupo?"; na kutaka waruhusiwe kuangalia "garden" [bustani] yangu; wakaambiwa nimetoka".

"Wakaulizwa walikotoka wakajibu wametoka Moshi na kwamba jamaa yao mmoja amewapa habari za bustani yangu na wakaendelea kuomba wakaribishwe lakini hawakuruhusiwa na badala yake wakapewa simu niongee nao, kisha wakaombwa waje [wakati] nikiwapo; wakasema tarehe 9/3/2015".

Mzee Kasori aliendelea kueleza; "tarehe 7/3/2015, Jumamosi, walikuja tena watu wawili [wengine] vijana wakiwa na nguo zilizofunika sura zao kutoka utosini hadi miguuni, huku machoni wamevaa miwani ya giza na mikononi wamevaa "gloves" [glavu] nyeusi wakiwa na usafiri wa gari aina ya Toyota yenye namba zisizosomeka vizuri.

"Mtu wa familia yangu alipofungua geti na kuona kuona hali hiyo, aliogopa na kujifunika kanga kichwani; nao wakauliza kutaka kujua alikokuwa [yeye Kasori] na waonyeshwe bustani yake.

"Watu hao walijitambulisha kwamba walitoka Dodoma; wakauliza kama nyumba hiyo ilikuwa na mlinzi; na walipojibiwa kwamba inaye, wakasema watamsubiri [Kasori] hapo hapo langoni.

Katibu Myeka huyo wa Rais wa zamani ameeeleza katika ujumbe wake huo kuwa walipotakiwa wampigie [Kasori] simu, watu hao walikataa katakata, kisha wakampiga picha mwanafamilia huyo pamoja na geti hilo kabla ya kuondoka kwa kasi bila kuaga.

Akifafanua zaidi, Mzee Kasori anawataja, mbali na mlinzi wa kigogo anayemtuhumu kufadhili hujuma hii, watu wengine wawili na namba zao za simu, waliokodiwa kufanikisha mauaji; mmoja akiwa mkazi wa Dar es Salaam na mwingine yuko Arusha; na kumaliza kwa kusema:

"Mheshimiwa Rais, niseme tu kuwa, nitakapouawa mwaka 2015, basi kama ilivyo kwa hayati J. K. Nyerere, msitafute kumbukumbu zetu katika makaburi bali katika mioyo ya tulioboresha maisha yao; buriani Tanzania".

Februari mwaka huu, gazeti hili lilifanya mahojiano na Mzee Kasori juu ya kauli kwamba mmoja wa watu wanaotajwa kutaka kuwania Urais kupitia CCM, Edward Lowassa, aliwahi kupata baraka za Mwalimu Nyerere kuingia kwenye kinyang'anyiro kama hicho mwaka 1995.

Kwenye mahojiano hayo, Kasori alikanusha kwa nguvu zote jambo hilo kuwahi kutokea na kwamba ilikuwa ni kinyume chake; na kwamba Mwalimu alimwita kigogo huyo kuwa mtu "asiye na chembe ya sifa kuweza kugombea nafasi hiyo ya juu nchini".

Kasori alisema alielekezwa na Mwalimu ayafikishe maneno hayo kwa hayati Rashid Kawawa ili naye ayafikishe kwa "kigogo" huyo kwa vile Mwalimu hakuwa na muda wa kupoteza kwa ghilba kama hizo.

Katika kinyang'anyiro hicho cha Urais, Mwalimu alimpigia debe Benjamin Mkapa, akimpachika jina la sifa "Mr. Clean" [Mtu msafi] hadi akaweza kushinda na kupokea kijiti cha uongozi kutoka kwa Rais wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi.

Tangu kuchapishwa kwa mahojiano hayo na gazeti hili, Mzee Kasori amelalamika kupitia vyombo vya habari kuhusu kuandamwa na watu wasiojulikana kiasi cha kuhofia uhai wake.

Gazeti hili limefanikiwa kuzungumza na Kasori akiwa mafichoni kwa njia ya simu na akionekana kutojiandaa wala kuwa tayari kusema mengi, bali kwa kifupi tu, alisema:

"Kweli itashinda tunavyoishi. Kweli haihofu tisho wala nguvu ya majeshi. La uongo lina mwisho, kweli kitu cha aushi/Kweli itashinda kesho kama leo haitoshi, " alisema akinukuu mojawapo ya mashairi ya mshairi namba moja hapa nchini, hayati Shaaban Robert.

Mmoja wa marafiki wa karibu wa Kasori ambaye alihojiwa na gazeti hili wiki hii kutokana na habari hizi alisema; "Je, ni kweli maelezo aliyotoa kwenye mahojiano na gazeti lenu (Raia Mwema) ni ya kuchukiza na hatarishi kufanya mwanasiasa makini, anayejua ‘malumbano' ya kisiasa, kumfanya aape kutoa uhai wa mtu?

"Je, ni kweli muuaji mzoefu, tena kwa ushirikiano na maofisa wazoefu wa dola inavyodaiwa; anaweza kujibwaga nyumbani kwa mtu kufanya tendo hilo mchana kweupe na mbele ya macho makavu ya umma, kama anavyotaka Mzee Kasori tuamini?" alisema.

Samuel Kasori alikuwa Katibu Myeka wa tatu na wa mwisho wa Rais kwa uongozi wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere; wa kwanza akiwa ni Mama Joan Wickens, tangu uhuru; akafuatiwa na Joseph Butiku, ambaye kwa sasa ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere nchini.


Chanzo:
Raia Mwema
 
Katibu wa Nyerere atishwa, akimbia nyumba
Mwandishi Wetu
Toleo la 397
18 Mar 2015

KATIBU Myeka mstaafu wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, Samuel Kasori, ameyakimbia makazi yake yaliyopo mjini Arusha na kwenda kujificha kusikojulikana kwa hofu ya kuuawa na wale anaowaita “magaidi wa kisiasa”. Kasori ndiye aliyekuwa Katibu Myeka wa mwisho wa Nyerere kabla hajafariki dunia Oktoba 14 mwaka 1999, amedai kwamba wanaomtishia maisha wanamwona yeye kama kikwazo kwa kundi katika mbio za kuwania Urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu. Mstaafu huyo tayari ametoa taarifa katika ngazi za juu za nchi na katika vyombo vya dola na Raia Mwema linafahamu kwamba tayari Dola inafanyia kazi taarifa zake hizo. Katika mojawapo ya ujumbe mfupi wa maneno kupitia simu ya mkononi (SMS), Kasori aliandika kwa mmoja wa viongozi wa juu wa serikali na vyombo vya dola maneno haya; “Utakumbuka kwamba tarehe 12 Februari 2015, nilikutaarifu kuwa maisha yangu yanatishiwa na Mheshimiwa [amemtaja jina] kupitia kwa ADC [Aide de Camp – Mlinzi] wake [anamtaja jina] ambaye ni mtumishi wa Serikali [Usalama wa Taifa] niliyekuwa naye kwa hayati Mwalimu J. K. Nyerere…..”;na akaendelea kuelezea kwa kina kile anachokiita “hali hatarishi” akisema: “Tarehe 05/03/2015, siku ya Alhamisi, saa 11.00 jioni, wamekuja nyumbani kwangu, watu wawili wanaume, kijana na mzee wakiwa na usafiri wa Toyota, wakagonga geti langu wakitaka wafunguliwe; wakamuuliza mmoja wa wanafamilia yangu: “Mr. Kasori yupo?”; na kutaka waruhusiwe kuangalia “garden” [bustani] yangu; wakaambiwa nimetoka”. “Wakaulizwa walikotoka wakajibu wametoka Moshi na kwamba jamaa yao mmoja amewapa habari za bustani yangu na wakaendelea kuomba wakaribishwe lakini hawakuruhusiwa na badala yake wakapewa simu niongee nao, kisha wakaombwa waje [wakati] nikiwapo; wakasema tarehe 9/3/2015”.

Mzee Kasori aliendelea kueleza; “tarehe 7/3/2015, Jumamosi, walikuja tena watu wawili [wengine] vijana wakiwa na nguo zilizofunika sura zao kutoka utosini hadi miguuni, huku machoni wamevaa miwani ya giza na mikononi wamevaa “gloves” [glavu] nyeusi wakiwa na usafiri wa gari aina ya Toyota yenye namba zisizosomeka vizuri. “Mtu wa familia yangu alipofungua geti na kuona kuona hali hiyo, aliogopa na kujifunika kanga kichwani; nao wakauliza kutaka kujua alikokuwa [yeye Kasori] na waonyeshwe bustani yake. “Watu hao walijitambulisha kwamba walitoka Dodoma; wakauliza kama nyumba hiyo ilikuwa na mlinzi; na walipojibiwa kwamba inaye, wakasema watamsubiri [Kasori] hapo hapo langoni.

Katibu Myeka huyo wa Rais wa zamani ameeeleza katika ujumbe wake huo kuwa walipotakiwa wampigie [Kasori] simu, watu hao walikataa katakata, kisha wakampiga picha mwanafamilia huyo pamoja na geti hilo kabla ya kuondoka kwa kasi bila kuaga. Akifafanua zaidi, Mzee Kasori anawataja, mbali na mlinzi wa kigogo anayemtuhumu kufadhili hujuma hii, watu wengine wawili na namba zao za simu, waliokodiwa kufanikisha mauaji; mmoja akiwa mkazi wa Dar es Salaam na mwingine yuko Arusha; na kumaliza kwa kusema: “Mheshimiwa Rais, niseme tu kuwa, nitakapouawa mwaka 2015, basi kama ilivyo kwa hayati J. K. Nyerere, msitafute kumbukumbu zetu katika makaburi bali katika mioyo ya tulioboresha maisha yao; buriani Tanzania”.

Februari mwaka huu, gazeti hili lilifanya mahojiano na Mzee Kasori juu ya kauli kwamba mmoja wa watu wanaotajwa kutaka kuwania Urais kupitia CCM, Edward Lowassa, aliwahi kupata baraka za Mwalimu Nyerere kuingia kwenye kinyang’anyiro kama hicho mwaka 1995. Kwenye mahojiano hayo, Kasori alikanusha kwa nguvu zote jambo hilo kuwahi kutokea na kwamba ilikuwa ni kinyume chake; na kwamba Mwalimu alimwita kigogo huyo kuwa mtu “asiye na chembe ya sifa kuweza kugombea nafasi hiyo ya juu nchini”. Kasori alisema alielekezwa na Mwalimu ayafikishe maneno hayo kwa hayati Rashid Kawawa ili naye ayafikishe kwa “kigogo” huyo kwa vile Mwalimu hakuwa na muda wa kupoteza kwa ghilba kama hizo. Katika kinyang’anyiro hicho cha Urais, Mwalimu alimpigia debe Benjamin Mkapa, akimpachika jina la sifa “Mr. Clean” [Mtu msafi] hadi akaweza kushinda na kupokea kijiti cha uongozi kutoka kwa Rais wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi.

Tangu kuchapishwa kwa mahojiano hayo na gazeti hili, Mzee Kasori amelalamika kupitia vyombo vya habari kuhusu kuandamwa na watu wasiojulikana kiasi cha kuhofia uhai wake. Gazeti hili limefanikiwa kuzungumza na Kasori akiwa mafichoni kwa njia ya simu na akionekana kutojiandaa wala kuwa tayari kusema mengi, bali kwa kifupi tu, alisema: “Kweli itashinda tunavyoishi. Kweli haihofu tisho wala nguvu ya majeshi. La uongo lina mwisho, kweli kitu cha aushi/Kweli itashinda kesho kama leo haitoshi, ” alisema akinukuu mojawapo ya mashairi ya mshairi namba moja hapa nchini, hayati Shaaban Robert.

Mmoja wa marafiki wa karibu wa Kasori ambaye alihojiwa na gazeti hili wiki hii kutokana na habari hizi alisema; “Je, ni kweli maelezo aliyotoa kwenye mahojiano na gazeti lenu (Raia Mwema) ni ya kuchukiza na hatarishi kufanya mwanasiasa makini, anayejua ‘malumbano’ ya kisiasa, kumfanya aape kutoa uhai wa mtu? “Je, ni kweli muuaji mzoefu, tena kwa ushirikiano na maofisa wazoefu wa dola inavyodaiwa; anaweza kujibwaga nyumbani kwa mtu kufanya tendo hilo mchana kweupe na mbele ya macho makavu ya umma, kama anavyotaka Mzee Kasori tuamini?” alisema.

Samuel Kasori alikuwa Katibu Myeka wa tatu na wa mwisho wa Rais kwa uongozi wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere; wa kwanza akiwa ni Mama Joan Wickens, tangu uhuru; akafuatiwa na Joseph Butiku, ambaye kwa sasa ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere nchini. - See more at: Raia Mwema - Katibu wa Nyerere atishwa, akimbia nyumba
 
Mbio za urais Tanzania huwa ni kama mapambano ya vita...

Ndio wakati ambapo ajali huongezeka, wapiga manyanga hutafutwa kwa udi na uvumba, fitna na vijembe hushamiri...

Mwisho wa siku anayepewa nchi huishia kurudi nyuma kulipa fadhila...
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Lowasa haitaji msaada wa Mwalimu. Mwalimu alituwekea Nkapa, tumeona alivyobadilika na kuwa fisadi nyangumi
 
Huyo mzee anajitekenya na kucheka yeye mwenyewe, ametumwa na kambi yake kufanya maigizo ili kudhoofisha kambi ya fisadi Lowassa. Huenda muda huu Kasori kajifungia kwa kimada anakula papauchi na bia kwa hela toka WAMA
 
hekaya za abunuas

hivi wanahabari wetu wameishiwa namna hii hadi wanaokoteza hekaya na kuzita habari kma sio kutumika ni nini?
 
Huyo mzee anajitekenya na kucheka yeye mwenyewe, ametumwa na kambi yake kufanya maigizo ili kudhoofisha kambi ya fisadi Lowassa. Huenda muda huu Kasori kajifungia kwa kimada anakula papauchi na bia kwa hela toka WAMA
Mzee psycho huyo
 
Inatisha aisee! Watu wamefikia mpaka kutaka kutoa roho za wanadamu wenzao ili mradi tu waingie Ikulu pamoja na kuwa hawana hata sifa moja ya kuweza kuiongoza nchi.

Mbio za urais Tanzania huwa ni kama mapambano ya vita...

Ndio wakati ambapo ajali huongezeka, wapiga manyanga hutafutwa kwa udi na uvumba, fitna na vijembe hushamiri...

Mwisho wa siku anayepewa nchi huishia kurudi nyuma kulipa fadhila...
 
Mh! Kwa ushawishi gani aliokuwa nao mzee Kasori Watu Watake kumuua? Tatizo na yeye kukubali kutumika na maadui wa Lowassa
 
Mimi wala sioni kama hili ni jambo geni kwa Tanzania. Lowasa yuko tayari afanye lolote lile ili aingie ikulu kwa ajili ya pride yake na kuwakomesha kama kuwazomea adui zake. Na kwa ccm kuua watu si jambo la ajabu. Jiulizeni habari za ulimboka, mwakyembe, magufuli, Dr Mvungi, Dr. Balali, Dr. Nani aliyekuja na habari za Balali toka US, Dr.Kibona, Dr. Mgimwa, n.k n.k.

Kama haya yote na mengine mengi yamewahi kutokea, kwa mtu anayemfahamu vizuri Lowasa na unafiki wake wa kinyoka, hawezi kuona ni jambo la ajabu kutoa roho ya kila anayesimama mbele yake. Mzee Kisori amekuwa muwazi sana akililia Tanzania ya Mwalimu. Amewatahadharisha Watanzania ni hatari gani iliyopo kujaribu kumruhusu fisadi lowasa agombee nafasi ya uraisi. Kosa lake liko wapi? Kichaa chake mnaomwita psycho, kiko wapi? Is Lowasa a clean person hata awe na ndoto za kugombea uraisi kama si dharau kwa watanzania? Haya ya lowasa kulazimisha uraisi ni manufaa ya kushuka kwa elimu ya nchi? Kukata tamaa ya maisha kwa watz na kuamua liwalo na liwe? Au ni umaskini wa kila kitu wanadhani hili fisadi litakuwa linapitisha migao ya maziwa ya chai kila kaya asubuhi?

Tatizo kubwa ni la Watanzania. Anayehoji kwamba hili ni jambo lenye uzito kwa mwanasiasa makini kupanga mauaji, mwanasiasa makini ni nani? Lowasa si mwanasiasa makini zaidi ya fisadi jeuri. Lolote anaweza kufanya.

Mtu anayehoji muuaji kwenda kumfuata mtu nyumbani, anatakiwa aajiulize kwanza hawa waliouliwa hapo juu waliuawa wakiwa wapi? Hakuna waliouliwa nyumbani kwao? Watu wangapi wameuliwa ndani ya nyumba zao? Watu wamuawa hadharani kina mwangosi, na hakuna hatua yoyote imechukuliwa, leo mtu mwenye akilil unashangaa mtu amejifunika kumfuata mzee nyumbani kwake? Au wanataka afe halafe waeneza uvumi ameuawa kwa visasi vya mashamba na bustani yake nzuri?

Watanzania acheni kudharau mwiba kabla hamjakata miguu kwa cancer. Lowasa hata kama atamuua Mzeee Kisori, historia zake zinam disqualify hata kuwa mjumbe wa baraza la kata. Linachotumia ni rushwa kwa sababu ya umaskini wa Watanzania na ujinga wao vichwani.

Ninaomba serikali ipitishe muswada wa kumiliki silaha ili tujilinde. LOWASA NA MAJITU YA AINA YAKE HAWATAKAA WATAWALE NCHI HII. AFADHALI TANZANIA SASA IKAE CHINI YA VIONGOZI WA MITAA KUSIWE NA KIONGOZI WA SERIKALI KUU KULIKO KUMPA NCHI JAMBAZI, FISADI, NA MPENDA RUSHWA KAMA LOWASA.


Inatisha aisee! Watu wamefikia mpaka kutaka kutoa roho za wanadamu wenzao ili mradi tu waingie Ikulu pamoja na kuwa hawana hata sifa moja ya kuweza kuiongoza nchi.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom