Katibu wa Nyerere atishwa

Katibu wa Nyerere atishwa

Aidha kaomba kwa hiyari yake au kapachikiwa ukweli unabaki kuwa kapewa na Joan Wicken akaendelea kuwepoIkulu kama katibu wake muda aliokuwepo madarakani Nyerere. Kumbuka hilo.

Sasa huyu mwingine si alikuwa tarishi tu? tena pengine ni tarishi wa huyo Joan Wicken na wala si wa Nyerere.

Ukweli ubaki kuwa ukweli ingawa ni mchungu.

Ok dada. lets agree alikuwa tarishi, Kwa nini Rashidi na Lowasa walipenda kumtuma tarishi badala ya PA wa Nyerere?
 
Personal assistant tofauti na private secretary ie katibu mahsusi na katibu myeka!
 
Ok dada. lets agree alikuwa tarishi, Kwa nini Rashidi na Lowasa walipenda kumtuma tarishi badala ya PA wa Nyerere?

Sasa ulifikiri kazi ya tarishi ni nini? Unanchekesha!
 
Katibu wa Nyerere atishwa

KATIBU Myeka wa Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, Mzee Samweli Kasori, amepokea vitisho kutoka kwa watu kadhaa baada ya uamuzi wake wa ‘kufukua’ ukweli uliofichika, baada ya baadhi ya wanasiasa ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kulihusisha jina la Mwalimu Nyerere na mbio zao za urais. Hali hiyo inajitokeza ikiwa ni siku kadhaa tangu Mzee Kasori kunukuliwa na gazeti dada na hili la Raia Tanzania, kwamba baadhi ya wanasiasa wanatumia vibaya jina la Mwalimu Nyerere kwa malengo yao.

Gazeti la Raia Tanzania lilimnukuu Kasori, ikiwa ni siku kadhaa kupita tangu Mbunge wa Mbinga Magharibi, John Komba, anayedaiwa kuwamo kwenye kambi ya Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, kunukuliwa na gazeti hilo la Februari 10, mwaka huu, akidai kabla Mwalimu Nyerere hajaaga dunia alimkubali (aliridhika na) Lowassa.

“Ni kweli kwamba jina la Lowassa lilikatwa na Mwalimu kwa sababu mbalimbali, lakini Rais Mkapa alipotangaza Baraza lake la Mawaziri mwaka 1995, baada ya miaka miwili tu mwenyewe akaona kuna upungufu; akaamua kumuingiza Lowassa katika Baraza la Mawaziri. Ninaamini Mkapa alipewa ushauri na Mwalimu Nyerere,” alinukuliwa Komba. Vitisho dhidi yake Baada ya gazeti hilo la Raia Tanzania kuchapishwa likimkariri kujibu sehemu ya madai ya Komba, Mzee Kasori aliwasiliana na chumba chetu cha habari kueleza vitisho alivyopata kutoka kwa mmoja wa watumishi serikalini (jina lake na taasisi inahifadhiwa).

Katika vitisho hivyo vilivyotolewa kwa njia ya simu kwake, Kasori anatakiwa kuacha kuharibu mipango ya maisha ya watu (hata hivyo, gazeti hili halikuweza kubaini mara moja mipango hiyo inayovurugwa ya maisha ni ya nani hasa). Taarifa zaidi kutoka vyanzo vyetu kadhaa vya habari kutoka serikalini zinaeleza kwamba, Mzee Kasori amechukua hatua mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuzitaarifu baadhi ya mamlaka za juu serikalini.

“Salaam, leo Alhamisi Februari12, 2015, saa 4:45 asubuhi nimepokea simu kutoka kwa (anamtaja mtumishi wa serikali) akilalamika kwamba namharibia (anataja jina la mwanasiasa) shughuli zake za kutafuta maisha katika kuwania (anataja nafasi ya uongozi wa dola),” inaeleza sehemu ya ujumbe wa Mzee Kasori kwenda katika moja ya mamlaka za juu serikalini.

Ujumbe huo unaendelea kueleza; “Kweli huyu Mungu mpya aitwaye fedha ana nguvu za ziada ndani ya akili na mioyo yetu.”

Alichokisema Mzee Kasori Kwa kuzingatia maelezo ya Komba kama yalivyonukuliwa awali, gazeti la Raia Tanzania lilimtafuta Kasori, mmoja wa waliokuwa wasaidizi wa karibu wa Mwalimu Nyerere, ambaye aliweka bayana kwamba, haamini kama Mwalimu Nyerere aliridhishwa na Lowassa kama alivyodai Komba.

“Haya masuala nilikwishayaeleza yote na kuyaweka kwenye mtandao. Siogopi nilikwishayaweka wazi,” alianza kueleza Mzee Kasori. Katika maelezo yake hayo, Kasori anaendelea kusema: “Tanzania nzima mtakumbuka kuwa huyu Mheshimiwa Edward Lowassa alikuwa ni mmoja wa wagombea wa nafasi ya urais mwaka 1995 na akaenguliwa kwa hoja nzito ya kutokuwa muadilifu na Baba wa Taifa Mwalimu J.K. Nyerere, kwa ukweli (wala sio tuhuma) kuwa alikuwa amejilimbikizia mali nyingi kwa kipindi kifupi ndani ya CCM na Serikali.

Muda mfupi alikuwa ni mtumishi wa CCM, muda mfupi kama Mkurugenzi wa kituo cha Kimataifa cha Mikutano Arusha. “Mara baada ya kurudi Butiama, 1995, baada ya kuenguliwa kugombea nafasi ya urais, siku moja mapema asubuhi Bwana Lowassa alinipigia simu na kusema yafuatayo: “Bwana Kasori, naomba uende kumwambia Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, aende Monduli kusaidia kusafisha jina langu ili nisikose ubunge kutokana na yale aliyonisema Dodoma’.

Nilishikilia mkono wa simu (TTCL) kwa zaidi ya nusu saa tukiwa tunazungumza na hatimaye mimi nilipata ujasiri wa kumwambia Bwana Lowassa kuwa siwezi kwenda kusema maneno hayo kwa Baba wa Taifa na kwamba akitaka aje Butiama na nitamruhusu waongee ana kwa ana. Nikanyamaza na hatimaye yeye akawa wa kwanza kukata simu.

Hiyo ikawa itifaki njema kwangu! “Kesho yake tena asubuhi nilipokea simu, safari hii akawa ni Mheshimiwa Mzee Rashidi Mfaume Kawawa. Kwa maneno yake alisema, Bwana Kasori, jana ulizungumza na Edward Lowassa, naomba ufikishe ombi lake kwa Baba wa Taifa tafadhali” “Kutokana na heshima ya Mheshimiwa Mzee Kawawa, nilikubali na nikaenda na kabla ya hapo nilimuomba Mzee Kawawa akae karibu na simu ili nimpe jibu muda si mrefu. “Nilimueleza Baba wa Taifa kuwa, Mheshimiwa Edward Lowassa kupitia kwa Mheshimiwa Mzee Rashidi Mfaume Kawawa anaomba usaidie kusafisha jina lake kule jimboni kwake Monduli ili asikose ubunge kutokana na yale uliyomsema katika Kamati Kuu ya CCM Dodoma.

Jibu la Baba wa Taifa alilonipa ni kuwa, nenda umwambie Mzee Rashidi Mfaume Kawawa asiwe mjinga kama Lowassa”! “Kwa kuzingatia heshima kati ya wazee hao wawili, Kawawa sikumwambia hivyo! Badala yake nilimdanganya (nawaomba radhi tena Watanzania) jibu nililompa Mzee Kawawa ni kuwa juma lililokuwa linafuata tungekuwa Dar es Salaam na kwamba aje Msasani aongee na Baba wa Taifa.

Mheshimiwa Kawawa alikubali. “Nikarudi kwa Baba wa Taifa kusema uongo (naomba radhi tena) kuwa, Mzee Kawawa ameomba mzungumze tatizo la Lowassa tutakapofika Dar es Salaam. Baba wa Taifa alikubali na akaagiza nimuombe Mheshimiwa Mzee Kawawa kuwa Lowassa na Guninita na wapambe wengine wa Lowassa wote wafike Msasani. “Siku ya siku ikafika.

Tukawepo Msasani na Mheshimiwa Mzee Kawawa akaja. Lowassa hakuwepo! Sababu anazijua mwenyewe (muulizeni maana nasema ukweli). Mkutano ulipoanza mzungumzaji wa kwanza nikawa mimi, kueleza lengo la mkutano.

Mzungumzaji wa pili alikuwa Baba wa Taifa na swali la kwanza ni kuuliza Lowassa yuko wapi? “Bila kupoteza wakati Mwalimu alisema, Rashidi, huyu Kasori ananiambia eti niende Monduli nikasafishe jina la Mheshimiwa Lowassa eti asikose ubunge kwamba nilimchafulia Dodoma katika kikao cha Kamati Kuu ya CCM.

Kutokana na ombi lako nilimtuma akuambie usiwe mjinga kama Lowassa. Kasori alikuambia eh?” “Oneni, huko nyuma tayari nilishasema uongo kwa kutosema maneno hayo kwa Mheshimiwa Mzee Kawawa. Kweli hilo kurudiwa na Baba wa Taifa kwa Mzee Kawawa mbele yangu lilisababisha kalamu yangu kuanguka, nikatetemeka na nikatokwa na jasho jingi mbele ya hao wazee! Bila kutegemea na kwa mshangao mkubwa Mheshimiwa Mzee Kawawa alikubali kwa kuitikia “NDIO ALINIAMBIA”.

Mwalimu akacheka sana! Sababu sijui hadi leo kwa nini alicheka sana. “Kwa kuendelea, Mwalimu alimwambia Mzee Kawawa kuwa, Kasori ana umri mkubwa kuliko Lowassa. Kasori alipata taabu sana kufikisha kwangu ombi la Lowassa na aliniambia kuwa jana yake alikuwa amekataa ombi la Lowassa. Sasa nasema kuwa kwa umri wangu mimi mzee, Lowassa ni mtoto wangu tena mdogo sana. Kwa heshima mliyonayo kwangu na kwa Chama cha Mapinduzi mtanishangaa sana mkisikia niko Monduli eti nipo kwenye majukwaa nasafisha jina Bwana Lowassa asikose ubunge. “Kweli Lowassa ni jasiri sana kusema maneno hayo.

Hayo ningeambiwa na Kasori tu ningesita kumuamini. Lakini kwamba hata wewe Rashidi ulitumiwa kusema maneno hayo! Huyu Lowassa ni jasiri sana! Lakini kwa nini hajatuambia ukweli kuhusu mali hizo ambazo ni nyingi kuliko mimi ambaye nimekuwa Rais wenu kwa kipindi kirefu? Sasa Bwana Rashidi, nakuomba hivi, kamwambie mwenyekiti wa CCM Mheshimiwa Mwinyi aitishe wajumbe wote wa Kamati Kuu, chagueni tarehe na mahali popote Tanzania, mimi nitakuja kumsafisha Bwana Lowassa na nitagharamia mkutano huo kwa hela zangu.

Kamwe msitumie hela za chama wala serikali. Monduli sitokwenda, umesikia eh?” “Mkutano ukaisha hapo Msasani.

Hadi uchaguzi 1995, unafanyika na kumalizika Baba wa Taifa hakwenda Monduli. Alichukia sana tabia za Lowassa. Hadi Baba wa Taifa anafariki, sikuwahi na sijasikia wala kusoma popote ambapo Lowassa anakanusha alivyolimbikiza mali akiwa mtumishi wa CCM na serikali kwa muda mfupi kiasi cha kumzidi Rais wa Kwanza,” alidai Mzee Kasori.


Chanzo: Raia Mwema


CC: Tized, Mr Rocky, Fixed Point, Daudi Mchambuzi, lyinga, NATA, Chakaza, Elly B, Ablessed, Kill 3, everlenk, MziziMkavu, Ablessed, afrodenzi, Heaven on Earth, Power to the People, Jasusi, Eiyer, idawa, nguruvi, Mentor, Sikonge, Dingswayo, MANI, tpaul, Bramo, Bulesi Bulldog, Sangarara, MTAZAMO, Erythrocyte, Mag3, Mimibaba, zumbemkuu, Crashwise, amkawewe, Idimi, Ogah, Chakaza, mshana jr, JokaKuu, MWALLA, genekai, PRINCE CROWN, Tuko, Shark, lynxeffect22, samaki2011, MoudyBoka adolay, Elli, nyabhingi, Janjaweed, S.N.Jilala, MEANDU, Tabby, Candid Scope, Honolulu, August, dyuteromaikota, BONGOLALA, Gefu, Bigirita, Kozo Okamoto,

Mimi siko kambi ya Lowasa wala ya mtu yeyote. Lakini napata wasiwasi na maelezo haya, maana mtu mwenyewe kakili kuwa ni mwongo kamwongopea Nyerere itakuwa sisi.
Nadhani uzi huu una propaganda fulani.
 
Tatizo hapa ni jina la mama wickens,kwa sababu ni mzungu tunashabikia na kumdowngrade kasori.kasori ni msomi mzuri tu,na ndiye alikuwa katibu wa mwalimu,private secretary.leo kumwita tarishi ni kuonyesha jinsi gani mwandishi yuko biased.ana lake jambo,amelambishwa sukari ya fisadi.kama ni tarishi kwa nini kambi ya EL wanahaha kumzima mdomo?je Joe Butiku nae alikuwa nani wakati wickens akiwa bado mtumishi ie ps?
 
Nashangaa wakuu,mnataka kunasa katika mtego wa Faizafox.Yeye anaingiza kitu ambacho hakina umuhimu hapa.Kwamba mzee Kasori awe alikiwa mhudumu au tarishi hilo si la msingi.
Jambo la maana ni kwamba Lowasa alikataliwa na Mwalimu.Mwalimu akiishakukataa umekwisha.Na hili lazima tulitangaze watu wajue kuwa Lowasa alikataliwa.
 
Sasa ulifikiri kazi ya tarishi ni nini? Unanchekesha!

Usicheke dada. kumbe anachokisema Kasori ni sahihi, ila tatizo lako ni mtoa hoja na si hoja aliyoitoa? sipendi kukucheka dada maana hata Mtume Paulo ametuasa kuwarejesha kwa upole wote waliopotoka.
 
Katibu wa Nyerere kwa miaka yote alikuwa ni huyu mama wa kizungu, msitake kudanganya uongo usio na mpango, huyo mnaesema labda alikuwa tarishi wa Nyerere, Nyerere hakuwahi kumuamini Mwaafrika mwenzake kuwa katibu wake, kwa miaka yote aliyokuwa Ikulu:



Queen Elizabeth II, J.K. Nyerere and former Personal Assistant to Nyerere, Joan Wicken

Sio kwamba hujui unachokisema ila unajitoa akili kwa sababu zako za UDINI uliokujaa hadi kwenye hilo juba lako...mdini mkubwa wewe! Unafahamu maana ya KATIBU MYEKA weye ajuza au unapendaga kujitoa akili bila sababu? Tofautisha kati ya PA na Katibu Myeka....na usitake kutubadilishia mada.

baada ya maCCM kuona mmebanwa kotekote, mmeanza kuwatisha watu na kuwateaua wakuu wa wilaya kwa ajili ya kupitisha katiba ya CCM na kuiba kura. hamuambulii kitu mwaka huu, wapuuzi wakubwa!
 
Sio kwamba hujui unachokisema ila unajitoa akili kwa sababu zako za UDINI uliokujaa hadi kwenye hilo juba lako...mdini mkubwa wewe! Unafahamu maana ya KATIBU MYEKA weye ajuza au unapendaga kujitoa akili bila sababu? Tofautisha kati ya PA na Katibu Myeka....na usitake kutubadilishia mada.

baada ya maCCM kuona mmebanwa kotekote, mmeanza kuwatisha watu na kuwateaua wakuu wa wilaya kwa ajili ya kupitisha katiba ya CCM na kuiba kura. hamuambulii kitu mwaka huu, wapuuzi wakubwa!

Ewe punguani pitia nyuzi wacha kiherehere, hilo swali nimeshalijibu.

Joan Wicken ndiye katibu wa Nyerere huyo mwingine mnaemoachika labda alikuwa ni tarishi tu wa Ikulu hakuna zaidi.
 
Usicheke dada. kumbe anachokisema Kasori ni sahihi, ila tatizo lako ni mtoa hoja na si hoja aliyoitoa? sipendi kukucheka dada maana hata Mtume Paulo ametuasa kuwarejesha kwa upole wote waliopotoka.

Sasa Paulo au Joan Wicken ndiyo alikuwa katibu wa Nyerere?
 
Sasa Paulo au Joan Wicken ndiyo alikuwa katibu wa Nyerere?

Umeshamsahau MTUME Paulo mara hii dada? -usijali nitakukumbusha, ni yule tuliyekuwa tukimsoma huko nyuma kuwa katuasa kutii mamlaka. Warumi 13:1Neno: Bibilia Takatifu (SNT)

Kutii Mamlaka.
Katuasa mengi dada, ikiwemo kuwarejesha kwa upole mnaopotosha kwa kumjadili mtoa hoja badala ya hoja aliyoitoa.
Nimeahidi sitakucheka, na nawasihi ma-Great Thinkers wengine wasikucheke bali wakusaidie kwa upole kama MTUME Paulo alivyotuagiza.
 
“Salaam, leo Alhamisi Februari12, 2015, saa 4:45 asubuhi nimepokea simu kutoka kwa (anamtaja mtumishi wa serikali) akilalamika kwamba namharibia (anataja jina la mwanasiasa) shughuli zake za kutafuta maisha katika kuwania (anataja nafasi ya uongozi wa dola),” inaeleza sehemu ya ujumbe wa Mzee Kasori kwenda katika moja ya mamlaka za juu serikalini.

Ndugu yangu BAK leo umenisikitisha, hapa ni JF ulipaswa kumwaga jina la mtoa vitisho na idara anayofanyia kazi
 
Aisee, kivulicha Lowa- hasa kinatisha! Maembe na team nyingine zote wanapambana na Lowa-hasa tu, he is definitely a force to reckon with!

LEO CCM mna-highlight 'wizi' wa Lowasa uliokua unajulikana toka 1995 na Nyerere. Kwa mwenye akili atahoji: Ikawaje akaja kuwa Prime Minister? Ikaweje Rais cum M/Kiti wa chama chenu akamkubali akapendekeza jina lake kwa Bunge ili awe Waziri Mkuu? Ama mtasema CCM haihusiki na nafasi ya Uwaziri Mkuu?

Na ikawaje alipokumbwa na kashfa ya RICHMOND you the so called CCM Members hamkukomalia 'wizi' wake kwa nguvu stahiki kipindi hicho mnakurupuka now mnaacha kujadili 'issues' mnajadili watu?

And if 'usafi' is an issue, then nani alie msafi CCM? (Na kama yupo hilo genge lenu linalo-run CCM limemweka nafasi gani?) Je,ni huyu anaehonga wilaya? Ni huyu asie makini na teuzi zake? Ni huyu anaefanya biashara ikulu na familia yake? Ni huyu aliyeunda tume ya maadili ya viongozi isiyo na meno?

Msipende kuwaona watu ni wapu.mbav.u kiasi hicho wa.ji.nga nyinyi!

Jipangeni upya!
 
2015 Raia Mwema vs Edward Lowassa, baada tu uchaguzi linauzwa hili gazeti na itakuja New spinning machine!!!

Tutavuka tu 2015, SIMAMA UHESABIWE
 
Sasa Paulo au Joan Wicken ndiyo alikuwa katibu wa Nyerere?
Kasema " Mtume Paulo ametuasa hivi" Sasa mtume Paulo anaweza kuwa katibu wa Nyerere? Wewe lazima uchokoze watu kwa kuwapeleka huko ujuapo ili furaha yako itimie. Kwani Mwamedi anaweza kuwa katibu wa JK?
 
Back
Top Bottom