TANZIA Katibu wa CCM wilaya ya Mkuranga afariki dunia

TANZIA Katibu wa CCM wilaya ya Mkuranga afariki dunia

Hebu Tazama hapa
 

Attachments

  • Screenshot_20250826_144544.jpg
    Screenshot_20250826_144544.jpg
    261.8 KB · Views: 13
Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Mafia mkoani Pwani, Salehe Kikweo amefariki dunia wakati akiendelea kupatiwa matibabu Hospitali ya Mji Handeni, Mkoa wa Tanga.

Taarifa ya kifo hicho imetolewa na Katibu wa CCM, Wilaya ya Handeni, Mayassa Kimbau leo Jumanne Agosti 26, 2025 kupitia mitandao ya kijamii na kueleza Kikweo amefariki dunia asubuhi ya leo hospitalini hapo na mwili wake umehifadhia hapohapo.

Amesema taarifa zaidi kuhusu wapi yatafanyika mazishi yake itatolewa baadaye baada ya familia na viongozi wengine kukutana ili kupanga taratibu vizuri. Kikweo ni mwenyeji wa Handeni.

"Nimepokea kwa masikitiko makubwa sana taarifa ya msiba wa ndugu yetu, kaka yetu mpendwa Kikweo aliyefariki asubuhi hii ya leo na mwili umehifadhiwa Hospitali ya Bomani, mipango ya mazishi inaendelea kufanyika," imeeleza taarifa hiyo.

Akizungumzia msiba huo, Mwenyekiti wa CCM, wilayani Handeni, Amiri Changogo ambaye ni mmoja wa viongozi aliyefanya kazi na katibu huyo kwa muda, amesema kifo cha Kikweo kimetokea ghafla na wala hajaugua.

Maandiko matakatifu yanatutaka kumshukuru Mungu kwa kila jambo!
 
Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Mafia mkoani Pwani, Salehe Kikweo amefariki dunia wakati akiendelea kupatiwa matibabu Hospitali ya Mji Handeni, Mkoa wa Tanga.

Taarifa ya kifo hicho imetolewa na Katibu wa CCM, Wilaya ya Handeni, Mayassa Kimbau leo Jumanne Agosti 26, 2025 kupitia mitandao ya kijamii na kueleza Kikweo amefariki dunia asubuhi ya leo hospitalini hapo na mwili wake umehifadhia hapohapo.

Amesema taarifa zaidi kuhusu wapi yatafanyika mazishi yake itatolewa baadaye baada ya familia na viongozi wengine kukutana ili kupanga taratibu vizuri. Kikweo ni mwenyeji wa Handeni.

"Nimepokea kwa masikitiko makubwa sana taarifa ya msiba wa ndugu yetu, kaka yetu mpendwa Kikweo aliyefariki asubuhi hii ya leo na mwili umehifadhiwa Hospitali ya Bomani, mipango ya mazishi inaendelea kufanyika," imeeleza taarifa hiyo.

Akizungumzia msiba huo, Mwenyekiti wa CCM, wilayani Handeni, Amiri Changogo ambaye ni mmoja wa viongozi aliyefanya kazi na katibu huyo kwa muda, amesema kifo cha Kikweo kimetokea ghafla na wala hajaugua.

Kura za maoni isingewezekana ziishe hivi hivi
 
Mungu ni mkali soon atafikia lengo!!
KAZI ni kipimo cha utu
 
Maswaahiba wenzake walipenda kumuita kipara....rip katibu bingwa kabisa.
 
Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa MUNGU, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa. ILA AOMBE KWA IMANI, PASIPO SHAKA YEYOTE; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo, na kupeperushwa huku na huku. Maana mtu kama yule asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa BWANA. Mtu wa nia mbili husita-sita katika njia zake zote.”
Kwenye maombi Kuna Imani ya kuomba na kuna Imani ya kupokea.
 
Jamaa wajitafakari sana.

Wananchi wamewachoka kabisa.
 
Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Wilaya ya Mafia mkoani Pwani, Salehe Kikweo amefariki dunia wakati akiendelea kupatiwa matibabu Hospitali ya Mji Handeni, Mkoa wa Tanga.

Taarifa ya kifo hicho imetolewa na Katibu wa CCM, Wilaya ya Handeni, Mayassa Kimbau leo Jumanne Agosti 26, 2025 kupitia mitandao ya kijamii na kueleza Kikweo amefariki dunia asubuhi ya leo hospitalini hapo na mwili wake umehifadhia hapohapo.

Amesema taarifa zaidi kuhusu wapi yatafanyika mazishi yake itatolewa baadaye baada ya familia na viongozi wengine kukutana ili kupanga taratibu vizuri. Kikweo ni mwenyeji wa Handeni.

"Nimepokea kwa masikitiko makubwa sana taarifa ya msiba wa ndugu yetu, kaka yetu mpendwa Kikweo aliyefariki asubuhi hii ya leo na mwili umehifadhiwa Hospitali ya Bomani, mipango ya mazishi inaendelea kufanyika," imeeleza taarifa hiyo.

Akizungumzia msiba huo, Mwenyekiti wa CCM, wilayani Handeni, Amiri Changogo ambaye ni mmoja wa viongozi aliyefanya kazi na katibu huyo kwa muda, amesema kifo cha Kikweo kimetokea ghafla na wala hajaugua.

Leo wamekufa wengi
 
Back
Top Bottom