Mzalendo120
JF-Expert Member
- Jul 2, 2022
- 1,408
- 1,818
Ninawasalim wanajukwaa.
Moja kwa moja kwenye mada nikwamba yupo mtumishi mmoja ambae alikua mkuu wa shule moja ndani ya jiji la Tanga lakini alituhumiwa kufanya ubadhirifu wa mali ya umma takukuru walipoingilia kati mkuu huyo alisimamishwa kazi apishe uchunguzi
Kilichotokea ni mkuu huyo kurudishwa kazini na kupandishwa cheo akawa afisaelimu kata.
Jambo la ajabu ila lenye ukweli nikwamba bado mwalimu huyo ni afisaelimu kata ya Mabokweni ingawa DPP ametoa kibali mwalimu huyo apelekwe mahakamani na ameshapelekwa kwa zaidi ya wiki mbili sasa ikiwa shtaka lake ni uhujumu uchumi
Mtumishi huyo kuendelea kushikilia nafasi hiyo wakati tunaona watumishi wa umma waliotuhumiwa wamevuliwa madaraka inaleta ukakasi
Kwapicha hiyo wahusika waliompandisha cheo mtumishi huyo nikudharau mamlaka zilizowateua, kuendelea kudharau hata ofisi ya DPP na kuipa jamii taswira kwamba wizi kwa baadhi ya watumishi unaweza kukufanya upandishwe cheo hasa kama unafahamiana vizuri na mabosi zako
Ninaona kama hakuna uzembe kwa viongozi waliomteua mtumishi huyo basi inawezekana kuna harufu ya rushwa
Moja kwa moja kwenye mada nikwamba yupo mtumishi mmoja ambae alikua mkuu wa shule moja ndani ya jiji la Tanga lakini alituhumiwa kufanya ubadhirifu wa mali ya umma takukuru walipoingilia kati mkuu huyo alisimamishwa kazi apishe uchunguzi
Kilichotokea ni mkuu huyo kurudishwa kazini na kupandishwa cheo akawa afisaelimu kata.
Jambo la ajabu ila lenye ukweli nikwamba bado mwalimu huyo ni afisaelimu kata ya Mabokweni ingawa DPP ametoa kibali mwalimu huyo apelekwe mahakamani na ameshapelekwa kwa zaidi ya wiki mbili sasa ikiwa shtaka lake ni uhujumu uchumi
Mtumishi huyo kuendelea kushikilia nafasi hiyo wakati tunaona watumishi wa umma waliotuhumiwa wamevuliwa madaraka inaleta ukakasi
Kwapicha hiyo wahusika waliompandisha cheo mtumishi huyo nikudharau mamlaka zilizowateua, kuendelea kudharau hata ofisi ya DPP na kuipa jamii taswira kwamba wizi kwa baadhi ya watumishi unaweza kukufanya upandishwe cheo hasa kama unafahamiana vizuri na mabosi zako
Ninaona kama hakuna uzembe kwa viongozi waliomteua mtumishi huyo basi inawezekana kuna harufu ya rushwa