Huko jijini Arusha waziri mkuu Kasim Majaliwa amewasimamisha kazi baadhi ya watumishi wapishe uchunguzi kwa tuhuma za matumizi mabaya ya ofisi.
Baadhi ya tuhuma hizo zilizoelekezwa kwa mkurugenzi na timu yake ni kugawana fedha za umma na kuingizia fedha hizo kwenye akaunti binafsi za watumishi wa halmashauri.
Pia wamehamishwa watumishi hamsini na halmashauri hiyo ndani ya mwaka mmoja. Mpaka vibarua wamehamishwa halmashauri na mkurugenzi huyo.
Sasa turejee jijini Tanga
Kama ukidhani hicho ulichoona Arusha ni matumizi mabaya ukalalamika sasa Tanga ungeweza hata kuwasweka ndani kabisa.
Aliyekua mkurugenzi wa jiji la Tanga ambaye kwasasa hayupo Tanga bwana Mayeji,amewahi kufanya ubadhirifu unaofanana na huo akishirikiana na afisa elimu sekondari na mkuu mmoja wa shule.
Fedha zilitolewa kwenye akaunti ya serikali bila utaratibu halafu wakapewa wazabuni hewa. Mkurugenzi aliagiza vifusi kwa magari ya halmashauri hela akapewa yeye. Tenda za ujenzi na manunuzi hazikufanyika mkuu wa shule alinunua vifaa vyote alikokujua bila kushirikisha kamati. Malighafi kibao zilienda kujenga nyumba ya mkuu mmoja wa shule(ambaye ni mwanamke) na amelindwa na afisaelimu hadi leo.
Mbali na kwamba mkuu huyo wa shule alisimamishwa kupisha uchunguzi wa TAKUKURU,kabla ya uchunguzi kuisha aliitwa akawa anahudumu ndani ya ofisi ya afisaelimu. Wanaogopa kumuwajibisha maana waliiba wote halafu mkuu huyo wa shule aliahidi kwamba hatofungwa au kulipishwa mwenyewe.
Baada ya timu ya ufuatiliaji kutoka tamisemi kufika Tanga, afisaelimu na mkurugenzi waliulizwa kwanini wakae na mtuhumiwa? Kwa aibu walimuondoa ofisini huyo mtu wao.
Hata hivyo mkurugenzi aliyepo sasa nae ameungana na afisaelimu kwa kumpa mwalimu huyo uafisaelimu kata. Tanga wezi wanapongezana na kupandishana vyeo.
Suala la kuhamisha watumishi ili kuficha maovu,Tanga jiji ndio kilio kilichopo. Katika shule ulipofanyika ubadhirifu waliondolewa walimu 17 ndani ya wiki moja (tena bila kulipwa stahili zao)eti wamekua wasumbufu wamemsumbua mkuu wa shule. Kumbe kukataa kushiriki wizi ni kusumbua mamlaka. Kisa ni mtu wao kwa Tanga jiji hilo lipo wazi.
Afisa Elimu alisema kwanini akitoa maagizo walimu wapinge? Amekula hela na mkuu wa shule sasa anawashawishi walimu wakamsafishe yeye,mkuu wa shule na mkurugenzi huko takukuru.
Takukuru kuwa kimya
Nizaidi ya miaka miwili taasisi hiyo ipo kimya. Imeungana na wezi hao kwani ushahidi uliotolewa takukuru na watumishi hao,mkurugenzi wakipindi hicho na afisaelimu walielezwa kilichosemwa na kila mtu. Baadae waliotoa ushahidi wameendelea kunyanyaswa na mkurugenzi na afisaelimu na wakifika takukuru wengine walifukuzwa na wengine waliwekwa ndani. Takukuru walinunuliwa na aliyekua mkurugenzi wa jiji.
Hata hivyo aliyekua mkuu wa takukuru alisimamishwa kazi kwa tuhuma za rushwa lakini bado afisaelimu na mkuu wake wa shule wanajisifu mtaani eti wao nimakada watiifu.
Mh. Waziri mkuu ukistaajabu ya Arusha ya Tanga yatakuliza. Timu hiyo ya wizi na mabingwa wa kila aina ya rushwa unayoijua wapo wanakula mali ya umma huku wakiita Tanga shamba la bibi.
Mh. Waziri mkuu hata wakaguzi wa nje walinunuliwa na Mayeji bingwa wa kila aina ya rushwa. Ingawa Mayeji hayupo Tanga lakini ameacha waumini wake (wa kila aina ya rushwa)Tanga jiji. Mh. Waziri mkuu tuma timu yako ya watu makini kwani kama wakiwa legelege watakirimiwa kwa kila watakachokitaka na baadhi ya haohao walarushwa na watanyong'onyea
Baadhi ya tuhuma hizo zilizoelekezwa kwa mkurugenzi na timu yake ni kugawana fedha za umma na kuingizia fedha hizo kwenye akaunti binafsi za watumishi wa halmashauri.
Pia wamehamishwa watumishi hamsini na halmashauri hiyo ndani ya mwaka mmoja. Mpaka vibarua wamehamishwa halmashauri na mkurugenzi huyo.
Sasa turejee jijini Tanga
Kama ukidhani hicho ulichoona Arusha ni matumizi mabaya ukalalamika sasa Tanga ungeweza hata kuwasweka ndani kabisa.
Aliyekua mkurugenzi wa jiji la Tanga ambaye kwasasa hayupo Tanga bwana Mayeji,amewahi kufanya ubadhirifu unaofanana na huo akishirikiana na afisa elimu sekondari na mkuu mmoja wa shule.
Fedha zilitolewa kwenye akaunti ya serikali bila utaratibu halafu wakapewa wazabuni hewa. Mkurugenzi aliagiza vifusi kwa magari ya halmashauri hela akapewa yeye. Tenda za ujenzi na manunuzi hazikufanyika mkuu wa shule alinunua vifaa vyote alikokujua bila kushirikisha kamati. Malighafi kibao zilienda kujenga nyumba ya mkuu mmoja wa shule(ambaye ni mwanamke) na amelindwa na afisaelimu hadi leo.
Mbali na kwamba mkuu huyo wa shule alisimamishwa kupisha uchunguzi wa TAKUKURU,kabla ya uchunguzi kuisha aliitwa akawa anahudumu ndani ya ofisi ya afisaelimu. Wanaogopa kumuwajibisha maana waliiba wote halafu mkuu huyo wa shule aliahidi kwamba hatofungwa au kulipishwa mwenyewe.
Baada ya timu ya ufuatiliaji kutoka tamisemi kufika Tanga, afisaelimu na mkurugenzi waliulizwa kwanini wakae na mtuhumiwa? Kwa aibu walimuondoa ofisini huyo mtu wao.
Hata hivyo mkurugenzi aliyepo sasa nae ameungana na afisaelimu kwa kumpa mwalimu huyo uafisaelimu kata. Tanga wezi wanapongezana na kupandishana vyeo.
Suala la kuhamisha watumishi ili kuficha maovu,Tanga jiji ndio kilio kilichopo. Katika shule ulipofanyika ubadhirifu waliondolewa walimu 17 ndani ya wiki moja (tena bila kulipwa stahili zao)eti wamekua wasumbufu wamemsumbua mkuu wa shule. Kumbe kukataa kushiriki wizi ni kusumbua mamlaka. Kisa ni mtu wao kwa Tanga jiji hilo lipo wazi.
Afisa Elimu alisema kwanini akitoa maagizo walimu wapinge? Amekula hela na mkuu wa shule sasa anawashawishi walimu wakamsafishe yeye,mkuu wa shule na mkurugenzi huko takukuru.
Takukuru kuwa kimya
Nizaidi ya miaka miwili taasisi hiyo ipo kimya. Imeungana na wezi hao kwani ushahidi uliotolewa takukuru na watumishi hao,mkurugenzi wakipindi hicho na afisaelimu walielezwa kilichosemwa na kila mtu. Baadae waliotoa ushahidi wameendelea kunyanyaswa na mkurugenzi na afisaelimu na wakifika takukuru wengine walifukuzwa na wengine waliwekwa ndani. Takukuru walinunuliwa na aliyekua mkurugenzi wa jiji.
Hata hivyo aliyekua mkuu wa takukuru alisimamishwa kazi kwa tuhuma za rushwa lakini bado afisaelimu na mkuu wake wa shule wanajisifu mtaani eti wao nimakada watiifu.
Mh. Waziri mkuu ukistaajabu ya Arusha ya Tanga yatakuliza. Timu hiyo ya wizi na mabingwa wa kila aina ya rushwa unayoijua wapo wanakula mali ya umma huku wakiita Tanga shamba la bibi.
Mh. Waziri mkuu hata wakaguzi wa nje walinunuliwa na Mayeji bingwa wa kila aina ya rushwa. Ingawa Mayeji hayupo Tanga lakini ameacha waumini wake (wa kila aina ya rushwa)Tanga jiji. Mh. Waziri mkuu tuma timu yako ya watu makini kwani kama wakiwa legelege watakirimiwa kwa kila watakachokitaka na baadhi ya haohao walarushwa na watanyong'onyea