Uchaguzi 2020 Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally ndani ya Dakika 45 leo Septemba 14

jingalao

JF-Expert Member
Oct 12, 2011
35,053
28,245
Katibu Mkuu wa CCM(T) Msomi Dkt. Bashiru Ally anatarajiwa kuwepo katika kipindi cha TV cha Dakika 45 (ITV).
Unakaribishwa kusikia

1 - Mambo makubwa yaliyofanywa na CCM Kimataifa, kikanda, kitaifa hadi ngazi ya Kata na vijiini kwa kipindi kifupi cha miaka mitano ya Rais Magufuli.

2 - Sera na Ilani mpya ya CCM

3 - Ufafanuzi wa maswala mbalimbali kuhusu CCM na wanachama wake

4 - Muelekeo wa Kampeni

5 - Tathmini ya mapokeo ya jamii kwa Wagombea wa CCM.

Dkt. Bashiru hataropoka bali ataeleza kwa ustadi wa kisomi ndani ya Dk 45.

===

Bashiru: Tuwe na kumbukumbu, swala la kupita bila kupingwa si jipya tangu mwaka 1995. Hata ccm wanalalamika na wameweka pingamizi, na hata wao pia wamewekewa pingamizi.

Wanaolalamika wanapaswa kupeleka malalamiko kwenye kamati ya maadili ya uchaguzi, hata walipokuwa wanaomba teuzi ilikuwa lazima ajaze fomu ya maadili ya uchaguzi, na fomu ya gharama za uchaguzi.

Hatukuruhusu wajaze bila usimamizi, pia waseme watatumia kiasi gani kwenye gharama za uchaguzi, na mimi nisipolishughulikia hilo nitawajibishwa ndani ya chama, kulikuwa na mafunzo kwa makatibu na wanasheria wote wakigawana maeneo kwa wajumbe wote

Matokeo, wanalalamika kabla ya kupata kipinga katika sanduku la kura.

Jinsi watakavyofanya kampeni.
Tutafuata wapiga kura nyumba kwa nyumba, tumejipanga kutangaza ilani yetu kwenye vyombo vya habari mitandao ya kijamii.

Watu unaowaona hawajaandaliwa, wamevutiwa na wanaoyaona, swala sio kulaumu bali kujifunza umekosea wapi au mwenzako mwenye nguvu anaweza wapi.

Kuhusu Hoja za Uongo
Wapinani wetu wameanza kutuchafua kwa kusema uwongo, swala sio kulalamika swala ni kujibu hoja, matarajio yetu wataanza kubadilika, tunapozungumza mmoja wa wagombea urais yupo Dubai, na kule kuna wanachama wetu wamemuona, mgombea wa kwetu yupo Geita akitoka Geita anaenda Kagera kisha ataenda Kigoma.

Sasa huyu aliyekwenda Dubai akishindwa akisema ameonewa wapiga kura watampima. Kipande kingine ni kuanzia tarehe 12 Zanzibar, tunashindanisha watu na sifa, tunashindanisha vyama, tunashindanisha rekodi kijumlisha hayo ndio unapata mitambo.

Kutumia, wasanii na kuwabeba watu na magari
Nani kasema wasiwatumie, wasanii sio watumwa, unawezaje kumbeba Diamond, Alikiba, Zuchu, Mrisho, Mpoto, wasanii ni watu wenye akili na ujuzi ukiona wameenda sehemu kuna jambo jema. Kwa taarifa yako wasanii wanajitolea.. wanafanya kazi ktk mazingira magumu, wasanii wengine wako wanatafuta kura.

Wakulima, wafugaji na wasanii wanatuunga mkono hao wote wanaletwa na malori, na hii wanayoona ni midogo iko mikutano haionyeshwi kwenye vyombo vya habari, na wao wajaribu kutafuta wasanii tuone watapata wasanii wangapi

Chama hiki kina uwezo na nguvu kubwa... fikra itikadi na falsafa.
 
14 September 2020
Mahojiano haya yalirekodiwa mjini Dodoma katika Ofisi Kuu ya CCM Makao Makuu
🔴#Dakika45 na Bashiru Ally, Katibu Mkuu CCM.

.................................................................................
Dah ! Mgombea wa CCM Mpya John Pombe Joseph Magufuli sijawahi kumuona akifanyiwa mahojiano ya aina yoyote na chombo cha habari wala kushiriki katika mdahalo kushindanisha mipango na maono yake.
BASHIRU ALLY KAKURWA AKIWA GEITA 14/09/2020

Mambo yakiharibika wanaCCMpya wanaelekeza lawama siyo kwa Mgombea wao bali kwa wataalamu na wasaidizi kama Bashiru Ally kushauri kununua wanasiasa wa upinzani, Dr. Philip Mpango sera za fedha & Uchumi, Humphrey Polepole dhana potovu kuwa upinzani utakuwa umekufa 2020, Prof. Palamagamba Kabudi kuhusu korosho n.k kwa kumshauri mgombea wao vibaya.

Ingekuwa kipindi hiki hakijarekodiwa basi tungempelekea mtangazaji Fardhia Middle kuhoji vipi ACT-Wazalendo, CHADEMA, CUF, CHAUMMA wote waliwapeleka wagombea wa urais ktk kipindi pendwa cha Dakika 45 ITV Tanzania kuelezea na kutetea toka ndani ya mioyo yao sera, mipango na maono yao lakini CCM Mpya wanamficha mgombea wao asije studio kuhojiwa ?
 
Dah ! Mgombea wa CCM Mpya John Pombe Joseph Magufuli sijawahi kumuona akifanyiwa mahojiano ya aina yoyote na chombo cha habari wala kushiriki katika mdahalo kushindanisha mipango na maono yake.

Mambo yakiharibika wanaCCMpya wanaelekeza lawama siyo kwa Mgombea wao bali kwa wataalamu na wasaidizi kama Bashiru Ally kushauri kununua wanasiasa wa upinzani, Dr. Philip Mpango sera za fedha & Uchumi, Humphrey Polepole dhana potovu kuwa upinzani utakuwa umekufa 2020, Prof. Palamagamba Kabudi kuhusu korosho n.k kwa kumshauri mgombea wao vibaya.

Kila chama na mikakati yake, wao CHADEMA wamempeleka Lissu kwenye hicho kipindi, Magu yeye ameamua kutembea kijiji kwa kijiji, kila mtu ashinde mechi zake tusilazimishane njia za kupiga kampeni.
 
Comrade unatakiwa ujue kuwa iyo clip uliyoipakia hapa ni mwaka jana. Kwasasa tunafanya tathimini juu ya mwelekeo wa uchaguzi. Na kwa mwenendo wa kampeni unavyoenda pasi ya shaka Magufuli anashinda kwa kishindo
Kwa kuzomewa Mbeya na Kanda ya ziwa? Hivi nikuulize, wasanii siku ya kupiga kura watakuwepo kloa mahali wanatumbuiza? Wapiga kura watakuwa bado wanakumbuka muziki na diamond na kutoa kura? Nadhani unachopashwa kukijenga ni IMANI! Imani can move mountains hata pasipokuwepo muziki!
 
Comrade unatakiwa ujue kuwa iyo clip uliyoipakia hapa ni mwaka jana. Kwasasa tunafanya tathimini juu ya mwelekeo wa uchaguzi. Na kwa mwenendo wa kampeni unavyoenda pasi ya shaka Magufuli anashinda kwa kishindo

Prof. Rwekaza S. Mukandala wa UDSM amefanya uchambuzi wa kisayansi ktk siasa (political science) ambao haujapitwa na wakati, na ndiyo maana tunaona jinsi uchaguzi wa Oktoba 2020 ni mgumu kama Prof. Mukandala alivyotabiri katika kongamano hilo na ni kipimo kizuri kumpima mwanasiasa.

Kesho katibu mkuu wa CCM Mpya akimwakilisha mgombea wa CCM Mpya ngazi ya Urais atapimwa kufuatana na vigezo vingi ikiwemo haya yaliyosemwa UDSM kuhusu utawala na siasa kuelekea 2020.

Tuisubiri kesho wakati kipindi hiki kikirushwa hewani kupitia televisheni ya ITV tumchambue mgombea wa CCM pamoja na harakati zake za kujaribu kukiletea ushindi chama chake cha CCM hapo Oktoba 2020.
 
Kwa kuzomewa Mbeya na Kanda ya ziwa? Hivi nikuulize, wasanii siku ya kupiga kura watakuwepo kloa mahali wanatumbuiza? Wapiga kura watakuwa bado wanakumbuka muziki na diamond na kutoa kura? Nadhani unachopashwa kukijenga ni IMANI! Imani can move mountains hata pasipokuwepo muziki!
Comrade umeshawahi kijiuliza kazi ya kengele kanisani na adhana misikitini ni nini? Wasanii wanakuja kutoa burudani maana kazi na dawa pia ni mbinu ya kuwavuta watu waje wasikilize sera makini za chama cha mapinduzi.
 
kuwavuta watu waje wasikilize sera makini za chama cha mapinduzi.
Anayeletwa na muziki, haji kusikiliza sera. Kilichomleta ni muziki! CDM hakuna musiki, hakuna matangazo maana yote wamezimiwa na serikali, lkn watu wanakuja in lakhs wenyewe. This translates kuwa kuna IMANI ndani yao inayowavuta! Hawa wanakuja kusikiliza matumaini ya "upomyaji", sera za uponyaji and the like!
 
Prof. Rwekaza S. Mukandala wa UDSM amefanya uchambuzi wa kisayansi ktk siasa (political science) ambao haujapitwa na wakati, na ndiyo maana tunaona jinsi uchaguzi wa Oktoba 2020 ni mgumu kama Prof. Mukandala alivyotabiri katika kongamano hilo na ni kipimo kizuri kumpima mwanasiasa.

Kesho katibu mkuu wa CCM Mpya akimwakilisha mgombea wa CCM Mpya ngazi ya Urais atapimwa kufuatana na vigezo vingi ikiwemo haya yaliyosemwa UDSM kuhusu utawala na siasa kuelekea 2020.

Tuisubiri kesho wakati kipindi hiki kikirushwa hewani kupitia televisheni ya ITV tumchambue mgombea wa CCM pamoja na harakati zake za kujaribu kukiletea ushindi chama chake cha CCM hapo Oktoba 2020.
Katibu mkuu anaenda kupiga msumari wa mwisho kwenye jeneza la chadema. Uchambuzi wa prof. Umefanyika mwaka jana mambo yamebadilika imani ya wananchi kwa ccm imezidi kuongezeka
 
Anayeletwa na muziki, haji kusikiliza sera. Kilichomleta ni muziki! CDM hakuna musiki, hakuna matangazo maana yote wamezimiwa na serikali, lkn watu wanakuja in lakhs wenyewe. This translates kuwa kuna IMANI ndani yao inayowavuta! Hawa wanakuja kusikiliza matumaini ya "upomyaji", sera za uponyaji and the like!
Comrade tukutane tena October naimani hutaikimbia I'd yako
 
Wasanii wanaotembea na Magufuli kwenye kampeni za urais ni sawa na ubwabwa wa Mzee Rungwe. Vyote ni rushwa na kutojiamini uwezo wako wa kuvuta watu kuja kukusikiliza.
 
Katibu mkuu anaenda kupiga msumari wa mwisho kwenye jeneza la chadema. Uchambuzi wa prof. Umefanyika mwaka jana mambo yamebadilika imani ya wananchi kwa ccm imezidi kuongezeka

Imani hujengwa kwa ushawishi, hii hii CCM Mpya chama dola kilichokosa mvuto wa hoja iliyoahidi kufuta kabisa vyama vya upinzani 2020 kwa kuzuia kibabe shughuli za kisiasa kwa miaka 5 wapinzani wafutike uchaguzi uwe mwepesi.

CCM Mpya inayotamani ushindi wa mezani kwa kuogopa uchaguzi huru kupitia sanduku la kura, iliyoweka makada kama wasimamizi wa uchaguzi chini ya mwamvuli wa Wakurugenzi ma-DED ili wagombea wa CCM wapite bila kupingwa ktk uchaguzi usio wa haki na huru ndiyo imeweza kujenga imani ?
 
Imani hujengwa kwa ushawishi, hii hii CCM Mpya chama dola iliyoahidi kufuta kabisa vyama vya upinzani 2020 kwa kuzuia kibabe shughuli za kisiasa kwa miaka 5 wapinzani wafutike uchaguzi uwe mwepesi, iliyoweka makada kama wasimamizi wa uchaguzi chini ya mwamvuli wa Wakurugenzi ma-DED ili wagombea wa CCM wapite bila kupingwa ndiyo imeweza kujenga imani ?
Vyama vya siasa vipo kwa mujibu wa katiba, unaposema ccm iliahidi kuvifuta kabisa utakuwa na ushahidi wa hilo. Karibu sana comrade katika kutuletea muswada wa sheria ya kuvifuta vyama vya upinzani uliopelekwa bungeni na chama dola ccm.
Karibu.
 
Back
Top Bottom