Katibu Mkuu wa CCM akutana na Balozi wa Angola nchini

BWANKU M BWANKU

JF-Expert Member
Jan 12, 2019
328
414
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ndg. Daniel Chongolo amefanya mazungumzo na Balozi wa Angola nchini Tanzania Mhe. Sandro de Oliveira

Mazungumzo hayo yamefanyika leo tarehe 09 Septemba, 2021 Makao Makuu ya CCM Dodoma, ambapo Balozi aliambatana na mwakilishi wa Chama Tawala cha Angola MPLA Ndg. Antonio Lobito

Pamoja na mambo mengine, Mazungumzo hayo yamelenga kuimarisha uhusiano wa kihistoria uliopo kati ya nchi hizi mbili za Tanzania na Angola, ikiwa ni pamoja na Vyama vya Ukombozi vya CCM na MPLA uliojengwa na waasisi wa Mataifa hayo, Mwalimu Julius Nyerere na Agustino Netho.

Aidha katika hatua nyingine, Balozi amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa uongozi wake wenye maono na wenye kuwajali Watanzania katika kufikia maendeleo ya kweli.


IMG-20210909-WA0016.jpg


IMG-20210909-WA0017.jpg


IMG-20210909-WA0018.jpg


IMG-20210909-WA0019.jpg


IMG-20210909-WA0020.jpg
 
Back
Top Bottom