Katiba: Rais Kikwete kuusaini Muswada wa Tume ya Kusanya Maoni ya Katiba kwa Kishindo!

Hii inaweza kuwa catch 22:

a. Kikwete akikataa kuusaini mswada huu kuwa sheria ataonekana amedharau maamuzi ya wabunge wake ambao kwa mbwembwe na vijembe waliupigia debe kuwa ni mswada mzuri.

b. Akiamua kuuweka sahihi (kitu ambacho ndio kinauwezekenao mkubwa) bila kuufanyia marekebisho atakuwa ameonekana kudharau na kukataa kabisa hoja za CDM na hivyo kuwafanya CDM waonekane mashujaa kwani ni wao waliotoa ofa ya kuomba kukutana naye na ni wao ambao hawakuchukua msimamo mkali bado na hivyo akiwakatalia CDM wataonekana wana hekima zaidi. Watasema "tumejitahidi na mmetuona lakini Rais kaweka pamba masikioni" kwa hiyo tunarudi mitaani! Well.. kila mtu kaona wamejitahidi.

c. Akiamua kuusaini na kuuridisha tena Bungeni bado tatizo litakuwa pale pale kwani hoja ya madaraka makubwa aliyonayo itajadiliwa vipi wakati wabunge wa chama chake wanaamini anastahili madaraka hayo? Ikumbukwe kuwa hata ukirudishwa haina maana hoja za CDM zitaingizwa zaidi ni kuwa zitajadiliwa na wabunge wa CCM kwa mara nyingine watapitisha mabadiliko yale yanayokifaidisha chama chao.

Lolote kati ya a,b, na c likitokea tutarudi kwenye square one!
Mwanakijiji,

Kama Rais anajuwa kabisa kuwa kwa hakika hatakubaliana na maoni ya CDM,then ni kwanini amekubali kukutana nao?

Ok,umezungumzia matokeo ya kama akichukuwa option b kwa upande wa CDM,lakini tumesahau kuwa na yeye ana plan yake na pia anategemea matokeo flani hata endapo atachukua option b.

Je mategemeo yake ni tofauti na hayo CDM wanayotegemea endapo "ataweka pamba masikioni"?

Je madhumuni yake ni yapi haswa kukubali kukutana na CDM huku akijuwa kuwa hatapokea ushauri wao?

Binafsi naamini mwishowe anaweza akawaambia ushauri wenu ni mzuri sana naomba muupeleke kwenye tume niliyoiunda.

Sasa sijui hiyo ndo square one ama vipi.

Naamini CDM watakachoenda kuongea nae ni kuhusu mfumo mzima na utaratibu wa kupata katiba mpya ambapo ni wazi Rais amejirundikia madaraka yote ya kwenye process ya kupata katiba mpya.

Je CDM wataenda kumwambia kuwa tumekuja hapa kusema kuwa una madaraka makubwa sana kwenye hii process na kwa hiyo jipunguzie?

Akikubaliana na maoni ya CDM,basi siasa za Tanzania zitabadilika kabisa,ni maoni yangu hapo.
 
MMJ, nakubaliana na wewe. Na kama ilivyokuwa kwa hotuba ya mbayumbayu, hii hotuba ya juzi kuhusu katiba mpya itamtafuna Kikwete. It is was a big mistake kujitokeza kabla hajamsoma adui yako, ukamjua ni nani na amejidhatiti vipi. Nchi nyingine huwa wanafanya a quick survey kujua mood ya watu iko vipi kabla hujaongea jambo zito la kitaifa. CCM wana-ugonjwa wa kutoa majibu kwa maswali ambayo hawajulizwa! Wamejiaminisha wanajua nini watu wanataka!

Wale waliokuwa wanauliza CHADEMA wamepata nini kwa kutoka nje ya bunge waangalie kwa makini siasa zinachezwaje.

1. Kwanza watanzania wengi zaidi wanafuatilia kila move ya CHADEMA, Rais, na matakamko ya viongozi wengine kuhusu huu muswada. (CCM hawafaidi hata kidogo kwa watanzania kuelewa mambo, they are better off kuwa na wananchi mbumbumbu). Kutoka nje kwa CHADEMA ni sawa na kupiga filimbi, wananchi wameamka - balaa kwa CCM!

2. Rais amewekwa kwenye spot-light. (very tricky position to be in) ama ale matapishi yake na kuwatosa wabunge wa CCM jambo ambalo litakizika kabisa hiki chama, au ajidai watanzania hawakusikia filimbi iliyopulizwa na CHADEMA hivyo aendelee ni mipango yake - matokeo yake hatuwezi kujua!

In all probability CHADEMA watapata more capital injection kisiasa kwenye kama 'hawatakubali yaishe'!
 
Ikulu wametoa tamko leo jioni kuwa RAis Kikwete amekubali kukutana na uongozi wa CDM na ameagiza tarehe ipangwe haraka ili waweze kukutana. I guess baada ya mambo yanayotokea Dodoma mkutano unaweza kufanyika kabla ya mwisho wa wiki hii au mwishoni mwa wiki. Kwamba, wataweza kumshawishi asiusaini sidhani kama hilo litatokea kwani kuna implication yake kwa Rais Kukataa kusaini mswada.

Naamini atausaini lakini bila mbwembwe ili uweze kurudishwa bungeni na kufanyiwa marekebisho. Akikataa kusaini atakuwa na nafasi moja nyingine ya kuukubali kabla hajajikuta anajiweka yeye mwenyewe na chama chake matatani.

Mwache tu ajifanye kichwa ngumu katika swala hili la kuipata katiba mpya. Matatizo yoyote yale yatakayotokea nchini kwa kukurupuka na kuipitisha katiba ambayo Watanzania wengi hatuikubali kutakuwa hakuna mwingine wa kulaumiwa ila ni yeye msanii. Ajifunze kusoma alama za nyakati ili kuona Watanzania wa 2011 siyo wale wa mwaka 47.
 
Wanabodi,

Pamoja na juhudi zote zinazofanywa kumshawishi Rais Jakaya Kikwete asiutie saini huo muswada kugeuka sheria, nawaomba niwahakikishie kwa asilimia 100% chini ya 100%, rais Jakaya Kikwete, atautia saini muswada huo kwa kishindo na mbwembwe zote zinastahiki, tena atausani mapema zaidi kuliko hata ilivyokuwa inatarajiwa!.

At this point, nawaomba tuu wanabodi muipokee kauli hii kama taarifa tuu, nawaombeni sana msiniulize nimejuaje, wala msiniulize sababu zozote kwa sababu sitazijibu, ila eleweni tuu kuwa muswada utasainiwa!.

Hii inamaanisha hata juhudi za Chadema, kutaka kumuona rais, zitagonga mwamba!. Kwenye hili la mchakato wa katiba, JK hatakutana na yeyote, hatasikia chochote, si la muadhini, wala mnadi swala, na wala hata bow down kwa shinikizo lolote, toka popote na kwa yeyote mpaka kwanza autie saini muswada ule!

Jee, lengo langu ni nini kuwapatia taarifa hii?.
Lengo la ni dogo tuu, kuwaanda wanabodi kuubali ukweli mchungu, hivyo wanakuwa tayari kisaikolojia kuipa tume hiyo ya maoni ushirikiano unaostahili.

Baadhi ya Watanzania wengi tumekuwa tukiishi kwenye false hopes na matokeo yake wasipopata kile walichokipata, the weak wana despair hivyo kuwa tayari kufanya lolote.

JK alipoingia madarakani, alikuja na kauli ya "Maisha Bora Kwa Kila Mtanzania", hivyo Watanzania wakawa na too much expectations kuhusu yeye. Maisha ya Mtanzania wa kawaida ndio haya tunayoishi sisi, walikuwa na matumaini makubwa ya maisha bora, wameanza kukata tamaa na kielelezo ni matokeo ya urais uchaguzi mkuu wa mwaka jana. Kitendo cha kuwajaza watu too much expectation wakati unaujua ukweli halisi, ni kuwapa false hopes!.

Enzi za Nyerere, baada ya Vita vya Kagera, alitangaza miezi 18 ya watu kujifunga mikanda, hivyo kuwaandaa kisaikolojia na tulijifunga mikanda kwa furaha.

Hivyo wale wote, wenye too much expectations kwa kudhani kuwa this time rais Kikwete atasikiliza kilio cha Watanzania kutaka kuutendea haki muswada huo, nawaombeni mjiandae kisaikolojia msije kupata frustrations na kuwa tayari kwa lolote!.

Namalizia kwa kutoa wito, "If you can't get what you want, please take what you get"!, yaani kama umekosa kile "kingi' ulichokitaka "Muswada Bora" ambao ungezaa "Sheria Bora", ambayo ingeunda "Tume Bora ya Kukusanya Maoni", ambayo ingetupatia "Katiba Bora", basi jamani, tujiandae kupokea hicho kidogo kilichopatikana ambacho ni "Bora Muswada" ambao utatupatia "Bora Sheria" itakayounda "Bora Tume ya Kukusanya Maoni" ambayo itatupatia "Bora Katiba" naomba tuipe tume hiyo ya kukusanya maoni, ushirikiano wa kutosha ili angalau tupate hiyo bora katiba, "Something is Better Than Nothing"!

Wasalaam

Pasco (wa jf).

UPDATE 1.
Rais Kikwete amepokea Barua ya Chadema na Amekubali Kukutana Nao!

Kama wewe hutaki asaini sisi wengine tunaka ausaini.

Hayo ya maisha bora unafikiri yanakuja kwa kukaa na kulala kungojea> inabidi ufanye kazi kwa bidii fursa zipo. Tele, asiyeziona furs zilizopo Tanzania basi mimi namshangaa sana, wanakuja wachina, wahindi, na wengine wa nchi za kiafrika kibao, tunawaona wanachangamkia fursa zilizokuwepo, leo nyinyi mnataka nini zaidi ya hicho?

Kama kuhusu maisha bora mnangoja mdondoshewe kutoka mbinguni basi mmekosea, hakuna nchi duniani utakuwa na maisha bora kama hufanyi kazi na unangoja handouts.
 
Pasco, nadhani ulijiamini mno hadi ukazidisha kipimo... Nadhani imani yako ilikuwa derived kutoka kwenye mjadala wa katiba ndani ya Bunge la JMT uliohitimwa juzi. CCM walikuwa wamejipanga iwe isiwe lazima wadhibiti mabadiliko ya katiba ili yasiwe yale yayotakiwa na CDM na baadhi ya wananchi wenye upeo. Kwahiyo umekuwa thabiti katika pendekezo lako, pengine ulipewa dokezo, au ulitumia tabia ya taarifa (trend of data) za zamani. Kwa kifupi model yako imekudanganya...

Ulisahau kuwa katika model unayoifahamu, sasa kuna parameters mpya zimeingia na kuleta mabadiliko ya behaviour katika siasa za Tanzania, hivyo si salama ku-predict kwa kutumia uzoefu wa data za zamani. Pale "Ikulu" (lugha yako siyo?) pana pressure na usiombe kukalia kile kiti. Unaweza kupigiwa simu na Obama, Cameroune, nk na kushinikizwa ku-change direction. Lakini kuna hii pressure ya mood ya nchi, wanaharakati wakiungwa mkono na adui zake CDM na opposition parties wengine, inatosha kumfanya mtu mwenye roho ngumu kusita na kulainika.

Hali ya nchi sasa hivi ni tete, siyo kwenye siasa tu, bali kila sehemu unayoweza kufikiri. UWT wanapoleta taarifa kwa Mkuu wa Nchi huwa anapewa fursa kuona na kutambua mambo ambayo wewe huwezi kuyaona. Kwa kifupi, Pasco umekosea, na umekuwa nabii wa uongo. Next time usiwe na haraka ya kuibuka na jambo jipya linalohusiana na future time...
 
... hata juhudi za Chadema, kutaka kumuona rais, zitagonga mwamba!. Kwenye hili la mchakato wa katiba, JK hatakutana na yeyote, hatasikia chochote, si la muadhini, wala mnadi swala, na wala hata bow down kwa shinikizo lolote, toka popote na kwa yeyote mpaka kwanza autie saini muswada ule!..

UPDATE 1.
Rais Kikwete amepokea Barua ya Chadema na Amekubali Kukutana Nao!
Last edited by Pasco; Today at 05:16.

Pasco Mayala, ulitakiwa kusimama katika kauli yako kuwa rais hatakutana na yoyote wala hatasikia chochote, kwa kuwa wewe ndio msemaji wa Ikulu. Sasa kuja tena humu na kuanza kuedit edit, huoni kwamba unajishushia heshima humu? Wewe uliapa kwamba una uhakika rais hatakutana na yeyote, nami nikadhani labda upo karibu na Ikulu au ni mmoja wa wanafamilia wa JK; nashangaa leo umekimbilia kuedit maneno yako. Ungekuwa muungwana kama ungekaa kimya na kukubali kuwa umepotosha umma, kukubali makosa ni uungwana. Lakini kwa kuwa unataka tuendelee kukuamini kuwa upo karibu na JK, umewahi asubuhi asubuhi kuja kuweka update ambazo ziko kinyume kabisa na kiapo chako. Jifunze maneno ya kuandika, siku nyingine usikurupuke kuanzisha thread as if wewe ndo wewe !!
 
Hii inaweza kuwa catch 22:

a. Kikwete akikataa kuusaini mswada huu kuwa sheria ataonekana amedharau maamuzi ya wabunge wake ambao kwa mbwembwe na vijembe waliupigia debe kuwa ni mswada mzuri.

b. Akiamua kuuweka sahihi (kitu ambacho ndio kinauwezekenao mkubwa) bila kuufanyia marekebisho atakuwa ameonekana kudharau na kukataa kabisa hoja za CDM na hivyo kuwafanya CDM waonekane mashujaa kwani ni wao waliotoa ofa ya kuomba kukutana naye na ni wao ambao hawakuchukua msimamo mkali bado na hivyo akiwakatalia CDM wataonekana wana hekima zaidi. Watasema "tumejitahidi na mmetuona lakini Rais kaweka pamba masikioni" kwa hiyo tunarudi mitaani! Well.. kila mtu kaona wamejitahidi.

c. Akiamua kuusaini na kuuridisha tena Bungeni bado tatizo litakuwa pale pale kwani hoja ya madaraka makubwa aliyonayo itajadiliwa vipi wakati wabunge wa chama chake wanaamini anastahili madaraka hayo? Ikumbukwe kuwa hata ukirudishwa haina maana hoja za CDM zitaingizwa zaidi ni kuwa zitajadiliwa na wabunge wa CCM kwa mara nyingine watapitisha mabadiliko yale yanayokifaidisha chama chao.

Lolote kati ya a,b, na c likitokea tutarudi kwenye square one!

Yaani hii kama uchaguzi wa Igunga, CDM wins whateva the outcome!!!!!!!!! Hahahahahahaha!!!! hizi ni zali za kisiasa amabazo CDM wakiamua wanweza kuzitumia for the final push.
 
Ni lazima tukubali ukweli mchungu kuwa wanachama na wapenzi wengi wa cdm ni wachanga katika siasa vivyo hivyo kwa viongozi wetu. Mara zote mtu huvuna anachopanda. CDM tuliwekeza nguvu nyingi sana katika suala la umeya wa Arusha wakati wenezetu CCM walilitumia suala hilo kutudistract ili tusiwe makini katika muswada huu. Ndio maana hawakusita kutumia vyombo vya dola. Aidha kila mara baadhi yetu tulipotahadharisha kuhus nguvu nyingi tunyowekeza Arusha pekee tulipokea matusi ya nguoni.

Mavuno ni pale wengi tuliposhindwa kufahamu nini maana ya muswada kusomwa mara ya kwanza na pili bungeni hivyo nguvu ya umma kushindwa kupatikana. Laiti kama CDM ingekuwa na priotisation na kuwekeza katika elimu ya uraia katika kipindi cha kuelekea kusomwa muswada huo na kufanya mikutano kama ile ya operesheni sangara kuelimisha umma utaratibu unaotakiwa kufuatwa na serikali na bunge katika kuupitisha muswada huo; nina hakika leo tungekuwa na muswada uliosomwa kwa mara ya kwanza na wananchi tungekuwa katika kutoa maoni yetu kwa lengo la kuuboresha muswada huo.

Waingereza wana msema kuwa "A war is a series of battles" "Vita ni mfululizo wa mapigano ya hap na pale". Hawezekani kuwa kila siku CDM ishinde mapambano yake basi pasingekuwepo wapinzani. Hivyo namuunga mkono Pasco kuwa badala ya kuwekeza nguvu nyingi katika kukutana na JK, ambao kwangu naona pia ni mtego mwingine kw CDM tuwekeza katika kutoa elim u kwa umma kupitia mikutano na sio maandamano kuhusu masuala yenye maslahi kwa taifa k.m kuundwa kwa serikali ya Tanzanganyika na ile ya Zanibar na ya M<uungano, kupunguzwa kwa madaraka ya Rais, Kuundwa kwa Tume huru ya uchaguzi, Mawaziri wasitokane na wabunge, vyeo vya RC na DC vifutwe n.k. Ni kutoakana na wananchi kupatiwa elimu ya kutosha kutakakowezesha wananchi kutoa maoni yao katika muelekeo huo, kupiga kura kukataa mambo hayo endapo Tume ya kukusanya maoni ya CCM na bunge la kutunga katiba la CCM watajaribu kutupitishia katiba mbovu.

Tukumbuke namna CCM ilivyokuwa ikiwachezea CUF katka kujenga muafaka wao. Nina hakika CCM na JK watafanya kila jitihada kuviendeleza vikao vya kamati ya CDM na JK viwe vya muda mrefu huku Serikali ikichanga mbuga kuandika katiba wanayotaka. Pia kutokana na CDM kusubiri jibu la JK watakuwa wameshajifunga hivyo kushindwa kuchukua hatua zingine zozote.
 
Msingi wa hoja yako ni hiyo ibara ya katiba uliyoinukuu; nami nakuuliza, ina maana haijawahi kutokea rais akaacha kusaini muswada katika historia ya nchi hii bila kulivunja bunge?

Umekurupuka, japo kwa hoja inayoonekana kama nzito!
 
Pasco, nadhani ulijiamini mno hadi ukazidisha kipimo... Nadhani imani yako ilikuwa derived kutoka kwenye mjadala wa katiba ndani ya Bunge la JMT uliohitimwa juzi. CCM walikuwa wamejipanga iwe isiwe lazima wadhibiti mabadiliko ya katiba ili yasiwe yale yayotakiwa na CDM na baadhi ya wananchi wenye upeo. Kwahiyo umekuwa thabiti katika pendekezo lako, pengine ulipewa dokezo, au ulitumia tabia ya taarifa (trend of data) za zamani. Kwa kifupi model yako imekudanganya...

Ulisahau kuwa katika model unayoifahamu, sasa kuna parameters mpya zimeingia na kuleta mabadiliko ya behaviour katika siasa za Tanzania, hivyo si salama ku-predict kwa kutumia uzoefu wa data za zamani. Pale "Ikulu" (lugha yako siyo?) pana pressure na usiombe kukalia kile kiti. Unaweza kupigiwa simu na Obama, Cameroune, nk na kushinikizwa ku-change direction. Lakini kuna hii pressure ya mood ya nchi, wanaharakati wakiungwa mkono na adui zake CDM na opposition parties wengine, inatosha kumfanya mtu mwenye roho ngumu kusita na kulainika.

Hali ya nchi sasa hivi ni tete, siyo kwenye siasa tu, bali kila sehemu unayoweza kufikiri. UWT wanapoleta taarifa kwa Mkuu wa Nchi huwa anapewa fursa kuona na kutambua mambo ambayo wewe huwezi kuyaona. Kwa kifupi, Pasco umekosea, na umekuwa nabii wa uongo. Next time usiwe na haraka ya kuibuka na jambo jipya linalohusiana na future time...

Kwa utabiri wangu hakuna chochote kitakacopatikana katika mkutano wa JK na CDM kwa sababu zifuatazo:- Tokea awali Serikali ilionyesha sheria hii kuanza kutumika tar 01 Desemba 2011, Hii ilikuwa ni kabla ya muswada kuwasilishwa bungeni na ndivyo muswada ulivyoandikwa na kuwasilishwa bungeni.

Ni hadi pale chama cha majaji wastaafu kilipogundua na kutamka kuwa kitendo cha Serikali kuweka tarehe ya sheria kuanza kutumika ni sawa na kulidhalilisha bunge kwani kinaonyesha dhahiri kuwa serikali haitegemei mabadiliko ya aiana yoyote kana kwamba bunge ni sehemu ya kugonga muhuri tu; ndipo luga ikabadilishwa kuwa bunge linapendekeza sheria hiyo ianze kutumika tarehe hiyo.

Hali ya nchi si tete hata kidogo, kwa kuwa imethibitika dhahiri kuwa nguvu ya umma huptikana pale tu wananchi wanapokuwa wameshirikishwa na kuelewa tatizo lililopo kama ambavyo waliellimishwa kuhusu tatizo la ufisadi wakalielewa na waka wa tayari kutetea raslimali za umma kwa kutumia nguvu ya umma. Lakini katika hili la katiba CDM imeshindwa kufnya homework yake vizuri kama ilivyofanya katika tatizo la ufisadi. Hii inaweza kuthibitishwa na butwaa na sintofahamu waliyokuwa wananchi tena wengi wao wake wanaoitwa nguvu ya umma pale mabishano ya "Muswda kusomwa kwa mara ya kwanza au pili yalipoanza" Kama mtu ni mfuatiliaji kweli na si mshabika idadi kubwa ya watanzan ia hususan vija hawakuweza kutambua nani mkweli kati ya CDM au CCM. Na yote hii ilisababishwa na CDM kushindwa kufanya priotisation kipi kina umuhimu zaidi kati ya kutoa elimu ya mchakato wa katiba kabla haujawasiliswha bungeni na kutumia muda, nguvu na raslima nyingi kupambania umeya wa Arusha mjini. CCM walitega offside trick CDM tukajenga kibanda ARusha mjini na kusahau mchakato wa katiba; kuja kushtuka siku ya kuwasilishwa kwa muswada kaila mtu anapigwa butwaa nini maana ya kusomwa mara ya kwanza au ya pili.

Hivi sasa CDM imeipatia CCM fursa ingine ya kututengenezea offside trick ingine kupitia mkutano na JK. Nina haki CCM kwa uzoefu wake wa siasa watatuamia mikutano hiyo kuifunga CDM mdomo na ndio utakuwa mwisho wa mikiki ya CDM; kufikia 2015 tayari itakuwa ni CCM C

"Retreat is no Surrender" hata mwalimu Nyerer alisema |Kurudi nyuma sio kusalimu amri ni kijiimarisha" Turudi nyuma tujipange upya na tukubali nguvu ya umma hutokana na elimu ya umma kwanza, Hiv yo hakuna nguvu ya umma bila elimu ya umma. Tuingia katika mchakato wa katiba kwa kutoa kipaumbele katika kuelimisha umma, kwani huo ndio mwiko wa CCM.
 
Nadhani Nzitunga umenena vema,kiukweli hueanda strategy watakayotoka nayo ni ku-buy time ili 2015 itumike hii katiba chakavu iliyopo.lakini nadhani ni kwa gharama ya pesa yoyote watahakikisha wanapandikiza watu kuivuruga chadema,ili waimalize nguvu,na hili watanzania wapenda haki tunapaswa kuliona kwa macho mawili na kwa uangalifu,na kwa wale walioamua kutoka jumla,ni hakuna kurudi nyuma waanze kushika nafasi mabali mbali ili pale itakapoonekana baadhi ya viongozi ndani ya chadema wanaelemewa na vishawishi au na sumu hiyo ya kukidhoofisha chama basi waweze ku-take over.Pamoja tutashinda
 
Kwa utabiri wangu hakuna chochote kitakacopatikana katika mkutano wa JK na CDM kwa sababu zifuatazo:- Tokea awali Serikali ilionyesha sheria hii kuanza kutumika tar 01 Desemba 2011, Hii ilikuwa ni kabla ya muswada kuwasilishwa bungeni na ndivyo muswada ulivyoandikwa na kuwasilishwa bungeni.

Ni hadi pale chama cha majaji wastaafu kilipogundua na kutamka kuwa kitendo cha Serikali kuweka tarehe ya sheria kuanza kutumika ni sawa na kulidhalilisha bunge kwani kinaonyesha dhahiri kuwa serikali haitegemei mabadiliko ya aiana yoyote kana kwamba bunge ni sehemu ya kugonga muhuri tu; ndipo luga ikabadilishwa kuwa bunge linapendekeza sheria hiyo ianze kutumika tarehe hiyo.

Hali ya nchi si tete hata kidogo, kwa kuwa imethibitika dhahiri kuwa nguvu ya umma huptikana pale tu wananchi wanapokuwa wameshirikishwa na kuelewa tatizo lililopo kama ambavyo waliellimishwa kuhusu tatizo la ufisadi wakalielewa na waka wa tayari kutetea raslimali za umma kwa kutumia nguvu ya umma. Lakini katika hili la katiba CDM imeshindwa kufnya homework yake vizuri kama ilivyofanya katika tatizo la ufisadi. Hii inaweza kuthibitishwa na butwaa na sintofahamu waliyokuwa wananchi tena wengi wao wake wanaoitwa nguvu ya umma pale mabishano ya "Muswda kusomwa kwa mara ya kwanza au pili yalipoanza" Kama mtu ni mfuatiliaji kweli na si mshabika idadi kubwa ya watanzan ia hususan vija hawakuweza kutambua nani mkweli kati ya CDM au CCM. Na yote hii ilisababishwa na CDM kushindwa kufanya priotisation kipi kina umuhimu zaidi kati ya kutoa elimu ya mchakato wa katiba kabla haujawasiliswha bungeni na kutumia muda, nguvu na raslima nyingi kupambania umeya wa Arusha mjini. CCM walitega offside trick CDM tukajenga kibanda ARusha mjini na kusahau mchakato wa katiba; kuja kushtuka siku ya kuwasilishwa kwa muswada kaila mtu anapigwa butwaa nini maana ya kusomwa mara ya kwanza au ya pili.

Hivi sasa CDM imeipatia CCM fursa ingine ya kututengenezea offside trick ingine kupitia mkutano na JK. Nina haki CCM kwa uzoefu wake wa siasa watatuamia mikutano hiyo kuifunga CDM mdomo na ndio utakuwa mwisho wa mikiki ya CDM; kufikia 2015 tayari itakuwa ni CCM C

"Retreat is no Surrender" hata mwalimu Nyerer alisema |Kurudi nyuma sio kusalimu amri ni kijiimarisha" Turudi nyuma tujipange upya na tukubali nguvu ya umma hutokana na elimu ya umma kwanza, Hiv yo hakuna nguvu ya umma bila elimu ya umma. Tuingia katika mchakato wa katiba kwa kutoa kipaumbele katika kuelimisha umma, kwani huo ndio mwiko wa CCM.

Watanabe, umechagua jina la Profesor maarufu huko Japan, je alikufundisha nini? ... back to the track...
Prof Watanabe, wazo lako kuwa mkutano wa CCM & CDM hautazaa kitu, is a mere assumptions, naomba tungoje matokeo, na wahenga walisema the end justifies the means...

Kuhusu hali ya nchi kuwa au kutokuwa tete, inategemea na kile unachofahamu au usichokifahamu. Lakini mimi naamini kama nilivyosema...

Kuhusu strategy ya kushirikisha wananchi, nadhani wameshirikishwa, ila response yao inategemea kiwango cha ufahamu walio nao. Si rahisi kuwapa uelewa wa 100%, ila kuna kiwango cha chini (activation energy) kikifikiwa utaona reaction ikitokea, tena inaweza kuwa a spontaneous reaction...

Unasema CDM imeshindwa kufanya vizuri homework yake, huenda uko sahihi, lakini pia CCM inaweza kuwa haijafanya home zake mbili zaidi. Hii ni siasa, kila mtu ana strategies zake, na kama hana, hulazimika kubuni haraka kutegemeana na mpinzani wake anavyokuja. Hivyo si salama kutumia model ya zamani ku-predict reality ya kesho. Pia nimemwambia Pasco vivyo hivyo ....
 
Pasco, nadhani ulijiamini mno hadi ukazidisha kipimo... Nadhani imani yako ilikuwa derived kutoka kwenye mjadala wa katiba ndani ya Bunge la JMT uliohitimwa juzi. CCM walikuwa wamejipanga iwe isiwe lazima wadhibiti mabadiliko ya katiba ili yasiwe yale yayotakiwa na CDM na baadhi ya wananchi wenye upeo. Kwahiyo umekuwa thabiti katika pendekezo lako, pengine ulipewa dokezo, au ulitumia tabia ya taarifa (trend of data) za zamani. Kwa kifupi model yako imekudanganya...

Ulisahau kuwa katika model unayoifahamu, sasa kuna parameters mpya zimeingia na kuleta mabadiliko ya behaviour katika siasa za Tanzania, hivyo si salama ku-predict kwa kutumia uzoefu wa data za zamani. Pale "Ikulu" (lugha yako siyo?) pana pressure na usiombe kukalia kile kiti. Unaweza kupigiwa simu na Obama, Cameroune, nk na kushinikizwa ku-change direction. Lakini kuna hii pressure ya mood ya nchi, wanaharakati wakiungwa mkono na adui zake CDM na opposition parties wengine, inatosha kumfanya mtu mwenye roho ngumu kusita na kulainika.

Hali ya nchi sasa hivi ni tete, siyo kwenye siasa tu, bali kila sehemu unayoweza kufikiri. UWT wanapoleta taarifa kwa Mkuu wa Nchi huwa anapewa fursa kuona na kutambua mambo ambayo wewe huwezi kuyaona. Kwa kifupi, Pasco umekosea, na umekuwa nabii wa uongo. Next time usiwe na haraka ya kuibuka na jambo jipya linalohusiana na future time...

Na ni huyuhuyu Pasco juzi alimpuuza mkjj pale aliposema hata chadema wangeamua kuweka pingamizi kwa kutumia kifungu cha 86 cha kanuni za bunge,wasingeweza kwakuwa mwisho wa siku spika angehoji na ni dhahiri hoja isingepita.Pasco alimlaumu mwkjj kuwa anabase kwenye predictions zaidi.Chakushangaza mwandishi huyu wa bandiko hili amepredict vyakutosha tu kuwa "hata raisi aki....cdm hawato...."!Vinginevyo braza Pasco nawewe unachezea mulemule ulipokuwa hutaki mkjj achezee....!
 
Kama wewe hutaki asaini sisi wengine tunaka ausaini.

Hayo ya maisha bora unafikiri yanakuja kwa kukaa na kulala kungojea> inabidi ufanye kazi kwa bidii fursa zipo. Tele, asiyeziona furs zilizopo Tanzania basi mimi namshangaa sana, wanakuja wachina, wahindi, na wengine wa nchi za kiafrika kibao, tunawaona wanachangamkia fursa zilizokuwepo, leo nyinyi mnataka nini zaidi ya hicho?

Kama kuhusu maisha bora mnangoja mdondoshewe kutoka mbinguni basi mmekosea, hakuna nchi duniani utakuwa na maisha bora kama hufanyi kazi na unangoja handouts
.


Yaani umeongea kiini cha matatizo ya wa Tanzania wengi. Watz wengi wanategemea kuwa serikali ina uwezo wa kuwaletea utajiri nyumbani. Ndiyo hawa hawa wanaolalamika migodi ifungwe badala ya kuenda huko kwenye migodi na kutafuta kazi. Ndiyo hawa hawa wanaopinga mapori kupewa wawekezaji ili waanzishe mashamba ya kufa mtu, badala ya kuenda kuwauzia mbolea.


 
Kama Bunge la muungano limeridhiya na limeupitisha, kwanini yeye asisaini?


Na kama utaratibu ni by default, si bora tufute hata huo utaratibu wa raisi kupelekewa huo muswada, bunge likipitisha na kuridhia basi spika anadondoka mchezo umeisha au siyo? Kuna haja gani ya kuupeleka kwa raisi wakati wabunge wameridhia na kuupitisha ikiwa ni lazima atasaini tu?. Nakupa hint tu kidogo fuatilia nini kilitokea kuhusu ule muswada wa sheria mpya za uchaguzi 2010.
 
Hii ni sehemu ya Hotuba ya JK, ukiisoma kwa makini utaona ni ndoto za alinacha kuamini kuwa atabadili uamuzi alioukwishaufanya yeye na chama chake lakini kwa kuwa Watanzania ni watu wa kuishi kwa matumaini tuendelee tu kusubiria muujiza:

Ni kutokana na hoja hizo Spika akaamua Muswada uendelee kujadiliwa na Bunge na leo Bunge limeupitisha Muswada huo. Baadae Muswada utaletwa kwangu kwa ajili ya kutiwa saini uwe Sheria. Baada ya hapo itabakia kazi yangu na Rais wa Zanzibar kuunda hiyo Tume ili mapema mwakani kazi ya kukusanya maoni ya wananchi ianze. Lengo letu ni kuwa ifikapo mwaka 2014 zoezi zima liwe limekamilika ili mwaka 2015 tufanye uchaguzi tukiwa na Katiba mpya. Itapendeza tukisherehekea miaka 50 ya Muungano na Katiba mpya. Ni matumaini yangu kwamba wananchi wote watashiriki kwa ukamilifu kutoa maoni yao kwa Tume hiyo.

....

Ndugu Wananchi;
Kwa upande wa mchakato wa kupata Katiba mpya nawasihi Watanzania tujiandae kwa maoni ya kutoa kwenye Tume ya Katiba mara itakapoanza kazi. Kwa wale ambao hawatapata walichokitaka nawaomba warudi kundini, sote tuungane kwa hatua inayofuata. Najua wanayo maoni mengi mazuri wayatayarishe na kuyawasilisha kwa Tume itakayoundwa. Njia ya maandamano na vurugu si ya busara kufuata. Haijengi bali inabomoa, haina faida bali hasara nyingi, haina faraja bali machungu kwa pande zote. Busara ituongoze sote kuchagua njia inayojenga, yenye faida, furaha na faraja kwa wote. Tutofautiane bila kupigana. Serikali itaendelea kutekeleza wajibu wake wa kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa nchi ya amani na utulivu.

Mwisho
Ndugu Wananchi,
Naomba nimalizie kwa kuwashukuru wananchi kwa kuwa na subira kwa kipindi chote hiki toka tutangaze nia yetu ya kuanza mchakato wa kupata Katiba mpya. Kwa mara nyingine tena nawaomba mjiandae kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kupata Katiba mpya mara utakapoanza ili tuendelee kuijenga na kuiendeleza nchi yetu na vile vile tuendelee kuithamini na kuitunza amani ya nchi yetu.

BUNGE NA DOLA YA CHAMA TAWALA LIMEUNGANA KATIKA HILI!
 
Kilichobaki ni "kurudi kundini" na kusubiria mabadiliko ya 15 ya Katiba ya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977 kama yalivyofanywa 2014
 
Back
Top Bottom