Katiba: Rais Kikwete kuusaini Muswada wa Tume ya Kusanya Maoni ya Katiba kwa Kishindo!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,467
113,567
Wanabodi,

Pamoja na juhudi zote zinazofanywa kumshawishi Rais Jakaya Kikwete asiutie saini huo muswada kugeuka sheria, nawaomba niwahakikishie kwa asilimia 100% chini ya 100%, rais Jakaya Kikwete, atautia saini muswada huo kwa kishindo na mbwembwe zote zinastahiki, tena atausani mapema zaidi kuliko hata ilivyokuwa inatarajiwa!.

At this point, nawaomba tuu wanabodi muipokee kauli hii kama taarifa tuu, nawaombeni sana msiniulize nimejuaje, wala msiniulize sababu zozote kwa sababu sitazijibu, ila eleweni tuu kuwa muswada utasainiwa!.(Nyongeza A: Rais atatakiwa kuukubali Muswada huo kabla ya kumalizika muda wa siku ishirini na moja tangu Muswada huo ulipowasilishwa kwake la sivyo basi itabidi alivunje Bunge.) Ibara ya 97 ya Katiba ya JMT ya 1977!.

Hii inamaanisha hata juhudi za Chadema, kutaka kumuona rais, zitagonga mwamba!. Kwenye hili la mchakato wa katiba, JK hatakutana na yeyote, hatasikia chochote, si la muadhini, wala mnadi swala, na wala hata bow down kwa shinikizo lolote, toka popote na kwa yeyote mpaka kwanza autie saini muswada ule!

Jee, lengo langu ni nini kuwapatia taarifa hii?.
Lengo la ni dogo tuu, kuwaanda wanabodi kuubali ukweli mchungu, hivyo wanakuwa tayari kisaikolojia kuipa tume hiyo ya maoni ushirikiano unaostahili.

Baadhi ya Watanzania wengi tumekuwa tukiishi kwenye false hopes na matokeo yake wasipopata kile walichokipata, the weak wana despair hivyo kuwa tayari kufanya lolote.

JK alipoingia madarakani, alikuja na kauli ya "Maisha Bora Kwa Kila Mtanzania", hivyo Watanzania wakawa na too much expectations kuhusu yeye. Maisha ya Mtanzania wa kawaida ndio haya tunayoishi sisi, walikuwa na matumaini makubwa ya maisha bora, wameanza kukata tamaa na kielelezo ni matokeo ya urais uchaguzi mkuu wa mwaka jana. Kitendo cha kuwajaza watu too much expectation wakati unaujua ukweli halisi, ni kuwapa false hopes!.

Enzi za Nyerere, baada ya Vita vya Kagera, alitangaza miezi 18 ya watu kujifunga mikanda, hivyo kuwaandaa kisaikolojia na tulijifunga mikanda kwa furaha.

Hivyo wale wote, wenye too much expectations kwa kudhani kuwa this time rais Kikwete atasikiliza kilio cha Watanzania kutaka kuutendea haki muswada huo, nawaombeni mjiandae kisaikolojia msije kupata frustrations na kuwa tayari kwa lolote!.

Namalizia kwa kutoa wito, "If you can't get what you want, please take what you get"!, yaani kama umekosa kile "kingi' ulichokitaka "Muswada Bora" ambao ungezaa "Sheria Bora", ambayo ingeunda "Tume Bora ya Kukusanya Maoni", ambayo ingetupatia "Katiba Bora", basi jamani, tujiandae kupokea hicho kidogo kilichopatikana ambacho ni "Bora Muswada" ambao utatupatia "Bora Sheria" itakayounda "Bora Tume ya Kukusanya Maoni" ambayo itatupatia "Bora Katiba" naomba tuipe tume hiyo ya kukusanya maoni, ushirikiano wa kutosha ili angalau tupate hiyo bora katiba, "Something is Better Than Nothing"!

Wasalaam

Pasco (wa jf).

UPDATE 1.
Rais Kikwete amepokea Barua ya Chadema na Amekubali Kukutana Nao!

UPDATE 2.
Hii ni sehemu ya Hotuba ya JK, ukiisoma kwa makini utaona ni ndoto za alinacha kuamini kuwa atabadili uamuzi alioukwishaufanya yeye na chama chake lakini kwa kuwa Watanzania ni watu wa kuishi kwa matumaini tuendelee tu kusubiria muujiza:

Ni kutokana na hoja hizo Spika akaamua Muswada uendelee kujadiliwa na Bunge na leo Bunge limeupitisha Muswada huo. Baadae Muswada utaletwa kwangu kwa ajili ya kutiwa saini uwe Sheria. Baada ya hapo itabakia kazi yangu na Rais wa Zanzibar kuunda hiyo Tume ili mapema mwakani kazi ya kukusanya maoni ya wananchi ianze. Lengo letu ni kuwa ifikapo mwaka 2014 zoezi zima liwe limekamilika ili mwaka 2015 tufanye uchaguzi tukiwa na Katiba mpya. Itapendeza tukisherehekea miaka 50 ya Muungano na Katiba mpya. Ni matumaini yangu kwamba wananchi wote watashiriki kwa ukamilifu kutoa maoni yao kwa Tume hiyo.

....

Ndugu Wananchi;
Kwa upande wa mchakato wa kupata Katiba mpya nawasihi Watanzania tujiandae kwa maoni ya kutoa kwenye Tume ya Katiba mara itakapoanza kazi. Kwa wale ambao hawatapata walichokitaka nawaomba warudi kundini, sote tuungane kwa hatua inayofuata. Najua wanayo maoni mengi mazuri wayatayarishe na kuyawasilisha kwa Tume itakayoundwa. Njia ya maandamano na vurugu si ya busara kufuata. Haijengi bali inabomoa, haina faida bali hasara nyingi, haina faraja bali machungu kwa pande zote. Busara ituongoze sote kuchagua njia inayojenga, yenye faida, furaha na faraja kwa wote. Tutofautiane bila kupigana. Serikali itaendelea kutekeleza wajibu wake wa kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa nchi ya amani na utulivu.

Mwisho
Ndugu Wananchi,
Naomba nimalizie kwa kuwashukuru wananchi kwa kuwa na subira kwa kipindi chote hiki toka tutangaze nia yetu ya kuanza mchakato wa kupata Katiba mpya. Kwa mara nyingine tena nawaomba mjiandae kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kupata Katiba mpya mara utakapoanza ili tuendelee kuijenga na kuiendeleza nchi yetu na vile vile tuendelee kuithamini na kuitunza amani ya nchi yetu.

BUNGE NA DOLA YA CHAMA TAWALA LIMEUNGANA KATIKA HILI!
 
Wanabodi,

Pamoja na juhudi zote zinazofanywa kumshawishi Rais Jakaya Kikwete asiutie saini huo muswada kugeuka sheria, nawaomba niwahakikishie kwa asilimia 100% chini ya 100%, rais Jakaya Kikwete, atautia saini muswada huo kwa kishindo na mbwembwe zote zinastahiki, tena atausani mapema zaidi kuliko hata ilivyokuwa inatarajiwa!.

At this point, nawaomba tuu wanabodi muipokee kauli hii kama taarifa tuu, nawaombeni sana msiniulize nimejuaje, wala msiniulize sababu zozote kwa sababu sitazijibu, ila eleweni tuu kuwa muswada utasainiwa!.

Hii inamaanisha hata juhudi za Chadema, kutaka kumuona rais, zitagonga mwamba!. Kwenye hili la mchakato wa katiba, JK hatakutana na yeyote, hatasikia chochote, si la muadhini, wala mnadi swala, na wala hata bow down kwa shinikizo lolote, toka popote na kwa yeyote mpaka kwanza autie saini muswada ule!

Jee, lengo langu ni nini kuwapatia taarifa hii?.
Lengo la ni dogo tuu, kuwaanda wanabodi kuubali ukweli mchungu, hivyo wanakuwa tayari kisaikolojia kuipa tume hiyo ya maoni ushirikiano unaostahili.

Baadhi ya Watanzania wengi tumekuwa tukiishi kwenye false hopes na matokeo yake wasipopata kile walichokipata, the weak wana despair hivyo kuwa tayari kufanya lolote.

JK alipoingia madarakani, alikuja na kauli ya "Maisha Bora Kwa Kila Mtanzania", hivyo Watanzania wakawa na too much expectations kuhusu yeye. Maisha ya Mtanzania wa kawaida ndio haya tunayoishi sisi, walikuwa na matumaini makubwa ya maisha bora, wameanza kukata tamaa na kielelezo ni matokeo ya urais uchaguzi mkuu wa mwaka jana. Kitendo cha kuwajaza watu too much expectation wakati unaujua ukweli halisi, ni kuwapa false hopes!.

Enzi za Nyerere, baada ya Vita vya Kagera, alitangaza miezi 18 ya watu kujifunga mikanda, hivyo kuwaandaa kisaikolojia na tulijifunga mikanda kwa furaha.

Hivyo wale wote, wenye too much expectations kwa kudhani kuwa this time rais Kikwete atasikiliza kilio cha Watanzania kutaka kuutendea haki muswada huo, nawaombeni mjiandae kisaikolojia msije kupata frustrations na kuwa tayari kwa lolote!.

Namalizia kwa kutoa wito, "If you can't get what you want, please take what you get"!, yaani kama umekosa kile "kingi' ulichokitaka "Muswada Bora" ambao ungezaa "Sheria Bora", ambayo ingeunda "Tume Bora ya Kukusanya Maoni", ambayo ingetupatia "Katiba Bora", basi jamani, tujiandae kupokea hicho kidogo kilichopatikana ambacho ni "Bora Muswada" ambao utatupatia "Bora Sheria" itakayounda "Bora Tume ya Kukusanya Maoni" ambayo itatupatia "Bora Katiba" naomba tuipe tume hiyo ya kukusanya maoni, ushirikiano wa kutosha ili angalau tupate hiyo bora katiba, "Something is Better Than Nothing"!

Wasalaam

Pasco (wa jf).

UPDATE 1.
Rais Kikwete amepokea Barua ya Chadema na Amekubali Kukutana Nao!
Mkuu tumekusikia na hakika hiyo TUME ya rais itapokea MAONI ya wananchi... Mnnnnnh! - maoni! na sio PINGAMIZI hivyo kinachofuatia ni yale yale muendelezo wa mama Spika wa bunge - Bora muswada ukipata sheria utakuwa bora sheria ambayo itatuletea bora katiba..
- Shukran
 
Mkuu Pasco
Bandiko lako lina kila dalili ya kubali yaishe! huo pia ni utaratibu mzuri katika maisha ingawa si mara zote utaratibu huu una maana hasa unapoongelea suala kubwa la kitaifa kama Katiba. Wakati huu ni muhimu rais kukumbushwa kuwa nchi yetu inafuka moshi na kila hatua inayochukuliwa na serikali inatakiwa kuwa na tahadhari kubwa kama bado wanadhani kuwa nchi yetu ni ya amani. Bongo haina tofauti na nchi zinginw nyingi duniani zinazohangaikia stability ya nchi zao leo due to matatizo ya kiuchumi yanayosababisha maisha magumu kupindukia kwa kundi kubwa la watu. Kikwete ameshikilia majani makavu na kuna watu wameshikilia kiberiti hivyo kama majani haya hayatakuwa handled kwa umani mkubwa then wenye viberiti watia moto kisha nchi itakuwa ya ajabu sana kuliko tunavyodhani. Believe me there thousands of young people who have nothing to lose and therefore ready for anything.
 
Hii inamaanisha hata juhudi za Chadema, kutaka kumuona rais, zitagonga mwamba!. Kwenye hili la mchakato wa katiba, JK hatakutana na yeyote, hatasikia chochote, si la muadhini, wala mnadi swala, na wala hata bow down kwa shinikizo lolote, toka popote na kwa yeyote mpaka kwanza autie saini muswada ule!
Hii thread yako imepitwa na wakati kwa taarifa yako tayari amekubali kukutana na kamati ndogo ya Chadema.
 
Mkuu tumekusikia na hakika hiyo TUME ya rais itapokea MAONI ya wananchi... Mnnnnnh! - maoni! na sio PINGAMIZI hivyo kinachofuatia ni yale yale muendelezo wa mama Spika wa bunge - Bora muswada ukipata sheria utakuwa bora sheria ambayo itatuletea bora katiba..
- Shukran

Hebu nifahamishe matatizo makubwa mawili ya muswada huo ukiwa kama ulivyo???
 
Pasco said:
If you can't get what you want, please take what you get.

Pasco,

..huu ushauri ungeuelekeza kwa Raisi na CCM pia.

..itafika mahali they may not get what they want.

..hopefully at that time watatusikiliza wananchi na kuweka maslahi ya taifa mbele.
 
Shida ni kwamba JK anataka umaarufu na mbwembwe za kusaini mbele ya makamera, bila kutumia hata muda kidogo kutafakari impact ya haraka-haraka hizo kwenye muswada ambao utagharimu katiba ya life-time ya watanzania.
Nashindwa kuelewa rais ambaye niliamini ni mtu rational anashawishiwa na nani kuwa na haraka hizo, badala ya kutulia...
 
sijui lini utaacha kutumika......unatumika sana pasco...hata ule mswaada ya sheria ya uchaguzi aliusaini kwa madaha hivyo hivyo ...lakini ulirudi bungeni.....
 
At this point, nawaomba tuu wanabodi muipokee kauli hii kama taarifa tuu, nawaombeni sana msiniulize nimejuaje, wala msiniulize sababu zozote kwa sababu sitazijibu, ila eleweni tuu kuwa muswada utasainiwa!.
!
Source???
 
Topical said:
Hebu nifahamishe matatizo makubwa mawili ya muswada huo ukiwa kama ulivyo???

Topical,

..mswada unaitambua ZNZ kama mbia sawa wa serikali ya Muungano.

..ZNZ ni mbia sawa na TGK siyo serikali ya muungano.

..mswada pia hautoi nafasi kwa wananchi kupiga kura ya maoni kama wanataka muungano ama la.

..muswada unaruhusu kujadiliwa kwa muungano, bila kuwepo kwa Tanganyika ambayo ni mbia wa muungano huo.

..vilevile mswada umempa madaraka Raisi kuteua wajumbe wa Tume ya kukusanya maoni ya Katiba, na zaidi Raisi ndiye anaye-set hadidu rejea za tume hiyo.

..ingekuwa vema angalau bunge la Jamhuri liwe na uwezo wa kuwadhibitisha wajumbe wa tume ya katiba na zaidi kuzipitia na kuziboresha hadidu za rejea za tume hiyo.

..mwisho mswada una VITISHO vya ADHABU YA KIFUNGO kuhusu yeyote atakayeupinga.
 
Ikulu wametoa tamko leo jioni kuwa RAis Kikwete amekubali kukutana na uongozi wa CDM na ameagiza tarehe ipangwe haraka ili waweze kukutana. I guess baada ya mambo yanayotokea Dodoma mkutano unaweza kufanyika kabla ya mwisho wa wiki hii au mwishoni mwa wiki. Kwamba, wataweza kumshawishi asiusaini sidhani kama hilo litatokea kwani kuna implication yake kwa Rais Kukataa kusaini mswada.

Naamini atausaini lakini bila mbwembwe ili uweze kurudishwa bungeni na kufanyiwa marekebisho. Akikataa kusaini atakuwa na nafasi moja nyingine ya kuukubali kabla hajajikuta anajiweka yeye mwenyewe na chama chake matatani.
 
hivi wewe pasco ni wa kutuandaa sisi?? wewe huyu unatuandaa kwa lipi ambalo tulikuwa hatulijui tangu mswaada umeenda bungeni ,jk amehutubia wazee wa ccm dsm....nini hatukijui hadi uje eti unatuandaa kutoa maoni....acha kujikosha mtoto wa kiume...yeye acha asaini mbele ya kamera sisi hatuna shida ila ajue tutakutana makutano junction....yeye na katiba yake na sisi na katiba yetu....
 
Topical,

..mswada unaitambua ZNZ kama mbia sawa wa serikali ya Muungano.

..ZNZ ni mbia sawa na TGK siyo serikali ya muungano.

..mswada pia hautoi nafasi kwa wananchi kupiga kura ya maoni kama wanataka muungano ama la.

..muswada unaruhusu kujadiliwa kwa muungano, bila kuwepo kwa Tanganyika ambayo ni mbia wa muungano huo.

..vilevile mswada umempa madaraka Raisi kuteua wajumbe wa Tume ya kukusanya maoni ya Katiba, na zaidi Raisi ndiye anaye-set hadidu rejea za tume hiyo.

..ingekuwa vema angalau bunge la Jamhuri liwe na uwezo wa kuwadhibitisha wajumbe wa tume ya katiba na zaidi kuzipitia na kuziboresha hadidu za rejea za tume hiyo.

..mwisho mswada una VITISHO vya ADHABU YA KIFUNGO kuhusu yeyote atakayeupinga.

a. Zanzibar kuwa mbia sawa na JMT tatizo lake nini?

b. Hilo la kutaka kupiga kura either tunataka muungano au la ?? (tuko pamoja)

c. Hilo la kuchaguliwa na tume kwa wajumbe sioni tatizo kwasababu ukisema iende bungeni kama kawaida ccm ni wengi na watapitishwa hata mtu kama Tambwe..

d. Hilo la kuweka hadidu za rejea, sioni tatizo kwasababu rais ni taasisi kwasababu hata ikienda bungeni ccm bado ni wengi..
 
Uchaguzi mkuu wa 2010 umabadilisha kabisa Tanzania. Things will never be the same na mshindi (wa siasa) ni yule tu atakayeweza kukubali ukweli na kuufanyia kazi. Kwenye huu muswada H.E Jakaya Mrisho Kikwete anatakiwa achague ama afanye maamuzi kama Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania au Mwenyekiti wa CCM. Kwa maneno mengine Kikwete anatakiwa achague ama amilikishe CCM huu muswada au aufanye uwe wa watanzania wote (wafuasi wa vyama vya siasa na wale wasio wafuasi wa chama chochote).
 
Ikulu wametoa tamko leo jioni kuwa RAis Kikwete amekubali kukutana na uongozi wa CDM na ameagiza tarehe ipangwe haraka ili waweze kukutana. I guess baada ya mambo yanayotokea Dodoma mkutano unaweza kufanyika kabla ya mwisho wa wiki hii au mwishoni mwa wiki. Kwamba, wataweza kumshawishi asiusaini sidhani kama hilo litatokea kwani kuna implication yake kwa Rais Kukataa kusaini mswada.

Naamini atausaini lakini bila mbwembwe ili uweze kurudishwa bungeni na kufanyiwa marekebisho. Akikataa kusaini atakuwa na nafasi moja nyingine ya kuukubali kabla hajajikuta anajiweka yeye mwenyewe na chama chake matatani.
Unajua nini, JK asipousaini huu muswada atakuwa amewapiga goli kubwa sana la kisigino wote wale wanaomdhihaki ndani ya chama na nje..hata kama hataweka mabadiliko makubwa. Yeye anaweza tu kuchukua sababu ndogo sana ya kutosaini kisha muswada ukarudi bungeni... tik...tak... siku zinakwenda na yeye hatakuwa na makosa wala wa kulaumiwa...
 
Kwa leo Pascho msukuma mwenzangu nimekunawa hata hivyo siwezi kushangaa maana yawezekana una element hizo,endelea na juhudi zako iko siku utapata unachokitafuta kwa kuonyesha dhahiri uko upande gani.Ila nashangaa unajifanya kuwaandaa watu kutoa maoni.kwa kuwa kuhesabu kunaanza na moja ndipo upate idadi ya unaotaka kuwaandaa,mimi umenikosa,wala sitaki kushawishiwa na yeyote mi siko tayari wala sitoenda kutoa maoni.Ila nimejifunza kitu kutoka kwako nimeshajua uko upande gani
 
mwanaume anapenda sifa huyu balaa...kwa hiyo kikwete kakutuma uje usema hapa kuwa atasaini?!!! nakushangaa sana kijana wewe.....hivi kama una mtoto wako mdogo(under 15)hivi unadhani kwa katiba hii ya ccm itakayoandaliwa huyo mwanao ataikuta tanzania yenye neema baada ya miaka 30?? hivi huwa unawaza kweli na kufikili sawa sawa? jaribu kushughulisha akili yako na mawazo yako yavuke masaa ya chakula cha usiku kijana!!! ......
 
Kwenye mkutano wake na wazee "wananchi" alisema kwa majigambo 'NITASAINI MUSWADA' nitashangaa kama atabadili mawazo at last minute. JK anahitaji msaada wa kifikra,kiroho na kiakili analipeleka taifa kwenye shimo lenye kina kirefu kutoka kwake labda Yesu atakaporudi mara ya tatu ooops mara ya pili
 
Back
Top Bottom