mujusi
JF-Expert Member
- Jan 22, 2010
- 237
- 58
Nimesoma kwenye Guardian ya leo (pg 3). Mbunge Nimrod anasema hakuna haja ya katiba mpya na kutaka kutengeneza mpya ni sawa na kutaka kupindua nchi. Anaendelea kusema " Rais, Wabunge na Viongozi wa Serikali wameapa Kuiheshimu na kuilinda Katiba na siyo kuibadili. Ninachouliza wana JF, kama wazo ndio liko hivi kweli hii Katiba ya sasa itaweza kuandikwa upya ukitilia maanani kwamba anaesema hivi ni Mbunge(miongoni wa watakaoamua kama kuna haja ya kuandika upya) na Mwanasheria maarufu hapa nchini?