Katiba mpya ni muhimu kwa maendeleo na mstakabali wa vizazi vya sasa na vijavyo

Ngongo

JF-Expert Member
Sep 20, 2008
18,926
31,169
Heri ya X Mass.

Tunamshukuru Mungu kwa siku kuu ya leo,na kwa namna ya kipekee kabisa nawapongeza waKristo wote Tanzania na Duniani.

Wakati bado tunaendelea kusheherekea siku hii muhimu naomba tuwarejeshe katika mjadala wa mchakato wa KATIBA MPYA.

Ni hakika KATIBA ya sasa ina mapungufu mengi na tena imepitwa na wakati.
Ukitazama STRUCTURE ya Katiba utaona imejikita katika KUMSIKILIZA,KUMTII,KUMWABUDU,KUMSIFU,KUMNYENYEKEA RAIS wa JMT.

Si vibaya RAIS wa JMT akatengenezewa utaratibu wa kiMungu Mungu tatizo kubwa ni kwamba RAIS wa JMT ni mwanadamu mwenye mapungufu mengi.Akitumia vibaya katiba watu wengi wataumia sana tena sana.Hakuna mahali pa kupinga maamuzi mabaya ya RAIS.Akiamu kutuingiza katika vita tutaingia,akiamua kukwapua fedha za wananchi nje ya utaratibu wa sheria atakwapua hakuna wa kumzuia,akiamua kuingiza jeshi mtaani kutandika wananchi asiowapenda hakuna wa kumkatalia.Viongozi wote wanaapishwa kumtii Raia na si katiba.

Hakuna tatizo iwapo Rais atakuwa malaika lakini kama ni hawa watawala mapenda madaraka hakika sioni Tanzania ikipiga hatua za maana.

KATIBA MPYA ni muhimu sasa kuliko wakati wowote Mwl alituachia katiba mbaya ni wajibu wetu wote kuhakikisha KATIBA MPYA itakayopunguza madaraka makubwa ya RAIS.Itakayo hakikisha uhuru wa Mahakama,Bunge na tume ya uchaguzi.

Ngongo kwasasa KIBANDA MAITI.
 
Naunga mkono hoja, bila Katiba mpya itakayoundwa itakayoendana na mfumo wa vyama vingi, hatutoboa Hadi mwisho wa Dunia!
 
Heri ya X Mass.

Tunamshukuru Mungu kwa siku kuu ya leo,na kwa namna ya kipekee kabisa nawapongeza waKristo wote Tanzania na Duniani.

Wakati bado tunaendelea kusheherekea siku hii muhimu naomba tuwarejeshe katika mjadala wa mchakato wa KATIBA MPYA.

Ni hakika KATIBA ya sasa ina mapungufu mengi na tena imepitwa na wakati.
Ukitazama STRUCTURE ya Katiba utaona imejikita katika KUMSIKILIZA,KUMTII,KUMWABUDU,KUMSIFU,KUMNYENYEKEA RAIS wa JMT.

Si vibaya RAIS wa JMT akatengenezewa utaratibu wa kiMungu Mungu tatizo kubwa ni kwamba RAIS wa JMT ni mwanadamu mwenye mapungufu mengi.Akitumia vibaya katiba watu wengi wataumia sana tena sana.Hakuna mahali pa kupinga maamuzi mabaya ya RAIS.Akiamu kutuingiza katika vita tutaingia,akiamua kukwapua fedha za wananchi nje ya utaratibu wa sheria atakwapua hakuna wa kumzuia,akiamua kuingiza jeshi mtaani kutandika wananchi asiowapenda hakuna wa kumkatalia.Viongozi wote wanaapishwa kumtii Raia na si katiba.

Hakuna tatizo iwapo Rais atakuwa malaika lakini kama ni hawa watawala mapenda madaraka hakika sioni Tanzania ikipiga hatua za maana.

KATIBA MPYA ni muhimu sasa kuliko wakati wowote Mwl alituachia katiba mbaya ni wajibu wetu wote kuhakikisha KATIBA MPYA itakayopunguza madaraka makubwa ya RAIS.Itakayo hakikisha uhuru wa Mahakama,Bunge na tume ya uchaguzi.

Ngongo kwasasa KIBANDA MAITI.
NI WENYE AKILI KUBWA NDIO WANALIJUA HILO LAKINI MAMBUMBUMBU hayajui umuhimu wa KATIBA MPYA
 
NI WENYE AKILI KUBWA NDIO WANALIJUA HILO LAKINI MAMBUMBUMBU hayajui umuhimu wa KATIBA MPYA

Ebu tuvute fikra kidogo Rais anamteua Mkuu wa Mkoa wa Dar au Tabora.Kwa vyovyote Mkuu wa Mkoa atakuwa anafikiria Rais anataka nini na si wananchi wa Mkoa huo wanataka nini !.
Ndio maana kila siku utamsikia Mkuu wa Mkoa X anamsifu Rais kama Mungu na kuwaacha wananchi wa Mkoa X wakiendelea kusota wasijue wapi pa kukimbilia.

Usishangae kila Mwanasiasa kila siku anamsifia Rais anaupiga mwingi,hili ni tatizo la kikatiba na si wanasiasa kama tunavyofikiri.Kafulila kila siku ana kazi ya kumsifia Rais pengine akipiga hesabu zake mbona Chalamila karejeshwa.
 
Katiba mbovu iliyopo ilikuwa ni fikra mbovu za Nyerere
Kwa hakika Mwl Nyerere alitukosea sana waTanzania,masuala yote tuliyopigania na kufanikiwa kumfukuza Mwingereza alijitwisha yeye na kutuacha sisi walalahoi bin taabani tukinyanyaswa na watawala.

Mamlaka aliyokuwa nayo Malkia Elizibeth alijitwika.
 
Heri ya X Mass.

Tunamshukuru Mungu kwa siku kuu ya leo,na kwa namna ya kipekee kabisa nawapongeza waKristo wote Tanzania na Duniani.

Wakati bado tunaendelea kusheherekea siku hii muhimu naomba tuwarejeshe katika mjadala wa mchakato wa KATIBA MPYA.

Ni hakika KATIBA ya sasa ina mapungufu mengi na tena imepitwa na wakati.
Ukitazama STRUCTURE ya Katiba utaona imejikita katika KUMSIKILIZA,KUMTII,KUMWABUDU,KUMSIFU,KUMNYENYEKEA RAIS wa JMT.

Si vibaya RAIS wa JMT akatengenezewa utaratibu wa kiMungu Mungu tatizo kubwa ni kwamba RAIS wa JMT ni mwanadamu mwenye mapungufu mengi.Akitumia vibaya katiba watu wengi wataumia sana tena sana.Hakuna mahali pa kupinga maamuzi mabaya ya RAIS.Akiamu kutuingiza katika vita tutaingia,akiamua kukwapua fedha za wananchi nje ya utaratibu wa sheria atakwapua hakuna wa kumzuia,akiamua kuingiza jeshi mtaani kutandika wananchi asiowapenda hakuna wa kumkatalia.Viongozi wote wanaapishwa kumtii Raia na si katiba.

Hakuna tatizo iwapo Rais atakuwa malaika lakini kama ni hawa watawala mapenda madaraka hakika sioni Tanzania ikipiga hatua za maana.

KATIBA MPYA ni muhimu sasa kuliko wakati wowote Mwl alituachia katiba mbaya ni wajibu wetu wote kuhakikisha KATIBA MPYA itakayopunguza madaraka makubwa ya RAIS.Itakayo hakikisha uhuru wa Mahakama,Bunge na tume ya uchaguzi.

Ngongo kwasasa KIBANDA MAITI.
Chadema wanataka katiba mpya, ila wanataka CCM wafanye kazi ya kutengeneza hiyo katiba.
Kama kweli Chadema wangekuwa na nia ya dhati ya katiba mpya, badi angalau wangekuwa wametengeneza 1st draft tuone katiba wanayoitaka inafananaje!
 
Katiba mpya haipaswi kupatikana katika jamii ya waoga itakua haina msaada wowote.
 
Mwaka 2023 uwe MWAKA wa KUIPIGANIA KATIBA MPYA ILIYO BORA..CDM yaleteni makundi mengine kama Viongozi wa DINI,NGOs,Vyama vya KITAALUMA,Wanafunzi wa Vyuo vikuu,Wanadiaspora,Vyama vya Wakulima,WAfugaji kwenye VUGUVUGU LA KUDAI KATIBA MPYA ILIYO BORA
 
Heri ya X Mass.

Tunamshukuru Mungu kwa siku kuu ya leo,na kwa namna ya kipekee kabisa nawapongeza waKristo wote Tanzania na Duniani.

Wakati bado tunaendelea kusheherekea siku hii muhimu naomba tuwarejeshe katika mjadala wa mchakato wa KATIBA MPYA.

Ni hakika KATIBA ya sasa ina mapungufu mengi na tena imepitwa na wakati.
Ukitazama STRUCTURE ya Katiba utaona imejikita katika KUMSIKILIZA,KUMTII,KUMWABUDU,KUMSIFU,KUMNYENYEKEA RAIS wa JMT.

Si vibaya RAIS wa JMT akatengenezewa utaratibu wa kiMungu Mungu tatizo kubwa ni kwamba RAIS wa JMT ni mwanadamu mwenye mapungufu mengi.Akitumia vibaya katiba watu wengi wataumia sana tena sana.Hakuna mahali pa kupinga maamuzi mabaya ya RAIS.Akiamu kutuingiza katika vita tutaingia,akiamua kukwapua fedha za wananchi nje ya utaratibu wa sheria atakwapua hakuna wa kumzuia,akiamua kuingiza jeshi mtaani kutandika wananchi asiowapenda hakuna wa kumkatalia.Viongozi wote wanaapishwa kumtii Raia na si katiba.

Hakuna tatizo iwapo Rais atakuwa malaika lakini kama ni hawa watawala mapenda madaraka hakika sioni Tanzania ikipiga hatua za maana.

KATIBA MPYA ni muhimu sasa kuliko wakati wowote Mwl alituachia katiba mbaya ni wajibu wetu wote kuhakikisha KATIBA MPYA itakayopunguza madaraka makubwa ya RAIS.Itakayo hakikisha uhuru wa Mahakama,Bunge na tume ya uchaguzi.

Ngongo kwasasa KIBANDA MAITI.

Kwanza tuambie katiba ya sasa inatunyima vitu gani Kwa Maisha ya mtanzania mmoja mmoja?

Tuanze na Maisha yako ww, katiba ya sasa inakunyima nn?
 
Mwaka 2023 uwe MWAKA wa KUIPIGANIA KATIBA MPYA ILIYO BORA..CDM yaleteni makundi mengine kama Viongozi wa DINI,NGOs,Vyama vya KITAALUMA,Wanafunzi wa Vyuo vikuu,Wanadiaspora,Vyama vya Wakulima,WAfugaji kwenye VUGUVUGU LA KUDAI KATIBA MPYA ILIYO BORA

Tueleze mapungufu ya katiba hii kwanza
 
Kwanza tuambie katiba ya sasa inatunyima vitu gani Kwa Maisha ya mtanzania mmoja mmoja?

Tuanze na Maisha yako ww, katiba ya sasa inakunyima nn?

Katiba ya sasa huwezi kuishitaki Serekali hata kama wamekukosea.Chukulia mfano umefanya biashara na DAWASCO wameshindwa kukulipa deni huwezi kwenda mahakamani na hata ukiwadhinda huwezi kukamata assets zao.

Kwa katiba hii ambayo Majaji ni wateule wa Rais shauri likipelekwa mahakamani ni vigumu kuishinda serekali.

Kwa katiba hii Tume ya uchaguzi wote ni wateule wa Rais,kura yako si chochote si lolote hasa inapokuwa inakwenda kinyume na matarajio ya Rais.Haki ya kura yangu kuhesabiwa hakuna kabisa.

Kwa katiba hii ardhi yote ni mali ya Rais,Ikiwa serekali au mawakala wa serekali (wawekezaji) watahitaji au watataka kuchukua ardhi yako hakuna mahali pa kwenda zaidi ya kuporwa ardhi yako kirahisi kwa mgongo wa maslahi ya umma.
 
Katiba ya sasa huwezi kuishitaki Serekali hata kama wamekukosea.Chukulia mfano umefanya biashara na DAWASCO wameshindwa kukulipa deni huwezi kwenda mahakamani na hata ukiwadhinda huwezi kukamata assets zao.

Kwa katiba hii ambayo Majaji ni wateule wa Rais shauri likipelekwa mahakamani ni vigumu kuishinda serekali.

Kwa katiba hii Tume ya uchaguzi wote ni wateule wa Rais,kura yako si chochote si lolote hasa inapokuwa inakwenda kinyume na matarajio ya Rais.Haki ya kura yangu kuhesabiwa hakuna kabisa.

Kwa katiba hii ardhi yote ni mali ya Rais,Ikiwa serekali au mawakala wa serekali (wawekezaji) watahitaji au watataka kuchukua ardhi yako hakuna mahali pa kwenda zaidi ya kuporwa ardhi yako kirahisi kwa mgongo wa maslahi ya umma.


Mpaka hapo umeongea mambo ya kufikirika Tu na mambo ya kisiasa

Turudi kwako personal, Tangu umezaliwa mpaka sasa na umri huo uliona, ulishawahi kupata changamoto yoyote ambayo ilibidi kuishitaki serikali?

Hapo kwenye tume ya uchaguzi, unataka kuwe na maroboti? Au wakina mbowe ndio wakawe wasimamizi wa uchaguzi?

Hata watumishi wa tume wakichaguliwa na wanainchi Kwa kupiga kura still hakuna Jambo litabadilika

Tume inakuwa mzuri vyama pinzani vikishinda ila tume inakuwa mbaya mkishindwa
 
Tueleze mapungufu ya katiba hii kwanza
Hili mbona lilielezwa sana na Jaji Warioba na Wajumbe wake wakati wanakusanya maoni kwa ajili ya kuandaa Rasimu ya Katiba ya Warioba,AU ulikuwa bado MDOGO?

Kukusaidia tafuta nakala ya Katiba hii ya 1977 na Rasimu ya Katiba ya Warioba,ujione mapungufu ya katiba hii ya KALE
 
Back
Top Bottom