kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 16,255
- 16,185
Katiba yetu inahitaji kuandikwa upya kwakuwa Ina kasoro nyingi sana na viraka vingi. Uandishi wake umeshatafuna hela zetu nyingi Sana lakini hatukufika mwisho kwenye awamu ya 4 na haitaandikwa upya kwenye awamu ya 5 ingawa rasimu ipo. Na inavyoonekana hakuna Rais kutoka CCM atapenda iandikwe upya kwakuwa ya Sasa Ina manufaa makubwa kwa Rais na kwa CCM.
Hata Kama watu hawaipendi Chadema au hawampendi Mh. Lissu lakini wanapenda katiba mpya imaliziwe kuandikwa.
Wako watu ambao Wanaweza kuichagua Chadema ili kazi ya kuiandika katiba ikamilike.
Katiba Ikishakamilika miaka 5 ijayo watu wataamua upya chama kipi chenye sera safi za kiuchumi, kijamii na zinazoliunganisha Taifa na watu wake kiongoze nchi.
Kwenye ilani ya CCM hakuna kifungu kinachogusia kumalizia kuiandika upya katiba, hivyo hawataandika katiba. Ila Chadema na ACT Wazalendo wako wazi kwenye Ilani zao kuwa uandishi wa katiba mpya Ni kipaumbele Chao.
Samahani Kama Kuna mtu nimemkera lakini katiba ndio moyo wa taifa.
Hata Kama watu hawaipendi Chadema au hawampendi Mh. Lissu lakini wanapenda katiba mpya imaliziwe kuandikwa.
Wako watu ambao Wanaweza kuichagua Chadema ili kazi ya kuiandika katiba ikamilike.
Katiba Ikishakamilika miaka 5 ijayo watu wataamua upya chama kipi chenye sera safi za kiuchumi, kijamii na zinazoliunganisha Taifa na watu wake kiongoze nchi.
Kwenye ilani ya CCM hakuna kifungu kinachogusia kumalizia kuiandika upya katiba, hivyo hawataandika katiba. Ila Chadema na ACT Wazalendo wako wazi kwenye Ilani zao kuwa uandishi wa katiba mpya Ni kipaumbele Chao.
Samahani Kama Kuna mtu nimemkera lakini katiba ndio moyo wa taifa.