Lakini kati ya Mechanical na Mechatronics ipi ina soko. Nimefuatilia Mechatronics nimeona ina soko kubwa huko nje lakini nikaona wanaongelea sana sijui Robotics nk
Huku 3rd world countries naona kama haitakuwa na soko hivi.
Halafu hapa nina swali, kwenye TCU guidelines naona wameonesha kozi za Mechanical Engineering nk kwa chuo cha ATC bachelor yake inachukua miaka 3 ila vyuo vingine ni minne. Je, hii haimaanishi kwamba kuna vitu wamevipunguza kwenye mtaala wa ATC?
Ukitokea advance unasoma miaka 4 , diploma ndio 3. Usiangalia Leo Yako dili zaidi na future Yako, huoni Technology sinavyobadilika ?
Tanzania Kuna engineer wengi wakenya na wahindi kwenye industries wanakula maisha sababu ya sisi wenyeji hatuendani na wakati.
Kwa sasa any machine ina mifumo ya electronics sio mechanical pekeyake na Engineer anahitaji kua na uelewa wa pande zote mbili, na muajiri hupendelea kuajiri mtu multipurpose.
Soko la ajira Mechatronics lipo vzr na linakua, waajiri wengi wanaelewa umuhimu wake.
Why mechatronics from ATC ni best option for your future ?
Ina cover Mechanical + electronics.
Best mentor from ATC , In ATC , utasomeshwa na Prof na doctors kutoka nchini na wageni (south Korea) , utapata exposure nzuri juu ya Mechatronics, ndani yake utajua Robotics na AI.
Every semester Kuna midterm project, hii inasaidia kukupima uwezo wako wa vitendo katika somo husika.
Pia wingi wa vifaa vya kusoma kivitendo, Utafanya practical na design katika field mbalimbali ikiwemo CAM / CAD , 3D printing Technology, Electropneumatic and Electrohydraulic, Industrial Automation , PLC programming , CNC , Material Testing , Circuit design , Embedded systems. Na hizo practical vyuo vingi tz hakuna.
Ukiwa makini utamaliza na ujuzi unaofanana na mazingira halisi ya kazi. Tofauti na graduate wa vyuo vingi tz . Maamuzi ni Yako , focus on present / future Yako.
Multipurpose, kazi zote kutoka utumishi na Private sector zinazohusu Mechanical, Mechatronics, Automation , Instrumentation , Material engineering unauwezo wa kuomba na ukapata.
Fanya maamuzi mazuri , Skills make the difference.
From ATC Mechatronics Engineering Alumni.