Kati ya mwanamke na mwanaume, nani huathirika zaidi ikitokea ndoa imevunjika?

Kati ya mwanamke na mwanaume, nani huathirika zaidi ikitokea ndoa imevunjika?

Kati ya mwanamke na mwanaume, nani huathirika zaidi ikitokea ndoa imevunjika?


  • Total voters
    57

Ben-adam

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2023
Posts
1,126
Reaction score
2,517
Kati ya mwanaume na mwanamke, nani hupitia maisha ya tabu zaidi ndoa inapovunjika? tukitazama hali halisi ya maisha ya Watanzania, ukweli unauma: wanawake wengi wanakosa uhuru wa kiuchumi!

Mwanamke wa Kitanzania analelewa kuamini kuwa mwanaume ndiye "mkombozi wake" kifedha. Matokeo yake, wengi wanapofiwa, kuachwa au ndoa kuvunjika, maisha yao yanaanguka ghafla. Kwa nini?
Hawakuwa na mpango B wa kiuchumi, angalia mtaani jinsi single mothers wanavyoishi kwa tabu, (Wana depression haó) na utagundua wengi maisha yao yamebdilika baada ya ndia zao kuvunjika au sababu zinazofanana na hiyo

Mwanamke anapobaki peke yake bila rasilimali au kazi ya uhakika, ana hatari kubwa ya kuishi maisha magumu sana. Wanaume wengi huweza "kusimama tena" kwa sababu waliwekeza kwenye kazi, biashara, au vyanzo vyao vya kipato.

Hata ukiwapa mtaji wa milioni 10, ni wangapi wataitumia vizuri na kuifanya iwe chanzo endelevu cha kipato? Fanya utafiti. Pesa za wanawake wengi huishia kwenye matumizi ya haraka, sio uwekezaji wa muda mrefu, ni wangapi wenye project zao wenyewe?

Mwanamke asiye na uhuru wa kiuchumi akipatwa na changamoto (mfano kufukuzwa kazi au biashara kuanguka), mara nyingi huchagua mojawapo kati ya haya:

Kutafuta mwanaume/wanaume wengine kwa msaada wa kifedha (kujiuza) au
Kurudi kwa wazazi
Kuhangaika na maisha yasiyo na uhakika

💥Ukweli mchungu ni huu: Mwanamke wa Kitanzania anahitaji mwanaume ili aendelee kuishi vizuri

Si kwa sababu hawezi, bali kwa sababu mfumo unamfundisha kutegemea zaidi badala ya kujitegemea.

Lakini je, hii ni lawama kwa wanawake pekee? Hapana.

Mfumo wa malezi unawajenga hivi.
Wanaume wengi wanapenda wake waliowategemez.
Fursa kwa wanawake bado ni chache ukilinganisha na wanaume.

Suluhisho ni nini?

Wanawake wafundishwe uhuru wa kifedha kutoka wakiwa wadogo.
Misingi ya ndoa ibadilike, ndoa isiwe mkataba wa utegemezi bali ushirikiano wa maendeleo.
Wanawake wajifunze kuwekeza na kusimama wenyewe hata wakiwa ndani ya ndoa.

Tukubaliane, ndoa ikivunjika, mwanaume anapata shida kiakili na kihisia, lakini mwanamke anapata shida zaidi kiuchumi. Na ukiwa na shida ya pesa, maisha yanakuwa magumu mara mbili zaidi!

Je, unakubaliana? Tupe mawazo yako!
 
Km wana watoto hao ndio waathirika wakubwa.. km hawajazaa hamna anayeathirika..!!
Kwa mimi na mama chanja alie athirika ni mama chanja ,kwa sababu watoto wapo kwangu ila yeye kaolewa na mume wake anampa stress kakonda kama baiskeli ya phonex.

Juzu kati kanipigia analalama hatari nikamwambia asubiri nachoma nyama huku nikiisubiri iive na lainisha koo kwa kinywaji changamshi kwanza😉😉
 
Anaweza kuathirika yeyote kutegemeana na aina ya maisha mliyokuwa mkiishi na muda mlio ishi pamoja. Ndoa inapovunjika mara nyingi ni furaha kwa mmoja na huzuni kwa mwingine... Kusema mwanamke pekee ndiye anayeathirika zaidi kwenye kila anguko la ndoa HAPANA. Yeyote yule anaweza anguka kivyovyote vile kutegemeana na misingi kadhaa
 
Kwa mimi na mama chanja alie athirika ni mama chanja ,kwa sababu watoto wapo kwangu ila yeye kaolewa na mume wake anampa stress kakonda kama baiskeli ya phonex.

Juzu kati kanipigia analamika hatari nikamwambia asubiri nachoma nyama huku nikiisubiri iive na lainisha koo kwa kinywaji changamshi kwanza😉😉
Huwa ni hivyo!! Kwa mwaka wa kwanza anaweza aka survive vizuri tu lakini kadri siku zinavyoenda mambo huanza kuwa magumu, na wengine hufika mbali na kuanza kutafuta sababu za kurudi. Atatumia watoto nk
 
Huwa ni hivyo!! Kwa mwaka wa kwanza anaweza aka survive vizuri tu lakini kadri siku zinavyoenda mambo huanza kuwa magumu, na wengine hufika mbali na kuanza kutafuta sababu za kurudi. Atatumia watoto nk
Yani mimi kumrudia asahau kabisa, aligusia hilo jambo nikamwambia aje na cheti cha John Hopkins hospital , kwamba hana magonjwa ya zinaa na aje na wazazi wake wote wawili na wawe na miaka 90.
 
Nadhani hiyo dhana ya kusema mfumo wa kimalezi unamtengeneza mwanamke kuamini kuwa mwanaume ndiye mkombozi wa maisha yake.

Niwazi kuwa huo mfumo ulikuwa unafanya kazi miaka ya zamani na sio sasa.

Mifumo mingi ya kisasa ambayo tupo nayo katika ulimwengu wa kileo ina empower wanawake katika sector nyingi.

Wanawake wa miaka ya sasa wamekuwa wanufaika zaidi kuliko wanawake walioishi miaka ya zamani kabla ya huu utandawazi kushika hatamu.

Baada ya Talaka nani ni mnufaika zaidi kati ya mwanamke na mwanaume?

Hiyo inategemeana na hali yenu ya kiuchumi ambayo mlikuwa nayo katika kipindi chenu cha ndoa.

Kama mwanaume alijenga nyumba kadhaa au mradi wowote au ana miliki baadhi ya asset basi its obviously kuwa hizo mali zitaenda kugawanywa nusu kwa nusu kupitia ile sheria ya 50/50 ambayo kizazi cha sasa kupitia women empowerment kimempa faida mwanamke.

That means kwa scenario hiyo ni upande wa mwanamke ndio utaoenda kunufaika zaidi kwenye talaka.

Ila kama mwanaume alikuwa maskini halafu ndoa ikavunjiia. Maana yake hapo hakuna cha kugawana chenye kumfaidisha mwanamke na kwa mantiki hii Talaka itakuwa na hasara kwa mwanamke.
 
Back
Top Bottom