JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,460
Mwanamke mkazi wa Kijiji cha Sibwesa Wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi, Wande Emmanuel (30), amemjeruhi mumewe, Dotto Enosi (35) kwa kumkata na panga kichwani kisha na yeye kujinyonga kwa kutumia kitenge.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi, Ali Makame Hamad, alisema tukio hilo lilitokea ljumaa, na chanzo ni ugomvi wa kifamilia unaohusiana na shughuli za kilimo.
Kamanda Hamad alisema mwanaume alikuwa akimtuhumu mkewe kwa kutoshiriki katika shughuli za kilimo, hivyo kusababisha ugomvi.
Alisema kutokana na ugomvi huo Wande aliamua kumkata kwa mapanga mumewe na kumjeruhi baada ya kugundua kuwa anaweza kufariki na yeye kutuhumiwa kwa kesi ya mauaji.
Alisema baada ya kumjeruhi, Wande alizunguka nyuma ya nyumba yao na kujinyonga.
Kamanda Hamad alisema Dotto alipelekwa Hospitali ya Rufani mkoani Katavi kwa ajili ya matibabu, na sasa hali yake inaendelea vizuri.
Chanzo: Nipashe
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi, Ali Makame Hamad, alisema tukio hilo lilitokea ljumaa, na chanzo ni ugomvi wa kifamilia unaohusiana na shughuli za kilimo.
Kamanda Hamad alisema mwanaume alikuwa akimtuhumu mkewe kwa kutoshiriki katika shughuli za kilimo, hivyo kusababisha ugomvi.
Alisema kutokana na ugomvi huo Wande aliamua kumkata kwa mapanga mumewe na kumjeruhi baada ya kugundua kuwa anaweza kufariki na yeye kutuhumiwa kwa kesi ya mauaji.
Alisema baada ya kumjeruhi, Wande alizunguka nyuma ya nyumba yao na kujinyonga.
Kamanda Hamad alisema Dotto alipelekwa Hospitali ya Rufani mkoani Katavi kwa ajili ya matibabu, na sasa hali yake inaendelea vizuri.
Chanzo: Nipashe