Kasi ya Mnyika yamtisha JK

Kasi ya Mnyika yamtisha JK

Ni vigumu sana kupingana na ukweli, Mnyika daima alisimamia ukweli wa tatizo la maji Ubungo na DSM kwa ujumla, lakini Bunge kupitia Spika, Naibu wake na wabunge wa CCM wao walisimsmia uongo ndio maana mwisho wao unakuwa ni aibu.

"Njia ya muongo ni fupi" ndicho Anna Makinda na Ndugai walichopanda na sasa acha wavune.
 
Kasi ya Mnyika imtishe Jakaya? Kweli akutukanaye hakuchagulii tusi, Makocha wa Mnyika wamelambishwa sakafu kwa Nyakati tofauti, Mbowe 2005,Slaa 2010. Kama mnadhan kuitwa Ikulu ni ishu hata Mzee Yusuph Mzimba wa Yanga Asili na Mzee Dalali wa Simba kwa Nyakati tofauti wameenda magogoni kuzungumza na Mzee, Jakaya ni wa wote bila ya kujali Itikani,dini,kabila,jinsia wala kipato Hata mateja kama Ray C washaenda!
Songoro!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! umeishushia heshima ikulu na rais, hawa ulio wataja walienda kutalii, sasa sijui unamanisha kuwa agizo la rais halina umuhimu wowote kwa hiyo walioitwa nao wanaenda kutalii pia?

Nani kati ya uliowataja alishawahi kumtuhumu rais kuwa mdhaifu?

Ulichokiandika ni sawa na kulinganisha wabunge na wageni waalikwa bungeni!. PU*#@*U!
 
Last edited by a moderator:
Safi sana Mnyika ka kulivalia njuga tatizo la maji kwenye jimbo lako, nampongeza pia Rais Kikwete kwa hatua alizochukua kutaka kumaliza tatizo la maji, pia imedhirisha jinsi viongozi wa serikali yetu wasivyo na mipango thabiti ya kumaliza tatizo la maji, mpaka Rais anagundua kabisa kun ubabaishaji, namshauri angewafukukuza kazi hao wababaishaji ili tusonge mbele
Dah, heri yao wenzetu waliochagua mbunge wa watu. Sisi wa ukonga tuliyechagua CCM tulie tu. Yaani kule tuna mbunge ambaye hata kwa sura hatumfahamu. Hatumsikii bungeni wala jimboni. Kuwa na mbunge wa CCM ni kama laana.
 
Kasi ya Mnyika imtishe Jakaya? Kweli akutukanaye hakuchagulii tusi, Makocha wa Mnyika wamelambishwa sakafu kwa Nyakati tofauti, Mbowe 2005,Slaa 2010. Kama mnadhan kuitwa Ikulu ni ishu hata Mzee Yusuph Mzimba wa Yanga Asili na Mzee Dalali wa Simba kwa Nyakati tofauti wameenda magogoni kuzungumza na Mzee, Jakaya ni wa wote bila ya kujali Itikani,dini,kabila,jinsia wala kipato Hata mateja kama Ray C washaenda!

Huna hoja!
 
JJ Mnyika ni jembe ni wanasiasa wlaiopikwa wakapikika wasio natamaa bali wamtenguliza utaifa,uzalendo na uadilifu wa hali ya juu,Mungu akutangulie na kunyosha mapito yako Mbunge wa Ubungo
 
Msitusahau na sinza!! Hakunaga maji ni shida kweli kweli!
 
Hongera Rais kwa kukubali ukweli na huo ndo ukomavu wa kisiasa.
Hongera sana Mbunge Mnyika kwa msimamo thabiti usioyumba kuwatetea watu wako. Huo ndiyo uingozi shupavu, natamani sana tungekuwa na wabunge aina yako tanzania ingesonga mbele.
Hongereni wanainchi wa ubungo kwa chaguo sahihi, mwisho tunahitaji maji na si mbwembwe.
MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Niliona kwenye ITV bendera za CHADEMA kwenye msafara wa Rais.

Sent from my GT-I9100 using Tapatalk 2

Mkuu Dingswayo

Hiki ki message "Sent from my GT-I9100 using Tapatalk 2" una kiset vp
Na mie natumia ka GT-I9100, nataka ku set haka ka message
 
Last edited by a moderator:
[QUOTE=Tafadhali mtandao niwa watu wenye hekima matusi si sawa.Moja ya dhamila ya JF ni kupeana habari na kuelimishana. Mh.Mnyika ni sauti iliyotumwa na wana DSM/PWANI kufikisha ujumbe kwa Rais ya kwamba pamoja na matatizo yanayokumba Mkoa huu na Pwani ni maji. Kama sauti yake imesikika BRAVO. Hili halina mjadala na kumpongeza hakuna itikadi ya kisiasa.Fikiria adha ya maji Dsm.Kila pande zote ni uhaba wa maji na kama yakipatikana ni ghali na si salama ,mfano umeme majumbani hata ukikosa utatumia kibatari au mshumaa. Kutokana na busara za Mh Mnyika hongera kwa maono hayo mungu atakusaidia.Hata CCM wakitoa vilio vya wengi mkono tutaunga.Ushauri kwa kipindi hiki kigumu inaombwa wote wauza maji safi kuweni na huruma punguza bei ya ndoo na vilevile msichakachue ubora wake. Mh.Mnyika hebu fuatiliatena deni la Dowans manake umeme nalo kero.
 
Mahanga ni mhanga hata ubunge kachakachua.Kama aliwahi kuwa Wizara ya Barabara kwa sasa atafanya nini? Mwacheni 2015 kushnei.Watu wa Segerea msilie msikitie matendo yenu ya unafiki na ukabila.Onyango kama Odinga
 
Dah, heri yao wenzetu waliochagua mbunge wa watu. Sisi wa ukonga tuliyechagua CCM tulie tu. Yaani kule tuna mbunge ambaye hata kwa sura hatumfahamu. Hatumsikii bungeni wala jimboni. Kuwa na mbunge wa CCM ni kama laana.
Siita lukolo hiyo mijitu ya ccm ilisha laaniwa. Ila tulikua wajinga wakati wa kwenda wakati wa kurudi tutakua waelevu.
 
Mkuu Dingswayo

Hiki ki message "Sent from my GT-I9100 using Tapatalk 2" una kiset vp
Na mie natumia ka GT-I9100, nataka ku set haka ka message

Si ku set Mkuu, imekujatu na software ila sikuifanyia editing. Fungua app ya Tapatalk, nenda settings utaona sehemu imeandikwa Tapatalk signature, fungua hapo na unaweza ku edit.
 
hivi kikwete mpaka mnyika andamane ndio ajue mji hakuna Dar?
huyu kweli anatatizo la kutokujua au kufahamu. kama hakuna mnyika hakuna maji?
 
8E9U7951.JPG
muh mnyika aonesha utii, bashasha na tabasamu kwa mkuu wa nchi. huu ndiyo uzalendo. usipomtambua na kumheshimu mkuu wa nchi, hayo maji atayaleta nani? mnyika peke yake hana ubavu huo. lazima apate ridhaa na nguvu ya mkuu. nasikia suala la maji limo kwenye ilani ya ccm ya 2010- 2015. ccm wanasema mnyika anadandia tu
8E9U8052.JPG

tehtehteh! JK na mnyika wakishirikiana katika uzinduzi wa daraja lililojengwa na serikali ya ccm. safi sana mnyika kwa ushirikiano!
8E9U7984.JPG
mnyika yuko nyuma ya mkuu. huo ndiyo utii na ushirikiano!
8E9U8065.JPG
jk akiliteka jimbo la ubungo kimtindo
8E9U8191.JPG
jk akifurahia ushindani wa vyama vya ccm, chdm na cuf. sielewi bendera nyingi ni za chama gani katika jimbo la mnyika! tushindane bila kuumizana
 
Nafuuuu.............!!!!, Nafuuuuuuuuuu..........!! ENJOY FASTJET! SERVICIES.
 
Back
Top Bottom