Hapo ni kuanzia mwaka 2005 hadi 2012.Inakuwa kama Trilion 1 na mil mia moja hivi
Jiulize kama rais akitulia nyumbani kujenga nchi kama tunahitaji kukopa kopa.Mi nadhani safari zake zilikuwa na misukumo binafsi kama utalii nk.Mikopo ya Nje yenye Masharti ya Kibiashara
32. Mheshimiwa Spika, mwaka 2011/12 Serikali ilikadiria kukopa kiasi cha Dola za Marekani milioni 822, sawa na shilingi bilioni 1,271.6 kama mikopo ya kibiashara. Katika kipindi cha Julai 2011 hadi Aprili 2012, Serikali ilisaini Mkataba wa mkopo wa kiasi cha Dola za Marekani milioni 310 na Benki ya Standard ya Afrika Kusini. Hadi kufikia Aprili 2012, jumla ya Dola za Marekani milioni 229 ambazo zilitumika kulipia madeni ya barabara ya mwaka 2010/11. Aidha, Serikali ilisaini Mkataba wa mkopo wa Euro milioni 61 na Benki ya HSBC. Mkopo huu umeelekezwa kugharamia ujenzi wa mtambo wa kufua umeme wa megawati 60 Nyakato Mwanza. Serikali pia imesaini mkataba wa mkopo wa Dola za Marekani milioni 350 kutoka Benki ya Credit Suisse ya Uingereza ambapo Dola za Marekani milioni 200 zimepokelewa mwanzoni mwa Mwezi Juni 2012. Kiasi kilichobaki cha Dola za Marekani milioni 150 kitapatikana na kutumika mwaka 2012/13.
Tumezoea...CCM hakuna wa kumfunga paka kengele...dawa yao ni kuwang'oa 2015...
hawachukuliwi hatua kwasababu hiyo ngoma ilikuwa igawiwe pasu kwa pasu...watu wanaghushi document kutaka kuiba bilioni 3 wanahamishwa vitengo wakati mwalim anaiba shs.milioni 1 anafungwa miaka 10. kila siku Rais anaimba nchi kuongozwa kwa sheria wakati anaficha majambazi nyumbani kwake ikulu.
Hadi mwaka jana mwezi wa tiza tarehe 11 kwa mujibu wa Jason Bourne | The greatest WordPress.com site in all the land! mara ya mwisho saf
ari yake ilikuwa ni ya 337.Sasa zidisha hiyo kwa 3 bil tzsh.Halafu watumbie walichokipata in return kwenye safari hizo.
NO. Something is not right.
Utaratibu na sheria gani ya mtu/watu kutaka kughushi na kujipatia Tsh 3 billion halafu adhabu anayopata/wanayopata ni kushushwa cheo au kubadilishwa idara. THIS IS THE JEST OF FOOLS.
Halafu cha kushangaza, huyu jamaa, Mahadhi, sijui naibu Waziri. Haoni hata soni mbele ya kusanyiko la waandishi wa habari kusema maneno ya kitoto na kijinga kama haya.
TAKUKURU IS JUST A BATCH OF JOKE. Kwani wanapowapeleka watu mahakamani kwa rushwa za kishenzi shenzi huwa lazima waombe idhini kutoka kwa Rais?. Wanashindwa hata kuutetea uongo wao.
Vyombo vyetu vya habari navyo ni madudu tupu. Hakuna chombo cha habari chochote kilichofuatilia sakata hili kwa mwaka mzima mpaka linaletwa tena na Mh. Lowassa
Thanks Lowassa hata kama una motive nyingine kisiasa.
Hata hili halieleweki, wewe naona akili zako kuna mtu anazo kakushikia, mwambie akurudishie unadhalilika huku.
Kwanza mbona nchi hii ni full uislamu kila idara? Lakini pili, wangekuwa ni akina abeli, joshua, john, au yohana ungeone magari ya washawasha ya polisi na ving'ora yanavyopishana kuwafikisha mahakamani na kuwakuza kazi. Lakini kwakuwa ni wao watupu hatma anaachiwa raisKITAIFA
Na Patricia Kimelemeta, Mwananchi
Posted Jumanne,Marchi19 2013 saa 21:35 PM
KWA UFUPI
Mpango huo unadaiwa kusukwa Juni mwaka jana kwa maofisa haokuitaka Wizara ya Fedha kutoa kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya safari hewa ya Rais.
Dar es Salaam. Sakata la Mkuu wa Itifaki wa Ikulu, Anthony Itatiro, ambaye anahusishwa na njama za kutaka kuchota kiasi cha Sh3 bilioni kwa ajili ya safari hewa ya Rais, limechukua sura mpya baada ya Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje kutaka kujua hatima ya kigogo huyo jana.
Itatiro na maofisa wanne wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa walituhumiwa mwaka jana kuidhinisha kuchota kiasi hicho cha fedha bila ya kuwapo kwa ziara ya Rais kwenda nchi yoyote ya kigeni.
Mpango huo unadaiwa kusukwa Juni mwaka jana kwa maofisa haokuitaka Wizara ya Fedha kutoa kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya safari hewa ya Rais.
Naibu Waziri wa wizara hiyo, Juma Mahadhi alitoa maelezo hayo baada ya kuulizwa swali na Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje ya Bunge, Edward Lowassa.
Lowassa, ambaye pia ni Mbunge wa Monduli aliuliza swali hilo ghafla kwa Mahadhi wakati akitoka nje, baada ya kumalizika kwa kikao cha kamati yake kilichofanyika kwenye ofisi za Bunge jijini Dar es Salaam.
Mahadhi, ambaye alilazimika kutoa ufafanuzi wa swali hilo baada ya kubanwa zaidi na waandishi wa habari, alisema Rais Kikwete ndiyo mwenye mamlaka ya kuchukua hatua dhidi ya Itatiro kutokana na ripoti ya uchunguzi ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na Mkaguzi wa Ndani wa Wizara hiyo.
Alisema pia kuwa walishauriwa kuwa maofisa walioshirikiana na Itatiro nao wachukuliwe hatua za kinidhamu kufuatia njama hizo.
Alipotafutwa kuzungumzia suala hilo, Katibu Mkuu Ombeni Sefue hakupokea simu. Pia hakujibu pindi alipotumiwa ujumbe mfupi kwa njia ya simu. Naye Katibu Mkuu katika Ofisi ya Rais anayeshughulikia Utumishi, George Yambesi alisema hakuwa tayari kuzungumzia suala hilo kwani alikuwa likizo.
Mahadhi alisema wakati tukio hilo linatokea viongozi wakuu wa wizara hiyo walikuwa kwenye majukumu mengine ya Serikali, jambo ambalo lilisababisha nafasi zao kukaimiwa na watendaji hao.
Wale maofisa walitumia mwanya wao wa kukaimu nafasi ile ndiyo wakasuka mpango huo, aliongeza Mahadhi.
Alisema kutokana na hali hiyo baadhi ya maofisa hao wamechukuliwa hatua za kinidhamu ikiwamo ya kuwashusha vyeo na kuwabadilisha vitengo.
Mahadhi alisema kwamba huwa ni utaratibu wa kawaida kwa Rais anaposafiri maofisa wa Itifaki na wale wa Wizara ya Mambo ya Nje kupewa fedha na hazina kwa ajili ya kufanikisha ziara zake.
Ila maofisa hawa walitumia mwanya huo kuihadaa Wizara ya Fedha kwa kuandaa hoja ya safari feki ili kupata fedha hizo, aliongeza Mahadhi.
Maofisa wengine ni pamoja na ofisa katika Idara ya Itifaki, Shamim Khalfa, Kaimu Mhasibu Mkuu, Kasim Laizer, Mhasibu, Deltha Mafie na karani wa fedha) aitwaye, Shabani Kesi.