Ndugu wana Jamiiforums,
Tunashukuru kwa maoni yenu mliyoweka hapa juu ya utendaji mliouona kuwa si wa kuridhisha hasa kwa maendeleo ya benki yenu pendwa, NMB inafanyia uchunguzi maoni na malalamiko hayo na kama ikibainika kuna watu kwa makusudi wamefanya hayo, tunawahakikishia kuwa tutachukua hatua stahiki dhidi yao na wafanyakazi wengine wenye tabia kama hizo.
Ndugu wanajukwaa, NMB inajipambanua kwa kusimamia maadili mojawapo ikiwa ni uaminifu kwa wafanyakazi wake.
NMB pia inapenda kuwahakikishia wateja na jamii kwa ujumla kwamba itaendelea kusimamia sera zote za benki ikiwa ni pamoja na kutovumilia wafanyakazi wasio waadilifu.
Endapo kutatokea umepata huduma isiyoridhisha au ufanyajikazi usiofuata maadili, uaminifu na uadilifu, tafadhali toa taarifa kupitia njia zifuatazo:
1.
Kupitia tovuti: http://www.nmbtz.com
2.
Kupitia e-mail maalumu: whistleblower@nmbtz.com
3.
Kwa Posta – Unaweza kutuma barua kwa Afisa Mtendaji kama ifuatavyo:
Afisa Mtendaji Mkuu (Bahasha iandikwe “Siri”)
Makao Makuu ya NMB,
P. O. Box 9213,
Azikiwe/Jamhuri Street,
Dar es Salaam, Tanzania.
4.
Au kwa kupiga simu zifuatazo:
0658 751 000
Tigo
0779 751 000
Zantel
0685 751 000
Airtel
0800 751 000
Vodacom