Deleted_account
JF-Expert Member
- Nov 1, 2008
- 3,385
- 3,702
Ni maeneo ya kigamboni-kibada askari polisi wamempiga dereva wa magari makubwa yanayosafirisha mafuta. Polisi walimpiga vibaya dereva huyo juzi usiku bila kuwa na sababu za msingi,wamechukua vitu vyake ikiwemo hela cash zaidi ya laki 6,simu yake,mchele,etc na wakamuacha hapohapo,kibaya ni kwamba hata wananchi walitaka kuingilia lakini waliogopa kwasababu polisi walikuwa na bunduki. Taarifa zimemfikia IGP na sasa hivi mkuu wa kituo kigamboni anashughulikia hilo suala. Kwenye hiyo defender ya polisi alikuwa mtu anaitwa khatibu (a.k.a mavi) ni maarufu kwa kupiga watu na mwanamke anaitwa Suzy aka sunita huyu anamjua huyo dereva na wakati wanampiga alimtaja kwa jina " sunita tunakunywaga wote pombe kwanini unanipiga?" wamemuumiza vibaya sana.