Kashfa mpya: Kamati ya Bunge yahongwa

Labda anamaanisha ana mashine za kusaga nafaka kule Same anasambaza unga wa sembe!!!! Kama ni mengineyo naanza kurudia yale yale, kwamba sasa wezi wanatugeuzia kibao. Na bado. Kamati inayolengwa sina shaka kwamba ni ya Kina Mwakyembe na tutasikia mengi sana mwaka huu hadi tuwaachie kina Lowassa na Rostam wapete, vinginevyo kila kukicha kutakuwa na mapya. Kwa sasa nazidi (nilikuwa) kutilia shaka Tanzania Daima. Nitafafanua siku nyingine.

Mkuu Halisi,

Hawa Tanzania Daima nao wamepata virus vya Rostam nini?

Nimeona makala zao kama mbili tatu, nikakuna kichwa kwamba kulikoni hapa?
 
Labda anamaanisha ana mashine za kusaga nafaka kule Same anasambaza unga wa sembe!!!! Kama ni mengineyo naanza kurudia yale yale, kwamba sasa wezi wanatugeuzia kibao. Na bado. Kamati inayolengwa sina shaka kwamba ni ya Kina Mwakyembe na tutasikia mengi sana mwaka huu hadi tuwaachie kina Lowassa na Rostam wapete, vinginevyo kila kukicha kutakuwa na mapya. Kwa sasa nazidi (nilikuwa) kutilia shaka Tanzania Daima. Nitafafanua siku nyingine.

Kaka tunakuamini kaka....punguza munkari. Ur objectivity katika mapambano haya ni muhimu sana. siamini kama umeshindwa kufuatilia hii habari kwa undani zaidi na kufikia conclusion hizi

omarilyas
 
Kashfa mpya: Kamati ya Bunge yahongwa

Siasa za Bongo..kinyaa kitupu.
Si jui lini tutakaa chini na kutuliza makalio yetu kuhusu mustakabali wa maendeleo ya nchi yetu.badala ya kuumiza vichwa nyetu kufikiri tutatumiaje maliasili zetu alizotupa mungu kujikwamua kiuchumi hususani tuwe na umeme wa kudumu,maji ya uhakika ya tape,hospitali safi ,barabara safi,na mingineyo mazuri.

Badala yake tuna leta bla bla tu.Muda unakwenda wenzetu Rwanda wanapiga hatua japokuwa walikuwa na matatizo yao ya 1994 na hawana ardhi ya kutosha.Siiombei inchi yangu balaa lakini hawa mafisadi wanatutengenezea bomu,kuna siku watu(waliochoka na maisha hasa vijana wasio kuwa na kazi, forget not they have nothing to lose at all) watakapoingia mitaani wakitaka chao.

Hebu tujikumbushe kidogo kwani historia hujirudia:

WAKATI akichukua madaraka mwaka 1774, Mfalme wa Ufaransa, Louis XVI alikuta nchi imetopea katika lindi la uozo kijamii na kiuchumi kutokana na uongozi mbovu wa wafalme waliomtangulia.

Bunge lilikuwa la kitabaka, likiwakilisha matakwa ya walio nacho na matakwa ya Mfalme mwenye kauli isiyopingwa (L'Etat C'es Moi), aliyejiaminisha kuwa yeye ndiye alikuwa Ufaransa na Ufaransa ilikuwa ni yeye.
Raia waligawanywa katika matabaka matatu yenye hadhi tofauti kisiasa, kijamii, kiuchumi na katika kutendewa haki



Tabaka la tatu na la mwisho, lilikuwa la makabwela, lililojumuisha wakulima wadogo wadogo, wachuuzi, wafanyabiashara na wasomi. Hawa hawakuwa na fursa yoyote ya kufikia matabaka mawili ya juu

Moyo mgumu wa Mfalme Louis katika kuridhia maslahi na matakwa ya wakuu wengi haukumsaidia siku ilipowadia, Julai 1789, pale umma wa walala hoi wa Kifaransa, kwa kuchoshwa na "sikio la kufa", ulipofanya mapinduzi kwa njia ya maandamano yaliyotikisa mitaa ya Jiji la Paris, kisha kusambaa hadi vijijini. Magereza yalivunjwa, na wafungwa kufunguliwa, Ikulu (the Bastille) ikavamiwa, Loius na mkewe, Marie Anttoinete wakajaribu kutoroka, lakini wakakamatwa mpakani mwa nchi na kurejeshwa Paris, kisha wakanyongwa kwa usaliti wa Taifa.

Hatimaye Septemba, 1791, katiba ya kidemokrasia iliyokuwa ikingojewa kwa hamu na wanyonge wote, yenye kubainisha haki asilia za binadamu, haki za raia na mgawanyo wa madaraka, ikazaliwa.



Na muda wakuwapiga chini nafikiri iwe 2010.Wasiwasi wangu huko vijijini watu sijui wanauelewa na maweamka kiasi gani? maana yake CCM na propaganda zao za kuwafikisha baadhi yawazito kunako court huku wakitucheza shere itakuwa rungu lao tosha la kurudi madarakani kwa kishindo.tukumbuke hizi nondo zinazopatikana JF almost wanazipata waliopo mijini na wenye access ya internet.Magazeti kama kawa ndio kabisa,Tv usiseme kwanza umeme utatoka wapi wa kuwasha hizo TV zao??.
Ili tufanikiwe inabidi tuangalie strategics nyingine ili kufanikisha ukombozi wa inchi hii kutoka mikononi mwa wachache wezi.tusitegemee magazeti na mitandao tu kwamba tutafanikiwa vita hii.

Anyway nafikiri tuendelee kuishi kwa matumaini kwamba ipo siku mapinduzi ya kweli yatakuja.Naamini uwezo tunao basi tuanzeni kujaribu 2010.
 
Kamati inayoongoza kwa BAHASHA za kaki toka kwenye zile taasisi za umma inazozikagua ni ile anayoiongoza Mh.Zitto.
 
Hivi sheria za nchi ( Tanzania) sinasema nini kuhusu sikuukuu ya wajinga April 1st?..

MJ
 
Back
Top Bottom