PostGE2025 Bunge la Ulaya (EU) lapinga Msaada wa Euro Milioni 156 (Tsh. Bilioni 440+) kwa Tanzania. Wataja Haki za Binadamu na Uchaguzi wa 2025

PostGE2025 Bunge la Ulaya (EU) lapinga Msaada wa Euro Milioni 156 (Tsh. Bilioni 440+) kwa Tanzania. Wataja Haki za Binadamu na Uchaguzi wa 2025

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Makumbele

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2009
Posts
287
Reaction score
1,222
Wakuu,

Kuna mvutano mzito unaoendelea huko Ulaya kati ya Bunge la Umoja wa Ulaya (European Parliament) na Kamisheni ya Umoja wa Ulaya (European Commission) kuhusu mpango wa kuipatia Tanzania msaada wa kimaendeleo wa kiasi cha Euro Milioni 156 (zaidi ya Tsh. Bilioni 440).

Kwa mujibu wa taarifa zilizochapishwa na jarida la Euractiv leo Juni 3, 2026, Wabunge wa Ulaya wameungana kupinga vikali kutolewa kwa fedha hizo kwa sasa. Wameituhumu Kamisheni ya Ulaya kwa kutaka kutoa fedha hizo bila kuweka masharti madhubuti ya kulinda haki za binadamu.

Mambo Muhimu Yaliyojitokeza Kwenye Sakata Hili:
  1. Vurugu na Vifo vya Baada ya Uchaguzi (Oktoba 2025): Wabunge wa EU wameibua hoja nzito kuhusu ukandamizaji wa maandamano kufuatia uchaguzi mkuu uliopita wa Oktoba 2025. Kwenye taarifa yao, wanadai kuwa zaidi ya watu 500 walipoteza maisha kwenye vurugu hizo.
  2. Kufungwa kwa Tundu Lissu: Bunge hilo limehoji kuendelea kuswekwa gerezani kwa zaidi ya mwaka mmoja kwa kiongozi wa upinzani, Tundu Lissu. Wabunge hawa (wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje, David McAllister) wanadai mashtaka anayokabiliwa nayo ni ya kisiasa.
  3. Mvutano wa 'Nani Asimamie Fedha Hizo?': Awali, msaada huu ulisitishwa mwaka jana baada ya Bunge kupiga kelele. Ili kutatua hili, Kamisheni ya Ulaya ikapendekeza kuwa fedha hizo zisimamiwe nje ya udhibiti wa moja kwa moja wa Serikali ya Tanzania. Hata hivyo, Wabunge bado wamekataa wakisema mpango huo hauna masharti ya kutosha (meaningful conditionality) na hauoneshi hatua stahiki endapo hali ya Haki za Binadamu zitazidi kudorora.
  4. Kuzuiwa kwa Ziara ya Wabunge wa EU: Inaelezwa kuwa Mei mwaka huu (2026), Tanzania iliahirisha ziara iliyokuwa imepangwa ya Wabunge wa EU kutoka kamati ndogo ya Haki za Binadamu. Hatua hii imewakasirisha zaidi Wabunge hao wanaodai Tanzania haioneshi utayari wa kufanya mazungumzo.
Kamati ya maendeleo ya Bunge hilo tayari imepiga kura kupinga mpango wa Kamisheni wa kutoa fedha (Kura 81 zilikubali kupinga, 1 ikikataa). Kura ya mwisho ya Bunge zima inatarajiwa kupigwa mwezi huu. Ingawa kiutaratibu Bunge haliwezi kuilazimisha Kamisheni kubadili msimamo moja kwa moja, hili ni shinikizo kubwa sana la kisiasa linaloweza kuzuia mabilioni haya.

Je, mnadhani hatua hii ya Wabunge wa Ulaya itakuwa na msaada wowote kwa kuzingatia hali halisi ya kisiasa inayoendelea nchini baada ya Uchaguzi wa 2025?
  • Mpango wa Kamisheni ya Ulaya kutaka kutoa fedha hizo lakini nje ya udhibiti wa Serikali, mnauonaje kiusalama na kidiplomasia? Je, ni dharau kwa 'mamlaka ya nchi' (wazee wa 'sisi ni nchi huru' hapa najua wataibuka) au ni tahadhari ya wafadhili?
  • Kama msaada huu wa Tsh. Bilioni 440+ ukikwama jumla, mnadhani sekta zipi za kimaendeleo zitaathirika zaidi?
Chanzo: Euractiv - https://www.euractiv.com/news/european-parliament-revolts-over-eus-e150m-aid-for-tanzania/
 
Kamati za Mambo ya Nje na Maendeleo katika Bunge la Ulaya zimepiga kura kulitaka Bunge la Umoja wa Ulaya kuondoa mpango wa utekelezaji wa kila mwaka (Development Assistance) kwa Tanzania.

Matokeo ya upigaji kura: 81 wameunga mkono 1 dhidi ya 4 ambao hawakupiga kura.

===============

Foreign Affairs and Development Committees at the European Parliament have voted on asking the EU Commission to withdraw Annual Action programme (Development Assistance) for Tanzania.

Voting results: 81 in favour 1 against 4 abstentions
 
Muda mgumu sana kwa watawala haramu

TAARIFA YA HABARI ILIYOCHAMBUA ZIARA YA SAMIA URUSI KWA KINA IKIFUKUA MAKABURI YOTE 03 JUNE 2026

View: https://m.youtube.com/watch?v=RpBLOV4tYfw
Tanzanian President Samia Suluhu Hassan has commenced a critical three-day state visit to Russia to meet with President Vladimir Putin, marking the first such visit by a Tanzanian leader in nearly 60 years.

The high-stakes trip comes at a time when Tanzania's relations with the West have frayed over severe human rights concerns, including allegations of deadly electoral violence, political abductions, and crackdowns on activist groups.

Unapologetic about the crackdown, President Hassan is looking to secure vital economic lifelines.

Accompanied by a large business delegation, her agenda focuses on expanding bilateral trade, tourism, and mineral partnerships.

As Washington reviews its ties with Dodoma, Moscow continues to rapidly expand its strategic footprint in East Africa.
 
Foreign Affairs and Development Committees at the European Parliament have voted on asking the EU Commission to withdraw Annual Action programme (Development Assistance) for Tanzania.

Voting results: 81 in favour 1 against 4 abstentions
Their assurance was already reduced to less than 300m euro

Very insignificant
 
Foreign Affairs and Development Committees at the European Parliament have voted on asking the EU Commission to withdraw Annual Action programme (Development Assistance) for Tanzania.

Voting results: 81 in favour 1 against 4 abstentions
Mwafrika ana asili ya ujinga sana vikwazo hivi pia vitaenda kumkandamiza yeye binafsi lakini atafurahia kama #ZUZU!
Kwa ukubwa wa mwenyezi mungu huenda yeye mshangiliaji ndiyo vikamkaba mara 50!
-Wengine tukiona ya aina hii huwa tunamfikiria mtu wa chini,elewa rais aumii wala hakuna kiongozi ataumia,ni miradi itachelewa kufanyika,infact #UZUZU_MBAYA_SANA.
 
Back
Top Bottom