Karibuni Mtaa wa MANGOMA (MUSIC Boulaverd).....D

Karibuni Mtaa wa MANGOMA (MUSIC Boulaverd).....D

Balantanda

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2008
Posts
12,484
Reaction score
4,825
Salama wakuu?.......

Nawakaribisha katika mtaa wetu huu wa mangoma(music boulaverd).....

Hapa tutajikumbusha mangoma yaliyotamba kipindi kileeee cha miaka ya 80 na 90 mwanzoni(91-92). Tutaaangalia wanamuziki/vikundi vilivyotamba enzi hizo,kumbi za muziki bongo zilizotamba enzi hizo,ma DJ waliotamba enzi hizo pamoja na wacheza Disco waliotamba enzi hizo(ambao walicheza mitindo kama Chacha, Beak Dance, Roboti, Bumping, Michael Jackson Style) ....

Leo nianze na ma DJ waliotamba enzi hizo pamoja na kumbi walizokuwa wakifanya vitu vyao.....

- DJ Chris Phaby "The Lover"- Huyu alikuwa anafanya vitu vyake Mbowe/Margott...
- DJ Ngomely, na DJ Kim(Abdulakim Magomelo),DJ Pop Juice- Hawa walikuwa wakifanya vitu vyao pale Rungwe Oceanic Beach Resort...
- DJ John Peter Pantalakis(JPP), DJ Choggy Sly na DJ Kalikali- Hawa walikuwa wakifanya vitu vyao Silver Sands na baadae wakahamia YMCA..
- DJ Eddy Sally na DJ Sweet Francis- Hawa walikuwa wakifanya vitu vyao pale Keys Hotel....
- DJ Seydou na DJ Yaphet Kotto- Hawa walikuwa wakifanya vitu vyao RSVP Club(RSVP Discotheque) a.k.a Mbowe...
- DJ Super Deo, DJ Paul MacGhee, DJ Joe Johnson Holela na DJ Young Millionaire- Hawa walikuwa Vision 200 Discotheque...
- DJ Mehboob- Yeye alikuwa Africana....
- DJ Emperor(Joseph Kusaga), DJ Bonny Luv na DJ Jesse(Mawingu Disco)- Hawa alikuwa akifanya vitu vyake pale New Africa Hotel....
- DJ Justin Kusaga - wa Mawingu/Clouds Disco pale Morogoro....
- DJ Nigger Jay(Masoud Masoud) - Yeye alikuwa pale YMCA....

Mimi nawakumbuka hawa kwa sasa,naomba tuendelee kujuzana wakuu wangu....

Karibuni sana kwenye Mtaa wa Mangoma....

Bala.
-
 
Hebu kabla sijaendelea zaidi tuburudike na kitu hiki Get Down on It wa Kool and The Gang.....

<strong>
 
Last edited by a moderator:
 
Last edited by a moderator:
sikuwa dar miaka hiyo ila nayakumbuka sana matangazo yao kwenye magazeti ya chama cha magamba yalikuwa yanahamasisha sana. chris phaby the lover nadhani alikuwa top
 
Na hiki...............All that she wants-Ace of Base.....




Napenda music, Thread zako kuna infor hua unatoa i really wish ningekua najua...
for hua ziko interesting especially ile ya BENDI ZETU ZA ZAMANI... enways...
hii ni moja ya oldies ambayo sichoki kusikia.... it a beautiful song,,
 
Last edited by a moderator:
Na hiki hapa

 
Last edited by a moderator:
Du..Mkuu Balantanda, we uko well stocked na madudu ya enzi hizo!
Hakika hata mimi sikuwa Dar kipindi hicho ila majina yoye hapo juu yalikuwa juu sana!
Hivi DJ JD Matlou amekuja kipindi gani?...au ndo wa juzijuzi?
 
Hahaaaaaaaaaaaaa......Dah...

Old is Gold bana...

 
Last edited by a moderator:
The Wacko Jacko..........

 
Last edited by a moderator:
Du..Mkuu Balantanda, we uko well stocked na madudu ya enzi hizo!
Hakika hata mimi sikuwa Dar kipindi hicho ila majina yoye hapo juu yalikuwa juu sana!
Hivi DJ JD Matlou amekuja kipindi gani?...au ndo wa juzijuzi?

Unamaanisha John Dilinga?...

Kama ni huyo yeye ni bwa'mdogo mkuu...Alianza kuvuma kati ya mwaka 1996 na 97 nafikiri,yeye pamoja na akina DJ Mike Mhagama,Sos B,Ramkim Ramadhan,Sunday Simba Shomar,Monica Mfumia na wengine waliokuwa Radio One ya enzi hizo
 
Unamaanisha John Dilinga?...

Kama ni huyo yeye ni bwa'mdogo mkuu...Alianza kuvuma kati ya mwaka 1996 na 97 nafikiri,yeye pamoja na akina DJ Mike Mhagama,Sos B,Ramkim Ramadhan,Sunday Simba Shomar,Monica Mfumia na wengine waliokuwa Radio One ya enzi hizo
Mkuu,
Unatisha!. Umenikumbusha Sos Bizzo, ambaye baadaye akatoka na "Kukurukakara Zako Zitakuponza"!
Kiongozi, Una akiba ya kibao cha Wagadugu ya enzi hizo?...Nakumbuka wakati tukiwa form 2 ndo nyimbo hii ilitufanya wengine tupate wapenzi!... ha ha haaa!
 
Hapa je??.......

 
Last edited by a moderator:
Pia kulikuwa na mashindano ya Taifa ya Disco ambayo yalikuwa yakiendeshwa na chama cha Disco Tanzania(TDMA) ambacho kilikuwa chini ya uenyekiti wa Abdulhakim Magomelo(DJ Kim wa Kim & The Boys) na katibu mkuu Samweli Semkuruto.....

Ilikuwa raha sana kuona upinzani mkali miongoni mwa wacheza Disco wetu,na nakumbuka mara nyingi katika mashindano ya Bingwa wa kucheza Disco Taifa upinzani mara nyingi ulikuwa ni kati ya hayati Mussa Simba 'Black Moses' na Bosco Cool J....

Baadhi ya wacheza Disco wengine waliotamba enzi hizo ni pamoja na Athuman Digadiga, Ally Baucha, Samy Cool, Sydney, Huessin Shadrack Guga 'Kokoliko', Kibengo Shaban 'Kadet Bongoman', Savy Pops, Maneno Super Ngedere, Kanda Kid wa Kenya, King Jobiso, Bebe Computer, Sabbah A Jackson, Sammie Cool, Tito Jackson, John Maganga, Bob Richie, Smart Boy, MC Chunusi,Chuchu Lee, Shaba Ranks wa Tanzania, Max Prince/Priest na wengine wengi......

Kwa wacheza Disco wanawake wadada nawakumbuka wachache kama Jessica Ongala, Ashura Mponda 'Queen Clouds', Big Mama, Queen Eliza, Janet Jackson, Homa ya jiji na wengine.............
 
Kitu Careless whisper......

 
Last edited by a moderator:
Kitu hiki hapa chini naweza sema ndicho Asili ya muziki wa Bongofleva,Saleh Jabir alikiimba kwa Kiswahili kitu ambacho kilionekana ni kigeni sana...

Nakumbuka baadhi ya maneno kama 'Kata kata ngoma za kisasa,kata kata hata kwasakwasa kibao ni chako si cha kuazima hata ukiwa mtu mzima'.
'Kitu kimenikaa moyoni sasa naamua kukitoa mdomoni yooo I don't know kusema mengine naona choo'...
'Niko street nataka mic ya umeme niko kweye stage nayakata madebe..............Ice ice baby oooh oooh'.....

 
Last edited by a moderator:
Ingawa mi si wa enzi hizo ila Kwetu sisi wapenzi wa rap/hip hop NWA, a tribe called quest, brand nubian, na arrested development ndo mpango mzima

Hapa najiskilizia eazy duz it na eazy-er said than dun za eazy e; express urself wa NWA, can I kick it na jazz za tribe called quest; na all for one na concerto in x minor za brand nubian. Na jioni yangu yaenda poa hapa gizani
 
Mambo ya Black Box haya........aaaaaah

 
Last edited by a moderator:
Nakumbuka enzi za Cave Disco pale Arusha, kulikuwa na Dj mmoja jina nimeshau ila wengi tulikuwa tumemzoea kwa kusema kuwa ana (Samahani) Makalio Makubwa. Daaahh, jamaa kweli alikuwa kabeba mzinga....

Siku moja niliingia hapo na kusikia hiki kibao.......



Ila wimbo wake uliotamba zaidi ulikuwa ni huu uitwao HIGH LIFE maana ulikuwa karibu kila kona mitaani......

Huyu jamaa (Wally Badarou) kweli alichanganya Miziki ya Ulaya na Beats za Kiafrica alikotokea (BENNIN) na radha ya miziki ya USA/Europe na ndiyo maana alipendwa karibu na kila aliyemsikiliza beats zake.....

 
Last edited by a moderator:

Similar Discussions

Back
Top Bottom