Karibu kwetu tukuyu!

nimeona hlo basi sikutegemea hapo! Umenikumbusha kitu kisondela. Pimba ilisu mwakaleli
 
Duh mkuu umenikumbusha mbali sana
Katumba na kile kiwanda cha chai pale katumba
Chuo cha ualimu pale
Shule ya sekondari Ndembela
Ahhh Tukuyu nitarudi tena kutembelea huko aise
 
Daraja la mungu na Matema beach




 

Attachments

  • matema beach.JPG
    matema beach.JPG
    42.1 KB · Views: 121
  • daraja.JPG
    daraja.JPG
    79.3 KB · Views: 124
menikumbusha Miaka ya mwanzo ya themanini nikiishi Sumbawanga, kuna mzee mmoja alikuwa akilinda nyumba ya mkuu wa mkoa wakati huo ikijengwa, basi katika cheza cheza yetu na sababu tulikuwa tunaishi jirani pale Regional Block tulikuwa tunaingia mle ndani tunamkuta babu wa kinyaki ndo mlinzi pale, jioni hiyo babu kishajikoki na SUTE (pombe ya kienyeji) anatupa story za Tukuyu yeye alikuwa hana meno ya mbele so Tukuyu yeye anatamka TUKUJU, alipenda sana kusema wanangu Tujuku Bulaya wanangu bulaya kabsaaa yaani Tukuyu ulaya wanangu uklaya kabsaaa!
 
Duh mkuu umenikumbusha mbali sana
Katumba na kile kiwanda cha chai pale katumba
Chuo cha ualimu pale
Shule ya sekondari Ndembela
Ahhh Tukuyu nitarudi tena kutembelea huko aise

Ahahahah kuna Bro wangu alisoma TTC hapo tukuyu. alikuwa anatupa story jinsi Rungwe huko wananchi wanayotandikana vipapai. anadai raia huko wakiwa kwenye pombe si ajabu kuona mwenyekiti wa kijiji anatundika koti hewani mkwara huo kwamba hamna anayemuweza, diwani akiona hivyo anavuta mvua inalinyeshea lile koti tuu mpaka linadondoka hahaahaahaahah si mchezo, anasema walikuwa wakienda BTP ni full uoga maana raia wanawafanyizia, usichape mtoto wa mtu.
Kuna sehemu ina mteremko mkali sana na ajali nyingi sana zinatokea aliniambia panaitwa uwanja wa ndege, dah nasikia ni machinjioni hapo malori yanayokwenda Malawi nasikia mengi yanaishia hapo, ni full ajali hilo eneo
 
Halafu nasikia eti hilo beseni zima la ndizi mbivu ni shilingia mia tano tu. Ni kweli wandugu?
 
Halafu nasikia eti hilo beseni zima la ndizi mbivu ni shilingia mia tano tu. Ni kweli wandugu?

Hilo ni kweli kabisa, karibu ndugu. Pia kwa wale wenyeji au wale waliwahisafiri na mabasi ya Kyela, Tukuyu Dar, nani anazikumbuka sambusa za Sisi kwa Sisi? . Jamani zile sambusa bado mimi sijaona kwa sehemu nilizotembea
 
Kumbe watu wa Tukuyu tupo wengi humu. Na mimi nawaongezea hizo
Ndio mupo wengi humu na hasira zenu kwa utawala wa huyu mkweree mnazionesha kwenye thread zenu jinsi alivyowatenga kwasababu ya Mwandosya!

Nasikia mnataka kurudi kwenu Malawi kama banda alivyosema kuwa nyie ni wamalawi!!
 
Umenikumbusha mbali sana hasa hilo basi la njano, linaitwa Sikutegemea ndo tulikuwa tunapanda kwenda Lwangwa, na kwa mbali namuona Songombiya
 
Back
Top Bottom