Karibu Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, Morogoro

Karibu Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, Morogoro

Mbilimbi Mbovu

Senior Member
Joined
May 25, 2015
Posts
185
Reaction score
119
Historia ya Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine inaanza mwana 1965, ambapo kilianzishwa kikiwa Chuo cha Kilimo kilichokuwa kinatoa mafunzo ya kilimo kwa ngazi ya diploma.

SUA.png


Kufuatia kuvunjika kwa kilichokuwa Chuo Kikuu cha Afrika Mashariki na kuanzishwa rasmi kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1970, chuo hiki kilibadilishwa na kuwa Kitivo cha kilimo cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kuanza kutoa Shahada ya Sayansi katika Kilimo.

Mwaka 1974, Kitengo cha Misitu kilianzishwa na hivyo taasisi nzima ikanbadilishwa jina na kuitwa Kitivo cha Kilimo na Misitu. Kufuatia kuanzishwa kwa Shahada ya Sayansi za Tiba ya Mifugo mwaka 1976 pamoja na kuanzishwa kwa kitengo cha Utabibu wa Migugo, jina la taasisi likabadilishwa tena na kuwa Kitivo cha Kilimo, Misitu na Sayansi za Tiba ya Mifugo.

Julai 1 1984, kitivo kilibadilishwa kwa Sheria ya Bunge Na.6 ya mwaka 1984 na kuwa Chuo Kikuu Kamili na kupewa jina la Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine, kikiwa na vitivo vitatu; Kilimo, Misitu na SayansiTiba za Mifugo.

Hadi sasa, chuo kina vitivo vinne; Kitivo cha Kilimo, Kitivo cha Misitu na Uhifadhi, Kitivo cha Sayansitiba za Mifugo na Kitivo cha Sayansi.

s426-k-no



Kwa sasa chuo kina kampasi nne; Kampasi Kuu iliyopo Manispaa ya Morogoro, Kampasi ya Solomon Mahlangu iliyopo Mazimbu, Morogoro, Msitu wa Mafunzo Omolonyi, uliopo Arusha na Pori la Akiba la Mazumbai lililopo Manispaa ya Tanga.

Kwa sasa chuo kinatoa kozi 30 za shahada ya kwanza na kozi 45 za uzamivu.

Kampasi kuu ipo Manispaa ya Morogoro, mwendo mfupi kutoka Stendi Kuu ya Msamvu.

attachment.php


========================================
========================================


The history of Sokoine University of Agriculture dates back to 1965 when it started as an Agricultural College offering diploma training in the discipline of agriculture.

With the dissolution of the
University of East Africa and the consequent establishment of the University of Dar es Salaam (UDSM) in July 1970, the College was transformed into a Faculty of Agriculture of UDSM and thereby started offering Bachelor of Science in Agriculture. In 1974, the Division of Forestry was established and hence the faculty was named Faculty of Agriculture and Forestry.

The introduction of Bachelor of Veterinary Science in 1976 and the establishment of the Division of Veterinary Science, the Faculty was re-named "Faculty of Agriculture, Forestry and Veterinary Sciences". The Faculty was on the 1st of July 1984 transformed, through Parliamentary Act No. 6 of 1984, into a full-fledged University and became known as Sokoine University of Agriculture (SUA) with the Faculty of Agriculture, Faculty of Forestry and Faculty of Veterinary Medicine.

Currently SUA has four faculties namely; the
Faculty of Agriculture (FoA), Faculty of Forestry and Nature Conservation (FoF & NC), Faculty of Veterinary Medicine (FVM) and the Faculty of Science (FoS), the latter which was established in 2001. Other academic units include the Directorate of Research and Postgraduate Studies (DRPGS), Institute of Continuing Education (ICE), Development Studies Institute (DSI), Computer Centre (CC), Pest Management Centre (PMC), SUA Centre for Sustainable Rural Development (SCSRD) and the Sokoine National Agriculture Library (SNAL). SUA also hosts the African Seed Health Centre and Virtual Centre known as "Southern African Centre for Infectious Disease Surveillance".

The university which is located in Morogoro Municipality has 3,350 hectares of land for training, research and production in Morogoro municipality; 840 hectares of forest land in Arusha; 320 hectares of virgin forest for research in Usambara Mountains in Tanga and 500 hectares of miombo woodlands in Kitulanghalo in Morogoro region.

The university has four campuses namely, the Main Campus within Morogoro municipality; Solomon Mashlangu Campus (SMC) in Morogoro municipality; SUA Training Forest (SUATF) Olmotonyi in Arusha region and Mazumbai Forestry Reserve in Tanga region.


SUA's academic business is guided by the university's vision and missions as well as the Corporate Strategic plan (2005-2010), the latter that spells out plans in keeping with university's core missions and functions as well as the need to remain competitive.

The Vision of the university is "is to become a centre of excellence and a valued member of the global academic community in agriculture and other related fields, with emphasis on impacting practical skills, entrepreneurship, research and intergration of basic and applied knowledge in an environmentally friendly manner. ".

The vision is guided through the mission, which is "to Promote development through training, research, extension, provision of services to the public and private sector in an environmentally friendly manner.".

SUA is offering 30 undergraduate and 45 postgraduate degree programmes. It also offers non-degree programmes including Certificates and Diplomas. The University has a total of 7228 student population of which 1553 are postgraduates, 5475 are undergraduate, 152 are diploma and 48 are certificates students. It has a total of 1343 employees, 503 are academic members of staff of whom 58% are PhD holders and 835 are administrative staff of whom 36% are female.

To date, SUA is the only university, amongst 34 universities and university colleges in Tanzania that offers degree programmes in the broad field of agriculture.


SUA's main research objective is to provide leadership in basic and applied research in order to generate science evidence knowledge and innovations that respond to contemporary and emerging needs. SUA thus emphasizes that research becomes linked to development and societal issues. Research, outreach and consultancy services are driven by trained agricultural and natural resource manpower base that comprises 452 academic staff, out whom 50% have PhD qualifications.

Research capacity at SUA is further enhanced through collaborative research projects, which are supported by more than 50 memoranda of understanding. Currently, there are a number of ongoing research projects.

For more information please contact:
The Vice-Chancellor
Sokoine University of Agriculture,
P.O. Box 3000 CHUO KIKUU,
Morogoro, Tanzania
Tel. +256 23 2603511-4,
Fax +255 23 2604573
Email:
vc@suanet.ac.tz
Soma: Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine
 

Attachments

  • sua.png
    sua.png
    176.3 KB · Views: 1,711
Kama kigezo cha umaarufu ingekuwa umri, kwa nini unataka SUA iwe maarufu kama UDSM wakati chuo hicho ni mama yake?

Ukiacha umri, kuna vigezo kadhaa vinavyotumika kimataifa kulinganisha vyuo. Hujadokezo vigezo ulivyovitumia kuonyesha kwamba SUA iko chini ya vyuo ulivyovitaja.
 
Nafikiri hujafanya utafiti wowote kuhusu SUA ila umeamua tu kuandika bila ya kuwa na vigezo vyovyote, kwa muda wa miaka mingi sasa kila inapotolewa rank ya vyuo vikuu africa UDSM huwa inaongoza na SUA huwa inafuatia.

Hivyo vyuo unavyovija wewe huwa havionekani kabisa kwenye rank ya vyuo vikuu africa.
 
Senetor sina hakika kama unaperuzi takwimu na rank mbali mbali ya academic institutions duniani...

kwa kukusaidia tu Unapozungumzia kwenye jukwaa la kimataifa kuhusu vyuo na taasisi za elimu Tanzania utaanza na chuo kikuu cha Dar es Salaam na baadaye Chuo cha kilimo cha Sokoine...

na ukifunua zaidi utagundua kwamba kwa Afrika SUA imesimama sana linapokuja suala la vyou vya kilimo... Fanya utafiti kabla hujaconclude jambo!
 
Nakifahamu vizuri chuo cha Sokoine na ninaweza kufafanua kwa nn mtoa hoja ana wasiwasi na popularity ya hiki chuo midomoni mwa watu.

Kwa ufupi ni kwamba Sokoine ni chuo kikuu cha kilimo na masomo ya Kilimo yana nature ya science ambayo yanaogopwa na watu wengi sana nchini.

Umaarufu wa chuo hiki ni mkubwa sana kitaaluma kwani kina idadi kubwa sana ya maprofesa na madokta ukifananisha na chuo kama Mzumbe na pia kuna researcher wazuri sana pale SUA waliobobea haswa kwenye tafiti za kisayansi Pia walimu wengi wa Mzumbe kwa sasa wanasoma PhD SUA na UDSM kwa hiyo ukiangalia vizuri utagundua kuwa SUA inategemewa sana hata kutoa elimu kwa taasisi nyingine.

Vyuo kama Mzumbe, IFM n.k vinasikika sana kwa kuwa watu wengi ambao ni waoga wa masomo ya science wanakimbilia kule hasa wanawake hivyo utakuta kwa mtu mvivu wa kufikiri anaweza kuona ni vyuo maarufu kwa kuwa kuna watoto wengi wa wakubwa na watu wanaotaka uraisi kimasomo hasa waliopo makazini upendelea sn vyuo hivi Idadi ya PhD holders SUA ni 256 na Mzumbe ni 22 hapo nadhani unapata picha ya ubora wa chuo achilia mbali takwimu iliyotolewa hapo juu ambayo inaonyesha kuwa SUA ni chuo kikubwa tu Africa
 
vyuo kama mzumbe, ifm na iaa sio vya kulinganisha na sua na wala sio maarufu kitaaluma kama sua, labda umaarufu katika mambo mengine yasiyokuwa na msingi ndio sua unaweza jaribu kuilinganisha na ikawa sio maarufu!!!!......ila ukitaka shule nenda sua.
 
kama [RED]mzumbe,ifm na iaa[/RED],je sababu ni kwamba kozi za sua haziuziki sokon,masomo ya sua ni magumu hvo wanafunz weng wanapaogopa au tatizo ni nin na nin kifanyike ili kuifanya sua iwe maarufu kama ilvo udsm?

huwezi kuilinganisha sua na hapo red, linganisha sua na kcmc/bugando
 
  • Thanks
Reactions: Wa3
Ni kweli sua na udsm ni vyuo vizuri sana kwa upande wa vyuo vikuu,vipi taasisi za elimu ya juu kama dar es salaam institute of technology (dit) zamani dar technical college? Mnakionaje chuo hiki?
 
SUA inaheshimika mkuu..kutokuisikia kwako sio kigezo cha kutokuwa chuo bora.
pale ni elimu zaidi mkuu
 
Dark City
Nakumbuka Mazimbu,sitaki hata kukiongelea SUA,kwani nilikuwa pale hususani ktk yale makozi ya engineering na BVM,kuna kipande kinaitwa fucult of science yaani dakika yeyote ile jamaa wanakula kichwa,

anayesema kuwa kozi za SUA hazilipi anajidanya kwa sasa tupo manchi ya watu kwa ajili ya makozi tuliyo yasoma pale SUA,

Ukitaka utamu wa SUA we peleka mtoto wako ama ndugu yako atakupa jibu,

nakifananisha na hivi vyuo nipo sasa nao ni mchaka mchaka

kwa mfano watu wanao soma degree ya kwanza na yapili kwa bongo wanafunzi hawapublish paper zao,lakini hapa ni tofauti sana

sua
ardhi ni hazina
 
Ni kweli sua na udsm ni vyuo vizuri sana kwa upande wa vyuo vikuu,vipi taasisi za elimu ya juu kama dar es salaam institute of technology (dit) zamani dar technical college? Mnakionaje chuo hiki?

Kivipi mkuu?, au unamaana gani? hapa tunazungumzia kwa nini SUA si maarufu wewe unaleta mambo yako ya DIT. any way umaarufu anaoutaka ni kama UDOM kila siku kwenye magazeti ooh jaamaa wamegoma, mara college fulani wamefukuzwa nk, IFM wao ni kwenye skendo mara fulani shoga mara miss katoka IFM pia idadi kubwa ya madenti pale IFM ni MASHALOBALO
 
Kama kigezo cha umaarufu ingekuwa umri, kwa nini unataka SUA iwe maarufu kama UDSM wakati chuo hicho ni mama yake?Ukiacha umri, kuna vigezo kadhaa vinavyotumika kimataifa kulinganisha vyuo. Hujadokezo vigezo ulivyovitumia kuonyesha kwamba SUA iko chini ya vyuo ulivyovitaja.
cjazungumzia ubora mkuu,nimezungumzia umaarufu,mfano..vijana weng wanaomalza kdato cha 6,hukimbilia mzumbe,ifm nk 7bu kubwa ikiwa ni kwamba vyuo hvo ni maarufu au lugha nyingne unaweza kusema vina majina huku mtaani,so swali langu ni kwamba kwa nini sua imezidiwa umaarufu na vyuo vichanga kama mzumbe,ifm na vingne?
 
Huyo anatoka kulala usingizi wa siesta......sijui anatoka wapi.....sua si chuo maarufu??????koz haziuziki??????MIMI SIJASOMA SUA LAKINI NIMEISH CAMPUS ZA SUA KWA MIAKA MING AND MY PARENT WAZ A LECTURER THERE.......
Nafikiri hujafanya utafiti wowote kuhusu SUA ila umeamua tu kuandika bila ya kuwa na vigezo vyovyote, kwa muda wa miaka mingi sasa kila inapotolewa rank ya vyuo vikuu africa UDSM huwa inaongoza na SUA huwa inafuatia. Hivyo vyuo unavyovija wewe huwa havionekani kabisa kwenye rank ya vyuo vikuu africa.
 
Yeah wewe unaijua SUA....asante
Dark CityNakumbuka Mazimbu,sitaki hata kukiongelea SUA,kwani nilikuwa pale hususani ktk yale makozi ya engineering na BVM,kuna kipande kinaitwa fucult of science yaani dakika yeyote ile jamaa wanakula kichwa,anayesema kuwa kozi za SUA hazilipi anajidanya kwa sasa tupo manchi ya watu kwa ajili ya makozi tuliyo yasoma pale SUA,Ukitaka utamu wa SUA we peleka mtoto wako ama ndugu yako atakupa jibu,nakifananisha na hivi vyuo nipo sasa nao ni mchaka mchakakwa mfano watu wanao soma degree ya kwanza na yapili kwa bongo wanafunzi hawapublish paper zao,lakini hapa ni tofauti sanasuaardhi ni hazina
 
Huyo anatoka kulala usingizi wa siesta......sijui anatoka wapi.....sua si chuo maarufu??????koz haziuziki??????MIMI SIJASOMA SUA LAKINI NIMEISH CAMPUS ZA SUA KWA MIAKA MING AND MY PARENT WAZ A LECTURER THERE.......
me nilijua na wewe umesoma sua,kumbe umeishi 2,wacha waliosoma hapo wa argue hii mada na co wewe ulie ishi sua.
 
Sasa wewe ambae hata kupajua hupajui.....unataka umaarufu wa kuvaa vimini.....??????si unakiona ni chuo cha 90 afrika????we unadhan wanabahatisha?????
me nilijua na wewe umesoma sua,kumbe umeishi 2,wacha waliosoma hapo wa argue hii mada na co wewe ulie ishi sua.
 
Sasa wewe ambae hata kupajua hupajui.....unataka umaarufu wa kuvaa vimini.....??????si unakiona ni chuo cha 90 afrika????we unadhan wanabahatisha?????
hiv unajua mwananch wa kawaida wa morogoro anaweza akawa anaijua mzumbe zaidi ya sua mkuu?na hapa siöngelei umaarufu wa kuvaa vimini au vipedo bali nazungumzia umaarufu wa kujulikana miongon mwa watanzania wengi kwa either products zao walzotoa ktk soko au umaarufu wa kozi za chuo husika.
 
me nilijua na wewe umesoma sua,kumbe umeishi 2,wacha waliosoma hapo wa argue hii mada na co wewe ulie ishi sua.

Mkuu labda nikusaidie, vijana wengi wanaomaliza A-level wanakuwa wamesoma michepuo ya Arts na Biashara.. Michepuo hiyo SUA kwa iaka mingi hakukuwa na kozi zake. Pale ni pure science yaani unakuta Veterinary Medicine, Agriculture Engineering, Forestry, Animal Science, Crop Science n.k. Vijana wa siku hizi ukiwaambia wasome hayo ni sawa kuwaambia wapande Mlima Kilimanjaro, hawawezi!! Kila mtu anakimbilia BA, Accounts, Tax etc kwenye hivyo vyuo vyenu uchwara!!

So, kwa mtu asiyeyejua anaona SUA ni chuo cha kishamba!! Mimi nilimaliza UDSM lakini wakati nipo Japan Kagoshima University, ndipo nilipoona umuhimu wa SUA baada ya kukuta wanafunzi wengi wa SUA pale mpaka wa Undergraduate na jinsi jamaa wanavyoshirikiana na SUA katika masuala ya kuendeleza sayansi za kilimo, mifugo na chakula. Imenishawishi kufanya MSc yangu hapa SUA..

SUA NI CHUO MUHIMU SANA KWA MAENDELEO YA TANZANIA NA UMAARAFU WAKE UPO ZAIDI NJE YA NCHI, SIDHANI KAMA HAPO IMF AU CBE UNAWEZA KUTA PROJECTS ZA KIMATAIFA KAMA ZILIZOPO UDSM NA SUA!!
 
Wana umaarufu sana tu na kuna coz pale ni hot cake tu mdaumfano B.A RURAL DEVELOPMENT,INATOKA SUA TU KWA TANZANIA HII,LAKINI KUNA VERTENARY,ENVIRONMENTAL ENGINEERING,AGRICULTURE EXTENSION NDIO INATOA MABWANA NA MABIB SHAMBA,BIO-TECHNOLOGY AND LABORATORY SAYANSI,AGRONOMY N AGRIBIZNESS......FOREST NA KADHALIKA,KUNA BAADH YA ORGANIZATION HATA ZIKITOA NAFAS ZA KAZI HUWA WAZ,WANASEMA WANATAKA MTU KUTOKA SUA.......SO U CAN SEE HOW FAMOUS THEY R......PIA KUNA KOZ MPYA YA TUARIZM MENEJMENT.....NADHAN NDO IMEANZA THIS YR
hiv unajua mwananch wa kawaida wa morogoro anaweza akawa anaijua mzumbe zaidi ya sua mkuu?na hapa siöngelei umaarufu wa kuvaa vimini au vipedo bali nazungumzia umaarufu wa kujulikana miongon mwa watanzania wengi kwa either products zao walzotoa ktk soko au umaarufu wa kozi za chuo husika.
 
Ninachojua mimi SUA ni chuo kizuri, nimeona wengi wanaomaliza chuo hicho wapo karibu kila mahala wanafanya kazi tena nyingi tofauti kabisa na kozi walizosomea , lakini nahisi wanaandaliwa vizuri mbona wanaperfom sana wanafunzi wa SUA, labda jina ndo linapotosha ukweli kuhusu SUA, sio chuo cha Kilimo tu kwani kwa sasa kozi zinazotolewa ni zaidi ya 20 na kozi za kilimo perse hazifiki 10, UDSM inabaki kuwa juu ukilinganisha na SUA hivi vingine vinafuatia
 
Back
Top Bottom