SUA is redundant university! Wanafunzi wanakwenda kusoma kule kama kutimiza wajibu baada ya kumaliza masomo ya Form Six. Hatimaye wakishamaliza waakuta kuwa hayo waliyosoma hayahitajiki kwenye jamii hii ya Ki-Tanzania, na hali hii inapelekea watafute ajira za cheap labour kwenye kazi za fani za biashara.
Mimi sioni mchango wao uko wapi hao munaowaita maprofesa wa SUA wakati nchi iliyojaaliwa ardhi nzuri yenye rutuba kama hii bado sehemu mbalimbali za nchi watu wanakufa kwa njaa kwa sababu ya ukosefu wa chakula. Unaweza kufanya tafiti ya 'Namna Vipepeo wanavyopeana mimba na Kuzaa kwa kutumia vumbivumbi la majani ya kijani" then SUA watakupa PhD lakini utaisaidia vipi nchi hii iondokane na janga lanjaa kwa kutumia tafiti hiyo? Naona watu wanashabikia idadi ya PhD na Maprofesa waliopo SUA lakini wanasahau kuwa wanaofanyakazi huko vijijini ni wahitimu wa ngazi za vyeti katika vyuo vya Uyole, Mpwapwa, Ukiriguru. PhD haina maana kama huwezi kuifanyia vitu ambavyo ni tangible.
Kama degree za SUA ni marketable basi tungewaona wahitimu wao wakijikita katika maeneo yanayoendana na fani zao? Wale Maprofesa wa SUA wako selfish kwani walipaswa waishauri Serikali ibadili jina kutoka Sokoine University of Agriculture na kuwa 'SOKOINE UNIVERSITY" ili chuo kifundishe Agriculture kama kilimo, na kifungue macho kwa kozi zingine ile kiongeze soko kwa wahitimu wake. Mimi nikiwa mwajiri lazima nitampa graduate wa SUA raqw deal katika same position na graduate wa UDSM, IFM au Mzumbe wanapo qualify kufanya kazi kama credit officers kwenye bank