Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 11,866
- 4,260
Imeshakuwa kama kamchezo kwa viongozi mbalimbali kuitumia Kariakoo kama mfano mbaya pale wanapotaka kufananisha na jambo baya
Awali kabisa alikuwa Makamba. Nikaja kumsikia tena jamaa mmoja akiitwa Komba. Yupo PWC kama auditor. likuwa katika kipindi cha kippima joto ijumaa iliyopita-itv. sasa tena huyu mama Makinda. Msiwe kama watu wa Kariakoo. Watu wa Kariakoo ni kina nani hao? Ni wale wanaoishi pale au wale wanaofanya biashara na kununua?
KWa mtazamo wangu, kama Kariakoo isingekuwa sehemu ya biashara basi pagekuwa patulivu sana. Pangekuwa ni makazi tu ya watu hivyo kutokuwa na pilika zilizopo sasa. sasa tatizo ni pale sehemu hiyo kuwa ya kibiashara. kama wewe msomaji hujapita kariakoo leo utapita wiki ijayo. nami kadhalika. Kwa mantiki hiyo wale wa Kariakoo wanaopigiwa mfano na hawa viongozi ni MIMI na WEWE!! sisi ndio watu wa Kariakoo maana ile sehemu ni eneo lisilokwepeka kufika.
Mnakubaliana na hawa waropokaji?
Awali kabisa alikuwa Makamba. Nikaja kumsikia tena jamaa mmoja akiitwa Komba. Yupo PWC kama auditor. likuwa katika kipindi cha kippima joto ijumaa iliyopita-itv. sasa tena huyu mama Makinda. Msiwe kama watu wa Kariakoo. Watu wa Kariakoo ni kina nani hao? Ni wale wanaoishi pale au wale wanaofanya biashara na kununua?
KWa mtazamo wangu, kama Kariakoo isingekuwa sehemu ya biashara basi pagekuwa patulivu sana. Pangekuwa ni makazi tu ya watu hivyo kutokuwa na pilika zilizopo sasa. sasa tatizo ni pale sehemu hiyo kuwa ya kibiashara. kama wewe msomaji hujapita kariakoo leo utapita wiki ijayo. nami kadhalika. Kwa mantiki hiyo wale wa Kariakoo wanaopigiwa mfano na hawa viongozi ni MIMI na WEWE!! sisi ndio watu wa Kariakoo maana ile sehemu ni eneo lisilokwepeka kufika.
Mnakubaliana na hawa waropokaji?