Alikuwepo Askofu Mkuu Oscar Romero; alisimama dhidi ya utawala wa kidikteta na akatoa ujumbe wa kinabii (prophetic message). Alifanya hivyo baada ya mapadre wake kuuawa na utawala dhalimu. Pengo amezoea kukaa katika starehe mno, kula na kunywa na wakubwa na ameacha kusimama kama nabii. Anapenda heshima. Wakati umefika kwa Pengo kuonesha kuwa anastahili cheo alichonacho.
Tunahitaji Oscar Romero wetu... vinginevyo huku tunakokwenda kubaya. Oooh ninavyoogopa kusikia Shehe kauawa; Msidhani haiwezi kutokea au kwamba hawa Wakristu ambao ndani ya wiki moja viongozi wao wawili wameuawa nao wataendelea kukaa kimya..
Pengo... utafanya nini....
Kaka Pengo hausiki hapo, zanzibar ni jimbo na linajitegemea. Labda useme rais wa maaskofu ambaye ni rais wa TEC.
Ila mimi nashauri kwa sasa wakristu wote wasusie kufanya kazi na serikali mpaka itakapohakikisha wote waliousika na dhuluma dhidi ya dini wamechukuliwa hatua na kuhukumiwa.