Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,502
- 911,254
Kapuya huyo ni byebye hata alete JWTZ yote ihamie Kalua haya ni maamuzi ya Yule Aliye Juu...................................Kapuya anatumia ubabe sana, HATAKIWI,
Kapuya huyo ni byebye hata alete JWTZ yote ihamie Kalua haya ni maamuzi ya Yule Aliye Juu...................................Kapuya anatumia ubabe sana, HATAKIWI,
Siwezi kuweka picha mtanisamehe kwa sababu sina kamera. Habari ni za kweli kwa sababu nilikuwepo kwenye tukio. Hadi sasa mgeni yeyote atakiwi kuingia kaliua, akionekana mtu mgeni anakamatwa na kuhojiwa na vyombo vya dola. Pia mwanae na Kapuya aitwae Baraka imebidi atoroshwe kwa sababu wananchi wakimkamata wataua, yeye pia amekuwa katili sana na kundi lake kupiga watu hovyo na kuchukua wake za watu, mwaka jana aliua watu wawili kwa risasi ambapo ilitokea ghasia kubwa sana kama ya wiki jana, lakini vyombo vya dola vikafichaficha kumlinda, hadi sasa huyu Kijana ni WANTED na wananchi. Haijulikana KAPUYA kamkimbizia wapi. Mwaka huu ama zake ama za wananchi, wameapa wanyonge.
Tuchague viongozi wenye tija na machungu na nchi hii tuachene na wanyanyasaji hawaLeo nimepata wasaa wa kuongea kwa kirefu na jamaa yangu anayetokea kijiji cha Vumilia kilicho katikati ya Urambo kwa Samuel Sitta na Kaliua kwa Prof. kapuya kwa kweli huyu Profesa anatumia vibaya madaraka na pesa alizonazo kuwanyanyasa mananchi wa Kaliua waliomfikisha hapo alipo. Jamaa yangu alinieleze jinsi Prof. kapuya na mwanaye Baraka wanavyowanyanyasa wapinzani kwani maji yashawafika shingoni. Wakikuta mikutano ya CHADEMA inafanyika wanawavuruga kwa kutumia polisi na kuwapa vichapo wananchi bila hata huruma. Alieleza kuwa hivi karibuni kuna eneo lililo umbali wa kilometa 64 linalotakiwa kutengwa kama hifadhi ya taifa ambapo askari game walienda na silaha kuwafukuza wananchi wa hapo na ndipo zikatokea vurugu kubwa sana na ikabidi wale askari watumie silaha na waliuua watu zaidi ya 20 na habari hii ikazimwa kimya kimya ila wananchi wa Kaliua wanalifahamu hili fika. Pia mwanaye Baraka yaani yeye ndio yeye huko Kaliua wananchi wananyanyaswa sana na mibangi yake kwani anadiriki hata kuwapiga vibao polisi pindi wanapomsimamisha barabarani na hadi sasa amekwishafanya mauaji ya watu wasio na hatia watatu bila kufanywa chochote. Mwaka juzi alimpiga jamaa mmoja kwenye club yake ya usiku baada ya kutaka kumnyang'anya demu wake jamaa ambaye alikuja kufarika baada ya kulazwa hospitali ya wilaya ya Urambo kwa siku mbili. Kama hiyo haitoshi mwaka jana mwezi September alimuua mwanafunzi aliyekuwa kwenye disco la kumaliza kidato cha nne kwa risasi na ikasingiziwa ni mlinzi wake (yuko ndani hadi sasa). Tukio hilo liliwakasirisha sana wazee wa Kaliua wakamtengeneza jamaa akawa kama chizi, amabapo abbake aliahangaika huku na kule hadi Nigeria kutafuta mganga wa kumtibu na kufanikiwa. Hivi juzi mnamo mwezi July Baraka akitokea ulyankulu kuelekea Tabora alimgonga kwa makusudi mpita njia na kumsababishia kifo pale pale na polisi hawakumfanya kitu.
Hoteli ya Kapuya yashambuliwa, mwanawe chupuchupu
Mtoto wa kapuya na mauaji ya mwanafunzi Tabora
Polisi yamsafisha mtoto wa Kapuya
Sasa nauliza hivi nchi hii wanyonge tutaishia kunyanyaswa hadi lini na wenye madaraka na pesa na je jeshi la polisi linafanya kazi gani kudhibiti wauaaji kama huyu Baraka Kapuya? Iko Siku haya manyanyaso yataisha Inshalllah... Stay tuned more to follow...
I'd rather die as a man than live as a coward -Tupac Amar Shakur (R.I.P)
Picha tafadhali, unajua mkuuu matukio kama haya ndo yenyewe kwanza yatakuweka juu ktk kumbu kumbuzetu za JF hapa jamvini, kwa hiyo kama una picha za kash kash hizo weka picha hizo hapa. Ahsante kwa taarifa, kapuya hatakiwi muda mwingi sana, apumzike huyo mzee ndo aliyefanya mitihani ya Form Four 1998 ikaliki vibaya sana.
Picha tafadhali, unajua mkuuu matukio kama haya ndo yenyewe kwanza yatakuweka juu ktk kumbu kumbuzetu za JF hapa jamvini, kwa hiyo kama una picha za kash kash hizo weka picha hizo hapa. Ahsante kwa taarifa, kapuya hatakiwi muda mwingi sana, apumzike huyo mzee ndo aliyefanya mitihani ya Form Four 1998 ikaliki vibaya sana.
Du....Yaani kwako wewe hili tukio ndio lenyewe na linafaa kushabikiwa.........
Eh Mungu wa Watanzania wote endelea kutuona kwa jicho huruma na upendo uliotuonyesha miaka yote hii 48......hata kama tu watenda madhambi wakubwa...
Ni kweli kabisa,hata mimi nimeongea na jamaa yangu ambaye yupo huko na kaniambia fujo hizo zilitokea tarehe 11
Naam,
nimethibitisha kwamba Kapuya "Out"!
nimeongea na mtu anayefanya kazi halmashauri ya Urambo anadai huko Kaliua watu wana hasira sana na utendaji wa Kapuya, maneno yake machafu, pamoja na kwamba baada ya uchaguzi watahamishiwa mkoa mpya wa Katavi kinyume na matakwa yao. kwa hiyo ghafula CUF wamedondokewa na Zali la mentali
Hatuhutaji viongozi wa namna hii nchi hii WANANCHi wa Kaliua tusaidieni hili kwa kumnyima kura huyu jamaa mnyanyasajiHuyo Kapuya ni ahaji wa ajabu sana, alhaji mwenye bendi ya muziki, klabu za usiku, baa! Huyu haa mungu hamwogopi. Ananyumba pale urambo mjini karibi na benki, akiwa hapo kazi moja tu, wanawake mpaka jua lina tua! kiwa hapo anendesha majungu na masihara kuhusu mpira! Awamu ya kwanza alipokuwa Waziri wa Kazi kulikuwa na mradi wa ILO wa kutokomeza ajira za watoto kwenye zao la tumbaku, yeye kazi yake ilikuwa kupeleka mradi kwenye jimbo lake na kukataza mradi usifanye kazi kwenye jimbo liliokuwa chini ya CUF bila kujali ahari kwa watoto. Utafikiri kuna watoto wa CCM na watoto wa CUF! Alikuwa anajua baadhi ya maofisa wilayani wamejiundia NGO zao ili zipate hela za ILO lakini kwa kuwa walikuwa wanashabikia CCM hakuingilia. Hela za ILO zikaliwa na hata leo ukienda Urambo ajira ya watoto kama kazi!
Usione amevaa kanzu au joho la hija, shetwani mkubwaa yule!
mgombea ubunge wa urambo magharibi kupitia ccm prof. Juma kapuya ana hali ngumu sana katika jimbo la kaliua, hali ambayo imemlazim kutegemea vyombo vya dola kudhibiti wapinzani. Hakika wananchi hawamtaki kabisa kutokana na tabia ya wafuasi wake kuwapiga wananchi wanapouliza maswali magum kwenye mikutano yake ya kampeni, kwa madai kuwa wananchi hao eti wametumwa. Wiki jana imetokea fujo kubwa sana kaliua baada ya kijana mmoja kuuliza swali gumu, ambapo kapuya aliposhindwa kujibu alimtukana "******" ndipo wananchi wakachachamaa na kuanzisha fujo kubwa, polisi wa kaliua wakapiga risasi zaidi ya 10 hewani lakini wapi, ikabidi waombe msaada polisi urambo, nao wakaenda wakapiga mabomu na risasi zaidi ya 30 kutisha watu, wananchi wakatawanyika, ikawa sasa mtu yeyote anayeonekana amevaa nguo za ccm ni kichapo tu, hali iliyopelekea watu kutembea vifua wazi kwa usalama wakati wanaelekea makwao, jana yamepita magari ya jeshi(jwtz) yanaenda kaliua, hali ya hatari imetangazwa hapa kaliua, mwisho wa kutembea ni saa mbili usiku, ukikamatwa unawekwa ndani, kapuya anatumia ubabe sana, hatakiwi, anaetakiwa ni mgombea wa cuf anayeitwa kirungi. Hivi jamani hii ni haki?