Kapteni Tesha alipotelea wapi?

Kapteni Tesha alipotelea wapi?

1765081173580.jpg

Kwenye suala la captain Tesha na reactions za Watanzania ndipo nikahitimisha kuwa Watanzania zaidi ya 80% ni Matahira.
Yaani mwanakwaya wa Gwajima polisi jamii ambaye hata mafunzo ya jeshi hajapata akajivika uhusika wa mjeshi tena afisa kabisa na Watanzania wakaamini.
Ile video yenyewe tu inaonyesha ni mchezo mchafu.
Kofia ya mtumbani wakaweka bakoni kwa cherehani ya uswazi.
 
Unauliza swali la kijinga alafu unajiona smart.
Sasa wewe unategemea afanye nini sasa akiwa peke yake?
 
Tatizo la approach yako ni kwamba unashambulia watu waliomuamini Captain Tesha badala ya kuchambua mazingira yaliyomfanya ajitokeze na kutoa kauli ile.

Hii ni logical fallacy ya ad hominem, badala ya kushughulika na hoja, unashambulia watu binafsi.

Captain Tesha alifanya jambo la kipekee na la ujasiri.

Kumbuka Tesha alitumia jina lake halisi, hakujificha, na alitoa ujumbe wa matumaini kwa wananchi waliokuwa wamekata tamaa kutokana na matukio ya utekaji na mauaji.

Katika mazingira ambayo kusema ukweli kunaweza kukugharimu uhai wako, kitendo cha kujitokeza hadharani ni cha kuenziwa.

Kutorudi tena hakumaanishi alidanganya, kuna sababu nyingi za msingi zinazoweza kumfanya ashindwe kurudi, ikiwemo vitisho kwa familia yake au shinikizo kutoka vyombo vya dola.

Hizi ni sababu ambazo mtu yeyote mwenye akili timamu anaweza kuelewa.

Ni rahisi kwako kubeza ukiwa salama nyuma ya fake ID, bila sura, bila jina, na bila familia yako kujulikana.

Lakini ni vigumu kujitokeza hadharani na kupaza sauti dhidi ya utawala unaotumia nguvu.

Mwa hiyo kubeza jitihada za Tesha naona ni unafiki kwa sababu hujafanya hata nusu ya kile alichothubutu kufanya.

Tesha ali play part yake na alitoa mchango wake wa kipekee na tunamshukuru kwa hilo kwasababu sio wote wanaweza.

Hata kama hakurudi mara ya pili, sababu zake zinaweza kuwa nzito na za msingi.

Halafu hoja yako kwamba “mapinduzi hayatangazwi kabla” haina mashiko kwa sababu historia imetuonesha mara nyingi watu waliotoa onyo au kauli za matumaini kabla ya mabadiliko makubwa.

Thomas Sankara alitoa hotuba kali kabla ya mapinduzi ya Burkina Faso, Martin Luther King Jr. alitangaza ndoto ya “I Have a Dream” kabla ya mabadiliko ya kisheria kutokea Marekani. Kauli za onyo na matumaini mara nyingi hutangulia vitendo.

Kwa hiyo, Tesha kutoa onyo hakumfanyi awe muongo, bali ni sehemu ya harakati za kuamsha hamasa na fikra za wananchi.

Hapa hoja yenye mantiki ni kwamba Tesha alitoa mchango wake na raia wengi wana appreciate so kubeza jitihada zake ni kupuuza mazingira halisi ya gharama za kisiasa katika jamii.
Umeandika vema sana kaka.
 
Hiyo miaka miwili mbona midogo, watu waneshikiwa akili kwa miaka kama 6,000 na zaidi kuhusu mambo ya dini na Mungu na mpaka leo hawajastuka, ukiwaeleza ukweli wanakuwa wakali sana kutetea uongo wao.

Sasa tofauti ya issue ya Kinje na imani za dini ni ipi?

Tena hiyo ya Kinje ina ngivu zaidi kwa sababu adui mnamuona huyu Mjerumani, vita mnapigana hapahapa hamsubiri pepo.

Do not underestimate the stupidity of the general population.
Mkuu kama ile vita ingekuwq jinsi tunavyohadithiwa amini mwezi mmoja ulitosha vijana kutoroka ama kujisalimisha. Kumbuka risasi ikikugusa kichwa ama kifua au sehemu yoyote ile lazima udhurike. Iweje vijana wapigwe risasi na bado wawe na morali yakupambana? Ama walikuwa wengi kiasi gani.
 
Well, well, well……

Tulibezwa na kutukanwa sana sisi ambao tulimtilia mashaka yule mtu aliyejiita Kapteni Tesha.

Tuliitwa kila aina ya majina isipokuwa jina la mwana wa mungu.

Miezi kadhaa imepita sasa tokea ajitokeze na tokea Watanzania wachinjwe na risasi za Samia lakini huyo Kapteni Tesha hajatoa hata katamko ka kulaani mauaji.

Haikuhitaji mtu uwe mwanachama wa Mensa kujua kuwa huyo Kapteni alikuwa ni magumashi tu.

Huwezi kutoa onyo kwa mtawala yeyote yule kuwa eti asipobadilika basi utampindua halafu ukaendelea na mambo yako kama kawaida.

Mapinduzi huwa hayatangazwi kabla. Yanatangazwa yakishatokea.

Nacheka sana, tena kwa dharau nyingi, kuona kuna watu walidanganyika kirahisi namna ile.

Mambo kama hayo ndo hutenganisha wale wenye akili na busara na wale waongozwao na hisia [wasio na akili].

Hongera Kapteni Tesha [kama bado uko hai] kwa kujipatia umaarufu wa dakika 15.

Ajaye sijui atajiita nani? Luteni Kanali Matondo?

😀
Samia anaeza likabili jeshi zima pekee akiwa nje ya system?
 
Kipindi kile palilua moto,alitengenezwa ili wajue jeshini hali ipoje na kuwaangamiza wote watakosaliti.
Ile alikua chambo kuwabaini watakaosapoti na wasio na utii na amiri jeshi mkuu.. Ndio maana Mange alijiamini sana kua Jeshini kuna TAgi mara ghafla Tesha huyo katokea. Kumbe Tesha haluja kwa ajili yetu,alikua kuwanasa wasaliti jeshini.
 
Back
Top Bottom