Kanisa lamuandalia tuzo Lowassa

Kanisa lamuandalia tuzo Lowassa

.
Kuna neno limemisi, "Kanisa ni Moja Tuu, Takatifu Katoliki La Mitume!'.

Alianza TB Joshua, sasa yanafuatia makanisa haya madogo madogo, itafuatia misikiti, the by 2014 lifuatia Anglican, Mid 2015 Lutheran, October, 2015 ndipo itakuwa zamu ya lile Kanisa ni Moja Tuu, Takatifu Katoliki La Mitume!.
Japo yeye ni sauti tuu ya mtu aliye nyikani, Mungu Baba ataudhihirisha utukufu wake kupitia kwayo, kwa "jiwe walilolikataa waashi, litafanywa kuwa jiwe kuu la pembeni!", na litatimie lile neno "Wewe ni mwamba, na juu ya mwamba huu nitalijenga taifa langu!".
Kwa wale ambao ni wabishi kuliko Tomaso wakidhani kuna mambo ambayo hayawezekani!, nawahakikishia "nothing is impossible under the sun!" na "lisilowezekana kwa binadamu, kwa Mungu, linawezekana!".
Pasco.

futa hiyo kauli yako hapo kwenye red. mungu wa misikitini hapendi hela za dhulma. na huo msikiti utakaothubutu kama sio muhanga basi bakora zitahusika.
 
El hamia misikitini sasa kwa kuchangisha fedha kwa ajili ya hospital ya kisasa ya waislam!ili upate kura kila upande

wewe kweli bongolala! Unataka hospitali ya waislam ina maana kuna dawa ambazo zinaponya waislam pekee na haziponyi watu wengine? Biolojia yako umeisomea wapi ndugu? Au ndio udini umeshakuharibu mbona huko nyuma hukuwa hivi?
 
futa hiyo kauli yako hapo kwenye red. mungu wa misikitini hapendi hela za dhulma. na huo msikiti utakaothubutu kama sio muhanga basi bakora zitahusika.

Mmmh! Huyo mungu wa misikiti yukoje aisee?! Lazima atakuwa anatisha mbaya!
 
Mmmh! Huyo mungu wa misikiti yukoje aisee?! Lazima atakuwa anatisha mbaya!

anatisha kweli kweli na hasa pale watu wanapofanya makosa. soma historia za kina kaumu lutu, sodomizers kilichowakuta. uliza kilichomkuta firauni na kajeshi kake juu ya musa, soma watu wa nabii nuhu yaliyowakota. utaelewa kuwa mungu huyo anatisha katika level isiyoelezeka.
 
kuna tofauti gani kati ya kanisa na dhehebu???

KANISA ni nyumba ya ibada kwa wakristo wote. Na kwa waislamu nyumba ya swala ni msikiti. kwa wengine nyumba za ibada zinaitwa sinagogi au temple. KANISA = MSIKITI.

Dhehebu ni mgawanyiko wa makundi katika IMANI za dini zote, ukristo ni kama vile katoriki, KKKT, Sabato (SDA), Moravian na Assemblies of God. Na kwa waislamu Dhehebu ni kama vile Suni, shia, bohora, ismailia, answa sunna na ahamadya.
 
futa hiyo kauli yako hapo kwenye red. mungu wa misikitini hapendi hela za dhulma. na huo msikiti utakaothubutu kama sio muhanga basi bakora zitahusika.
. Kumbe kuna mungu wa misikitini?!, kwa uelewa wangu, nilidhania Mungu ni mmoja tuu ila majina ndio tofauti!. Kwa vile kuna Mungu na mungu, then nakukubalia mungu wa misikitini hapendi hela za dhulma. Kwa Mungu, pesa ni pesa tuu zikifanya jambo jema au jambo la kheri, zinaleta heri na thawabu zinapatikanika!.

Pasco.
 
Anajitolea kwenye mambo yapi ya kijamiii? Kujenga makanisa? Wakristo mumekuwa niwatu wa kukwamisha harakati kila siku. Aiwezekani kwa jitu kama hili (fisadi) kupewa tuzo ya heshima.

Kama LOWASSA angekuwa mchafu mpaka sasa asingekuwa ndani ya CCM. Kanisa haliwezi kumwadhibu Lowassa kwa niaba ya CCM.

Lowassa amefanya harambee mbalimbali za misikitini pia.

Tuachane na siasa chafu za kulitupia mzigo kanisa kwa makosa ambayo bado hayajatolewa hukumu ya kisiasa.
 
KANISA la Overcomers lililopo mkoani Iringa, limeandaa tuzo maalumu kwa ajili ya kumtunuku Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa, kutokana na mchango wake alioutoa katika jamii.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Askofu Mkuu wa kanisa hilo, Dk. Boaz Sollo, alisema jamii ya wakazi wa Mkoa wa Iringa inatambua mchango wa Lowassa ambaye pia ni Mbunge wa Monduli.

Dk. Sollo alisema kuwa tuzo hiyo itampa moyo wa kuendelea kushiriki zaidi katika shughuli mbalimbali za kijamii sambamba na kuiendeleza injili kama ambavyo amekuwa akifanya.

“Hii tuzo itamuongezea ujasiri wa kujituma katika kuisaidia jamii, sambamba na kuchangia ujenzi wa makanisa katika mikoa mbalimbali bila kujali wanaomkatisha tamaa ili kumrudisha nyuma.

“Tumeandaa tuzo maalumu kwa ajili ya kiongozi huyu ambaye haipiti wiki moja anasikika akifanya kazi za kijamii, habagui, hachagui na wala hana upendeleo,” alisema Dk. Sollo.

Aliongeza kuwa tangu alipojiuzulu uwaziri mkuu, hajawahi kuutembelea mkoa huo jambo linalowafanya wakazi wa mkoa huo kuwa na hamu ya kumuona kutokana na jitihada zake za kujihusisha katika masuala ya kijamii.

Alisema tuzo hiyo itatolewa mwezi ujao wakati wa harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa hilo na kituo cha redio ya dini ya Overcomers, ambayo ni maarufu kwa mikoa ya kusini.

Wakizungumza na MTANZANIA kuhusu tuzo hiyo, baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Iringa wamelipongeza kanisa hilo kwa kuandaa tuzo maalumu kwa ajili ya kutambua mchango wa kiongozi huyo.

CHANZO: Mtanzania
Nivizuri kutambua michango ya wadau mbalimbali katika kutatua matatizo ya jamii zetu nakupongeza sana kwa wazo hilo zuri.
 
anatisha kweli kweli na hasa pale watu wanapofanya makosa. soma historia za kina kaumu lutu, sodomizers kilichowakuta. uliza kilichomkuta firauni na kajeshi kake juu ya musa, soma watu wa nabii nuhu yaliyowakota. utaelewa kuwa mungu huyo anatisha katika level isiyoelezeka.
Mkuu, utakuwa umemchanganya Mungu na mungu!, huyo unayemzunguzia ni Mungu Baba, ambaye ndie Mungu muumba wa Adam na Eva (Hawa), ndiye Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakabo, ndiye Mungu wa Nuhu, ndiye Mungu aliyeiteketeza Sodoma na Gomora, ndiye Mungu wa Mussa, huyo mungu unaemzungumzia wewe ni mwingine, ila pia nakubaliana na wewe kuwa mungu huyo pia anatisha!, maana mambo yake sio tuu tunayasikia, mengine tunayashuhudia yakihubiriwa na kuona matokea ya mahubiri hayo!.

Pasco.
 
SIJAONA KOSA LA LOWASSA kuturudishia kidogo kidogo fedha zetu za RICHMOND kama ni kweli aliiba kama wasemavyo wengeni. HERI MWIZI anayerejesha fedha kwa jamii yetu kuliko aliyezificha uswiss.
 
futa hiyo kauli yako hapo kwenye red. mungu wa misikitini hapendi hela za dhulma. na huo msikiti utakaothubutu kama sio muhanga basi bakora zitahusika.


wewe si mtu wa kufuatilia matukio Lowassa ameripotiwa kufika misikitini kuchangisha fedha za harambee ingawa ni kwa uchache ikilinganishwa na makanisani. Tukumbuke tu kuwa Lowassa hajialiki bali anapewa mwaliko (hualikwa) hatuna sababu ya kumlaumu anapoitikia wito huo, ni mara nyingi anaalikwa kwenye harambee za makanisani kuliko misikitini
 
. Kumbe kuna mungu wa misikitini?!, kwa uelewa wangu, nilidhania Mungu ni mmoja tuu ila majina ndio tofauti!. Kwa vile kuna Mungu na mungu, then nakukubalia mungu wa misikitini hapendi hela za dhulma. Kwa Mungu, pesa ni pesa tuu zikifanya jambo jema au jambo la kheri, zinaleta heri na thawabu zinapatikanika!.

Pasco.
na maanisha mungu anayeabudiwa misikitini, hapendi hela za dhulma. kumbuka hata hela ya riba hairuhusiwi kutumika misikitini sebuse hizo za akina lowassa walizotuibiwa mcha peupe? tunajua pasco umeshadakishwa chako ndo maana kila siku unachonga humu toward lowassa.
 
Mkuu, utakuwa umemchanganya Mungu na mungu!, huyo unayemzunguzia ni Mungu Baba, ambaye ndie Mungu muumba wa Adam na Eva (Hawa), ndiye Mungu wa Ibrahim, Isaka na Yakabo, ndiye Mungu wa Nuhu, ndiye Mungu aliyeiteketeza Sodoma na Gomora, ndiye Mungu wa Mussa, huyo mungu unaemzungumzia wewe ni mwingine, ila pia nakubaliana na wewe kuwa mungu huyo pia anatisha!, maana mambo yake sio tuu tunayasikia, mengine tunayashuhudia yakihubiriwa na kuona matokea ya mahubiri hayo!.

Pasco.

pasco acha kutwist post yangu. iache kama ilivyo. wewe tunajua umeshadakiswhwa chako na lowassa. na sasa hivi lowasa yuko bise makanisani kugawa hela za dhulma. unataka uniambie Mungu wa akina nabii Ibrahim (AS), Lutu(AS), Issa bun Maryam(AS), yahaya(AS), Isihaka(AS), Yacubu(AS), Mohammad (saw), Ismail(AS), Idris (AS), Adam(AS) na wanaofanania na hao wanapenda hela za dhulma? kama hizo hela za akila lowassa zimekulewesha tafadhali usimshirikishe mungu. na hakika madhalimu watauona moto mkali uunguzao. Just a matter of time.
 
wewe si mtu wa kufuatilia matukio Lowassa ameripotiwa kufika misikitini kuchangisha fedha za harambee ingawa ni kwa uchache ikilinganishwa na makanisani. Tukumbuke tu kuwa Lowassa hajialiki bali anapewa mwaliko (hualikwa) hatuna sababu ya kumlaumu anapoitikia wito huo, ni mara nyingi anaalikwa kwenye harambee za makanisani kuliko misikitini
nitajie angalau msikiti mmoja. halafu kwanini yeye tu? hivi huwezi kujiuliza hilo swali? mbona sijasikia akina sitta, mwakyembe na wengineo wakialikwa?
 
pasco acha kutwist post yangu. iache kama ilivyo. wewe tunajua umeshadakiswhwa chako na lowassa. na sasa hivi lowasa yuko bise makanisani kugawa hela za dhulma. unataka uniambie Mungu wa akina nabii Ibrahim (AS), Lutu(AS), Issa bun Maryam(AS), yahaya(AS), Isihaka(AS), Yacubu(AS), Mohammad (saw), Ismail(AS), Idris (AS), Adam(AS) na wanaofanania na hao wanapenda hela za dhulma? kama hizo hela za akila lowassa zimekulewesha tafadhali usimshirikishe mungu. na hakika madhalimu watauona moto mkali uunguzao. Just a matter of time.
Mkuu Gudi, utakuwa umemchanganya Mungu na mungu!.
P.
 
Mkuu Gudi, utakuwa umemchanganya Mungu na mungu!.
P.
Mimi naongelea Mungu (Allah aliyetukuka) muumba vyote vilivyopo duniani na mbinguni vikiwemo viumbe VIOVU. pasco najua wewe una miungu. mara roho, mara mwana mara baba. anyway huchelewi kusema nakukashifu. kwaheri.
 
and what is wrong with that???
nani asiyefukuzia mshiko hapa duniani?
kama ni mkakati wao ili nao wasaidiwe na lowasa, i think its genius!
get over yourself..
 
Makasisi wetu na sadaka zilizojaa damu.
 
mwaka 2015 patachimbika lowasa(lutheran),slaa(katoliki)..lipumba(islam) sasa ivi kila mtanzania achague mtu wa dini na dhehebu lake tuone nani atakuwa mshindi
 
Back
Top Bottom