KalamuTena
JF-Expert Member
- Jul 7, 2018
- 13,189
- 17,157
Huna hata aibu.Ungekua na akili nzuri ungekuja na takwimu hapa utuambie msongamano katika masoko ya kariakoo, tandika na ilala umepelekea maambukizi kiasi gani na vifo kiasi gani.
Yaani kwa akili zako ndogo unataka kulazimisha kwamba watu huko masokoni wanakufa sana sana lakini wenzao kila siku wanaenda tena bila tahadhari ili na wao wafe?
Kuandikaandika tuu bila kuwa na takwimu ni sawa na kuimba taarabu tuu, na mtu yoyote mwenye akili nzuri zaidi atachukulia maneno yako kama umbea na majungu yaliyojaa chuki kwa maslahi yako binafsi.
Chukua tahadhari, kula vizuri, fanya mazoezi, mwombe Mungu sana sana kama wanavyofanya wenzio
Takwimu tangu lini unaowatetea wakazipenda?
Halafu usivyokuwa na akili, hujui kwamba hilo unalovimbishia shingo ndilo serikali ingekuwa mbele kabisa kulitimiza ili takwimu ziwepo za kutetea msimamo wake? Wewe hata hujui wajibu wa serikali ni nini?
Ngoja nikuulize tena. Serikali ikihimiza watu wajikinge kwa kuepuka misongamano na kufanya yanayojulikana kusitisha uenezi wa magonjwa wa milipuko, ikifanya hivyo watu hao watakuwa wamepungukiwa na kitu gani?
Unataka takwimu? Hizo zako za kuonyesha kwamba hakuna maambukizi yanaendelea kwa kasi kwenye mikusanyiko hiyo ziko wapi?
Nimekupa fursa nzuri ya kujieleza nilipokupa hoja rahisi uijibu, lakini kwa kuwa kichwani huna kitu unaona bora ujipigie pigie tu kivyako.
Usidhani "tunaandika andika hapa bila kujua tunachoandika, ila tunaowaandikia ili kuwastua serikali iliyotelekeza jukumu lake kwa wananchi na kuwatuma vilaza kama wewe hapa kuja hapa kutwa kupindisha mambo yaliyo wazi..., inasikitisha sana.